1Mufalme Ahasuero alipotawala ufalme wake ulikuwa na majimbo mia moja makumi mbili na saba, toka Uhindi mpaka Etiopia.
2Kiti chake cha kifalme kilikuwa katika muji mukubwa Susani.
3Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, mufalme Ahasuero akaandaa karamu kwa ajili ya viongozi na watumishi wake wa serikali, wakubwa wa majeshi ya Persia na Media, watu wenye heshima na wakubwa wa majimbo.
4Basi, kwa muda wa miezi sita, Ahasuero akaonyesha utajiri wa ufalme wake mutukufu, na sifa ya utawala wake.
5Muda ule ulipomalizika, mufalme aliandaa karamu kwa ajili ya watu wote wa muji mukubwa wa Susani, wakubwa kwa wadogo. Karamu hiyo iliyokamata muda wa siku saba, ilifanyika ndani ya kiwanja, katika bustani ya nyumba ya kifalme.
6Pahali pale kulikuwa kumepambwa kwa mapazia ya pamba ya rangi nyeupe na vitambaa vya rangi ya samawi. Mapazia hayo yalikuwa yamefungiwa pete za feza kwa kamba za kitani safi nyekundu-nyeusi, na kutundikwa kwenye nguzo za mawe ya marimari. Viti vya zahabu na feza vilikuwa vimewekwa kwenye sakafu iliyotengenezwa kwa mawe ya rangi ya marimari, nyekundu, nyeusi, manjano na nyeusi.
7Watu walipewa vinywaji katika vikombe mbalimbali vya zahabu. Na divai ya kifalme ilikuwa nyingi sawa mapato ya mufalme.
8Kila mutu alikunywa sawa vile alivyotaka; mufalme alikuwa ametoa maagizo kwa watumishi wa nyumba ya kifalme wamutendee kila mutu kadiri ya mahitaji yake.
9Wakati uleule, malkia Vashiti naye akawaandalia wanawake karamu ndani ya nyumba ya kifalme ya Ahasuero.
10Siku ya saba ya karamu hiyo, mufalme Ahasuero akiwa amejaa furaha kutokana na divai aliyokuwa amekunywa, akawaita matowashi saba waliomutumikia yeye mwenyewe: Mehumani, Bizita, Harbona, Bigita, Abagita, Zetari na Karkasi.
11Akawaamuru hao wamuletee malkia Vashiti, akiwa amevaa taji yake ya kimalkia. Malkia yule alikuwa na sura nzuri sana, hivyo mufalme alitaka kuwaonyesha wageni wake na viongozi uzuri wake.
12Lakini Vashiti akakataa kufika kwa amri mufalme aliyotoa kwa njia ya matowashi. Kwa hiyo, mufalme akakasirika sana na hasira yake ikawaka.
13Ilikuwa desturi ya mufalme kupata mashauri kutoka kwa wenye hekima, hivyo akawaita wanasheria na waamuzi kusudi wamushaurie la kufanya.
14Washauri wake wa kawaida walikuwa Karsena, Setari, Adimata, Tarsisi, Maresi, Marsena na Memukani – viongozi saba wa Persia na Media waliokuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.
15Akawauliza hivi: “Kulingana na sheria, malkia Vashiti afanyiwe nini? Maana, nimewatuma matowashi wangu kwake, lakini yeye amekataa kuitii amri yangu, mimi mufalme Ahasuero!”
16Hapo Memukani akamwambia mufalme na viongozi wake: “Zaidi ya kumukosea mufalme, malkia Vashiti amewakosea viongozi na kila mutu katika majimbo ya mufalme Ahasuero!
17Tendo hili la malkia Vashiti litajulikana na wanawake wote, nao watawazarau waume zao, wakisema: ‘Mufalme Ahasuero aliamuru malkia Vashiti akuje kwake, lakini yeye akakataa.’
18Leo hii, wanawake wa Persia na Media ambao wamesikia jinsi malkia Vashiti alivyofanya, watakuwa wanawaelezea viongozi wako; hivyo mazarau na chuki vitajaa kila pahali.
19Basi, ikikupendeza, ewe mufalme, toa amri kwamba Vashiti asikuje tena mbele yako. Amri hiyo iandikwe katika sheria za Persia na Media, kusudi isiweze kubadilishwa. Kisha, cheo chake cha umalkia, kipewe kwa mwanamuke mwingine anayekuwa bora zaidi kuliko yeye.
20Amri hiyo itakapotangazwa katika eneo lote la utawala wako, kila mwanamuke atamuheshimu mume wake, akuwe tajiri au masikini.”
21Wazo hilo likamupendeza sana mufalme na viongozi wake, akatimiza sawa vile Memukani alivyopendekeza.
22Basi, akapeleka barua kwa kila jimbo kwa luga na maandiko yanayoeleweka katika jimbo: kwamba kila mwanaume akuwe bwana wa nyumba yake, na kuitangaza habari hii kwa luga yake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.