Yeremia 1 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Maneno ya Yeremia mwana wa Hilkia, mumoja wa makuhani wa muji Anatoti, katika inchi ya kabila la Benjamina.

2Neno la Yawe lilimufikia Yeremia katika mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni, mufalme wa Yuda.

3Tena lilimufikia Yeremia wakati Yoyakimu mwana wa Yosia, alipokuwa mufalme wa Yuda. Neno la Yawe liliendelea kumufikia mpaka mwisho wa mwaka wa kumi na mumoja wa utawala wa Zedekia, mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda. Ni katika mwezi wa tano wa mwaka huo, ndio wakati watu wa Yerusalema walipelekwa katika uhamisho.

Yeremia anaitwa kuwa nabii

4Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:

5Mbele ya kukutengeneza katika tumbo la mama yako,

mimi nilikujua;

mbele haujatoka katika tumbo,

nilikuweka kwa kazi yangu;

mimi nilikuchagua kuwa

nabii kwa mataifa.

6Nami nikajibu: Ee! Bwana wangu Yawe,

mimi sijui kusema, ningali bado kijana.

7Lakini Yawe akaniambia:

Usiseme kwamba ungali kijana.

Utakwenda kwa watu ninaokutuma kwao,

na maneno yote nitakayokuamuru, utayasema.

8Wewe usiwaogope watu hao.

Niko pamoja nawe kwa kukulinda.

–Ni ujumbe wa Yawe.

9Kisha Yawe akanyoosha mukono wake, akagusa kinywa changu, akaniambia:

Nimetia maneno yangu ndani ya kinywa chako.

10Leo nimekupa mamlaka juu ya mataifa na falme,

ukuwe na mamlaka ya kuongoa na kubomoa,

mamlaka ya kuharibu na kuangamiza,

mamlaka ya kujenga na ya kupanda mbegu.

Maono mawili

11Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi: Yeremia, unaona nini? Nami nikasema: Ninaona tawi la muti wa uangalivu ambao maua yake yamekwisha kuchanua.

12Yawe akaniambia: Umeona vizuri, kwa maana nitakuwa na uangalivu kusudi maneno yangu yapate kutimia.

13Neno la Yawe lilinifikia mara ya pili kusema hivi: Unaona nini? Nami nikasema: Ninaona chungu kinachotokota, nacho kinainamia upande wangu tokea kaskazini.

14Yawe akaniambia: Maangamizi yataanzia tokea kaskazini na kuwapata wakaaji wote wa inchi hii.

15Maana ninaziita falme zote na makabila yote ya kaskazini. Wafalme wake wote watakuja na kila mumoja wao ataweka kiti chake cha kifalme mbele ya milango ya ukuta wa Yerusalema na kandokando ya kuta zake zote, na kuizunguka miji yote ya Yuda.

16Nami nitawahukumu Waisraeli kwa ajili ya uovu wao wote, kwa maana waliniacha mimi na kuifukizia miungu mingine ubani na kuabudu sanamu walizojitengenezea wenyewe.

17Sasa basi, wewe Yeremia ujiweke tayari. Simama! Uende kuwaambia mambo yote ninayokuamuru. Usiwaogope, kusudi mimi nisikufanye kuwa mwoga mbele yao.

18Na tangu leo, ninakufanya kuwa imara kama muji unaozungukwa na kuta, kama munara wa chuma na kama ukuta mugumu sana wa shaba. Utakuwa na nguvu juu ya inchi yote, juu ya wafalme wa Yuda, wakubwa wake, makuhani wake na watu wake wote.

19Watapigana nawe, lakini hawatashinda, kwa sababu mimi niko pamoja nawe kwa kukuokoa.

–Ni ujumbe wa Yawe.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help