1Katika siku zile kundi kubwa la watu walikusanyika tena. Nao walipokosa chakula, Yesu akawaita wanafunzi wake, na kuwaambia:
2“Ninawasikilia watu hawa huruma, kwa sababu wamekaa nami sasa muda wa siku tatu, nao hawana chakula tena.
3Kama nikiwaambia waende kwao pasipo kula wataregea katika njia, kwa maana wamoja kati yao wametoka mbali.”
4Wanafunzi wake wakamujibu: “Hapa katika pori mutu ataweza kupata wapi chakula cha kuwashibisha?”
5Yesu akawauliza: “Muko na mikate ngapi?”
Nao wakamujibu: “Tuko na mikate saba.”
6Basi Yesu akawaamuru watu waikae chini. Kisha akakamata ile mikate saba, akamushukuru Mungu, akaimega na kuwapa wanafunzi wake waigawanye kwa watu; nao wanafunzi wakaigawanya.
7Walikuwa vilevile na samaki ndogo chache. Yesu akamushukuru Mungu na kuwaambia wanafunzi wazigawanye vilevile.
8Wote walikula na kushiba. Kisha wanafunzi wakaokota vipande vya mikate na vya samaki vilivyobaki, wakajaza vitunga saba.
9Watu waliokula walikuwa yapata elfu ine. Kisha kuagana nao,
10mara moja Yesu akaingia ndani ya chombo pamoja na wanafunzi wake, akaenda katika jimbo la Dalmanuta.
Wafarisayo wanataka kitambulisho(Mat 16.1-4)11Wafarisayo wakamufikia Yesu na kuanza kubishana naye. Wakamupima wakimwomba awaonyeshe kitambulisho kinachohakikisha kwamba uwezo wake umetoka kwa Mungu.
12Yesu akaugua sana kwa huzuni, na kusema: “Sababu gani ninyi watu wa kizazi hiki munataka kuona kitambulisho? Kweli ninawaambia, hamutaonyeshwa kitambulisho!”
13Kisha akawaacha, akaingia tena ndani ya chombo, akaanza kuvuka ziwa.
Chachu ya Wafarisayo na ya Herode(Mat 16.5-12)14Wanafunzi walikuwa wamesahau kupeleka mikate, isipokuwa walikuwa na mukate mumoja tu ndani ya chombo.
15Yesu akawaagiza: “Mujiangalie vizuri, mujiepushe na chachu ya Wafarisayo na ya Herode.”
16Wanafunzi wakaanza kusemezana: “Anasema hivi kwa sababu hatuna mikate.”
17Yesu akatambua maneno waliyosema, basi akawauliza: “Sababu gani munasemezana juu ya kukosa mikate? Hamujafahamu wala kuelewa? Mioyo yenu ingali migumu?
18Muko na macho, lakini hamwoni? Muko na masikio, lakini hamusikii? Hamukumbuki
19wakati nilipomega mikate mitano na kulisha watu elfu tano? Wakati ule mulijaza vitunga ngapi na vipande vya mikate?”
Wakajibu: “Kumi na viwili.”
20Naye akawauliza tena: “Na wakati nilipomega mikate saba na kulisha watu elfu ine, mulijaza vitunga ngapi na vipande vya mikate?”
Wakamujibu: “Saba.”
21Basi Yesu akawauliza: “Na hata sasa hamujaelewa kitu?”
Yesu anaponyesha kipofu wa Betesaida22Yesu na wanafunzi wake wakafika Betesaida. Kule wakamuletea Yesu mutu mumoja kipofu na kumwomba amuguse kusudi apate kupona.
23Yesu akashika mukono wa yule kipofu na kumupeleka inje ya kijiji. Yesu alipokwisha kupakaa mate kwa macho ya mutu yule na kuweka mikono juu yake, akamwuliza: “Unaona kitu?”
24Kipofu akainua macho yake na kusema: “Ninaona watu wakitembea, lakini wanaonekana kama miti.”
25Yesu akagusa tena macho ya yule kipofu, naye akapata kuona vizuri. Macho yake yakapona, na kupata kuona vitu vyote waziwazi.
26Kisha Yesu akamwomba arudie kwake, akimwagiza asirudi katika kijiji.
Petro anajulisha kwamba Yesu ni Kristo(Mat 16.13-20; Lk 9.18-21)27Yesu na wanafunzi wake wakaenda pande za vijiji vilivyokuwa karibu na muji Kaisaria Filipi. Walipokuwa katika njia yeye akawauliza: “Watu wanasema kwamba mimi ni nani?”
28Nao wakamujibu: “Wamoja wanasema kwamba wewe ni Yoane Mubatizaji; wengine wanasema kwamba wewe ni nabii Elia na wengine wanasema kwamba wewe ni mumoja wa manabii wengine.”
29Halafu Yesu akawauliza: “Na ninyi munasema kwamba mimi ni nani?”
Petro akamujibu: “Wewe ni Kristo.”
30Basi Yesu akawaagiza wasimwambie mutu neno lile.
Yesu anajulisha habari za kufa na kufufuka kwake(Mat 16.21-28; Lk 9.22-27)31Kisha Yesu akaanza kuwafundisha wanafunzi wake, akisema: “Sherti Mwana wa Mutu ateswe na kukataliwa na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani pamoja na walimu wa Sheria. Atauawa na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake atafufuka.”
32Yeye aliwaambia maneno hayo waziwazi. Basi Petro akamwita Yesu pembeni na kuanza kumukaripia.
33Lakini Yesu akawageukia wanafunzi wake na kumukaripia Petro akisema: “Ondoka hapa karibu nami wewe Shetani, kwa maana mawazo yako si ya Mungu lakini ni ya kimutu.”
Namna ya kufuata Yesu34Kisha Yesu akaita kundi la watu pamoja na wanafunzi wake, na kuwaambia: “Kama mutu akitaka kunifuata, asijishugulikie mwenyewe, lakini ajitolee kwa kubeba musalaba wake na kunifuata.
35Kwa maana mutu anayetaka kulinda uzima wake, ataupoteza; lakini yule atakayetoa uzima wake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Habari Njema, ataulinda.
36Ni faida gani kwa mutu kupata utajiri wote wa dunia, lakini anapoteza uzima wake?
37Hakuna kitu chochote mutu anachoweza kutoa kwa kukomboa uzima wake.
38Kwa hiyo mutu yeyote anayesikia haya juu yangu na juu ya mafundisho yangu kati ya watu wa kizazi hiki kisichokuwa na uaminifu mbele ya Mungu na chenye zambi, Mwana wa Mutu atasikia haya juu yake vilevile. Itakuwa vile, atakapokuja pamoja na wamalaika watakatifu, akitukuzwa na Baba yake.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.