Yoshua 8 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Muji wa Ai unatekwa

1Yawe akamwambia Yoshua: “Usiogope, wala usikuwe na wasiwasi wowote; uwatwae waaskari wako wote uelekee muji wa Ai, maana nimetia mufalme wa Ai katika mikono yako, pamoja na watu wake, muji wake na inchi yake.

2Mutautendea muji wa Ai pamoja na mufalme wake kama vile mulivyoutendea muji wa Yeriko pamoja na mufalme wake. Mali zake pamoja na nyama wake mutakayoteka itakuwa ni mali yenu. Muende muushambulie muji kutoka upande wa nyuma.”

3Basi, Yoshua akaondoka, pamoja na waaskari wake wote kwenda Ai. Akawachagua watu hodari elfu makumi tatu na kuwaambia watangulie wakati wa usiku.

4Akawaamuru hivi: “Ninyi mutauvizia muji kutoka upande wa nyuma. Musiende mbali na muji, lakini mukuwe tayari wakati wote.

5Mimi, pamoja na watu wote wanaokuwa pamoja nami, tutaukaribia muji. Watakapotoka inje kuja kutushambulia kama pale mbele, sisi tutawakimbia.

6Nao wataendelea kutufuatilia mpaka wakuwe mbali na muji wao, maana watafikiri kwamba wanatukimbiza kama vile walivyofanya mbele. Sisi tutawaacha watufukuze.

7Hapo, ninyi mutatokea kutoka kule mulikokuwa munavizia na kuuteka muji, maana Yawe, Mungu wenu, atautia muji huo katika mikono yenu.

8Mukisha kuteka muji mutauteketeza kwa moto, kama vile Yawe alivyoamuru. Hayo ndiyo maagizo mutakayofuata.”

9Basi, Yoshua akawaambia waende pahali pao pa kuvizia; nao wakajiweka upande wa magaribi wa muji wa Ai, kati ya muji wa Ai na Beteli. Lakini Yoshua akalala usiku huo katika kambi ya Waisraeli.

10Yoshua akaamuka asubui mapema, akawakusanya Waisraeli na kuelekea katika muji wa Ai, akiwa pamoja na wazee.

11Waaskari wote waliofuatana naye walikaribia muji na kupiga kambi upande wake wa kaskazini, ngambo ya bonde kuelekeana na muji wa Ai.

12Halafu akatwaa watu wengine elfu tano na kuwaweka wavizie kati ya muji wa Beteli na Ai, upande wa magaribi wa muji wa Ai.

13Kundi kubwa liliwekwa upande wa kaskazini wa muji na wale waliobaki waliwekwa upande wa magaribi wa muji. Lakini usiku ule, Yoshua akalala katika bonde.

14Mufalme wa muji wa Ai alipoona hivyo, alifanya haraka na kwenda kwenye muteremuko wa kuelekea Araba kwa kushambulia Waisraeli katika vita. Lakini hakujua kwamba muji wake ulikuwa umeviziwa kutoka nyuma.

15Kisha Yoshua pamoja na watu wake wakajifanya sawa wenye kushindwa, wakaanza kukimbia kuelekea katika jangwa.

16Watu wote waliokuwa katika muji wakaitwa wawafuatilie Waisraeli; na walipokuwa wanamufuatilia Yoshua, walitoka na kwenda mbali na muji wao.

17Hakuna mutu yeyote aliyebaki katika muji wa Ai, waliuacha muji ule wazi wakaenda kuwafuatilia Waisraeli.

18Halafu Yawe akamwambia Yoshua: “Elekeza mukuki wako kule katika muji wa Ai maana nitautia muji ule katika mikono yako.” Yoshua akaelekeza mukuki wake kwenye muji wa Ai.

19Mara tu Yoshua alipouelekeza mukuki wake kule Ai, kundi lililokuwa likivizia upande mwingine likatoka na kuingia katika muji. Likauteka muji na kuuteketeza kwa moto.

20Watu wa Ai walipoangalia nyuma, wakaona moshi ukitoka katika muji ukipanda mpaka mbinguni. Nao hawakukuwa na uwezo wa kukimbia upande wowote, maana Waisraeli waliwageukia wale waliokuwa wanawafuatilia.

21Yoshua na Waisraeli wote walipoona kwamba kundi lililokuwa linavizia limeuteka muji, na kwamba moshi ulikuwa unapanda juu, waliwageukia na kuanza kuwaua.

22Watu waliobaki katika muji walitoka, lakini wote wakakuwa wamezungukwa na Waisraeli; nao wakauawa, wala hakukubaki hata mumoja wao.

23Lakini mufalme wa muji wa Ai walimuteka akiwa muzima na kumupeleka kwa Yoshua.

24Waisraeli walipomaliza kabisa kuwaua watu wote wa Ai kule katika jangwa ambako waliwafuatilia wakarudi katika muji wa Ai na kuwaua wote waliobaki mule.

25Jumla ya watu wa Ai waliouawa siku hiyo, wanaume na wanawake, walikuwa elfu kumi na mbili.

26Yoshua hakuushusha mukono wake aliokuwa akishikilia nao mukuki wake kuelekea Ai mpaka alipowaua wakaaji wote wa muji huo.

27Waisraeli waliteka tu nyama na mali kama vile Yawe alivyomwamuru Yoshua.

28Basi, Yoshua aliuteketeza muji wa Ai kwa moto na kuufanya mabomoko mpaka hivi leo.

29Kisha akamutundika mufalme wa Ai juu ya muti wa tini mpaka magaribi. Lakini jua lilipoanza kutua, Yoshua aliamuru maiti yake iondolewe juu ya muti na kutupwa kwenye mulango wa muji kisha walundike lundo kubwa la mawe juu ya maiti hiyo. Lundo hilo liko kule mpaka leo.

Sheria inasomwa kwenye mulima Ebali

30Kisha, Yoshua akamujengea Yawe, Mungu wa Israeli, mazabahu juu ya mulima Ebali, Ang. Kumb 27.2-8

31kama vile Musa mutumishi wa Yawe alivyowaagiza Waisraeli, kadiri ilivyoandikwa katika kitabu cha Sheria ya Musa kwamba itakuwa mazabahu iliyojengwa kwa mawe ambayo hayakuchongwa, wala kuguswa na chombo chochote cha chuma. Juu ya mazabahu hiyo wakamutolea Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani. Ang. Kut 20.25

32Na kule, mbele ya Waisraeli wote, Yoshua aliandika mufano wa sheria ya Musa juu ya mawe.

33Waisraeli wote pamoja na viongozi wao, wazee na waamuzi na wageni wote waliokuwa kati yao, wakasimama kila upande kuelekeana na Sanduku la Agano mbele ya makuhani Walawi waliokuwa wamelibeba Sanduku la Agano la Yawe. Nusu yao wakasimama mbele ya mulima Gerizimu na nusu nyingine wakasimama mbele ya mulima Ebali, kama vile Musa, mutumishi wa Yawe alivyoagiza pale mbele juu ya kubarikiwa kwa Waisraeli. Ang. Kumb 11.29; 27.11-14

34Kisha, Yoshua akawasomea sheria zote, pamoja na baraka na laana kama ilivyoandikwa katika kitabu cha sheria.

35Hakuna neno lililoamriwa na Musa ambalo Yoshua hakulisoma mbele ya Waisraeli, kati yao kukiwa wanawake, watoto na wageni.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help