1Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2Wewe mwanadamu! Umwambie mufalme wa Tiro kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi:
Wewe una kiburi cha moyo,
na umesema kwamba wewe ni mungu,
kwamba umeikalia kiti cha kifalme cha miungu,
umekaa mbali huko katika bahari.
Lakini, wewe ni mutu tu wala si mungu,
ingawa unajiona kuwa na hekima kama mungu.
3Wewe unajiona mwenye hekima kuliko Danieli,
unazani hakuna siri yoyote usiyoijua.
4Kwa hekima na akili yako
umejipatia utajiri,
umejikusanyia zahabu na feza
ukaziweka katika hazina zako.
5Kwa werevu wako mukubwa katika biashara
umejiongezea utajiri wako,
ukakuwa na kiburi kwa ajili ya mali zako!
6Kwa hiyo Bwana wetu Yawe anasema hivi:
Kwa vile unajiona mwenye hekima kama mungu,
7basi nitakuletea watu wageni,
mataifa ya hatari kuliko yote.
Wataharibu utukufu wa hekima yako
na kuchafua uzuri wako.
8Watakutumbukiza chini ndani ya shimo,
nawe utakufa kifo cha rafla katika kilindi cha bahari.
9Utaendelea kujiona kuwa mungu
mbele ya hao watakaokuua?
Katika mikono ya hao watakaokuangamiza,
utatambua kwamba wewe ni mutu tu, wala si mungu!
10Utakufa kifo cha haya kubwa
katika mikono ya watu wa mataifa.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
Kuanguka kwa mufalme wa Tiro11Tena neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
12Wewe mwanadamu! Imba wimbo wa maombolezo juu ya mufalme wa Tiro. Umwambie kwamba:
Bwana wetu Yawe anasema hivi:
Wewe mufalme wa Tiro ulikuwa mupaka wa ukamilifu;
ulijaa hekima na uzuri kamili.
13Ulikaa Edeni, bustani ya Mungu.
Ulipambwa kwa kila namna ya mawe ya bei kali,
akiki, topazi, yaspi, zabarajadi, berili,
sardoniki, yakuti samawi, almasi na zumaridi.
Ulikuwa na mapambo ya zahabu.
Yote uliwekewa tayari siku ulipoumbwa.
14Nilichagua kerubi kwa kukulinda,
uliishi katika mulima wangu mutakatifu
na kutembea juu ya mawe yanayometameta.
15Uliishi maisha makamilifu
tangu siku ile ulipoumbwa,
mpaka wakati ulipoanza kufanya uovu.
16Ustawi wa biashara yako
ulikujaza ukali, ukatenda zambi.
Kwa hiyo nilikufukuza kama muchafu,
mbali na mulima wangu mutakatifu.
Na yule kerubi aliyekulinda
akakufukuzia mbali na mawe yanayometameta.
17Ulikuwa na kiburi
kwa sababu ya uzuri wako.
Uliharibu hekima yako kwa sababu ya utukufu wako.
Nilikutupa chini kwenye udongo,
nikakufanya kuwa kitisho kwa wafalme.
18Kwa wingi wa mabaya yako
na udanganyifu katika biashara yako
ulipachafua pahali pako pa kuabudia;
kwa hiyo niliwasha moto kwako, nao ukakuteketeza,
nami nikakufanya kuwa majivu juu ya inchi,
mbele ya wote waliokuangalia.
19Wote wanaokufahamu kati ya mataifa
wameshikwa na mushangao juu yako.
Umekuwa kitu cha kuogopesha,
na kutoweka kwa milele.
Unabii juu ya Sidona20Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi: Ang. Yoe 3.4-8; Zak 9.1-2; Mat 11.21-22; Lk 10.13-14
21Wewe mwanadamu! Ugeukie upande wa Sidona na kutoa unabii juu yake.
22Sema hivi:
Bwana wetu Yawe anasema hivi:
Mimi nitapingana nawe Sidona,
na kuonyesha utukufu wangu kati yako.
Nitakapotimiza hukumu zangu juu yako
na kukuonyesha utakatifu wangu,
halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe.
23Nitakutumia ugonjwa mukali
na umwangaji wa damu utafanyika katika barabara zako.
Utashambuliwa kwa upanga toka pande zote
na watu wako watakaouawa, watakuwa wengi.
Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
Waisraeli watapata baraka24Mungu anasema: Mataifa jirani za Waisraeli ambayo yalikuwa yanawauzi hayataweza tena kuwaumiza Waisraeli kama vile kwa miiba na michongoma. Halafu watajua kwamba mimi ni Bwana wao Yawe.
25Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitawakusanya na kuwaleta Waisraeli kutoka katika mataifa yote ambamo walisambazwa. Hivyo nitawafanya watu wa mataifa waone kwamba mimi ni mutakatifu. Waisraeli wataishi katika inchi yao ambayo mimi nilimupa mutumishi wangu Yakobo.
26Watakaa humo kwa salama kabisa; watajenga nyumba na kupanda mizabibu. Wataishi bila hofu maana mataifa jirani zao ambayo yaliwauzi, mimi nitayaazibu. Hapo watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wao.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.