1Yesu alipoona yale makundi ya watu, alipanda kwenye kilima. Alipokwisha kuikaa, wanafunzi wake wakamujongelea.
2Naye akaanza kuwafundisha akisema:
Raha ya kweli(Lk 6.20-23)3“Heri wale wanaokuwa wamasikini wa roho,
maana Ufalme wa mbinguni ni kwao!
4Heri wale wanaokuwa na huzuni,
maana Mungu atawafariji!
5Heri wale wanaokuwa wapole,
maana watarizi dunia!
6Heri wale wanaokuwa na njaa na kiu ya kufanya yanayokuwa haki,
maana watashibishwa!
7Heri wale wanaokuwa na huruma,
maana Mungu atawahurumia!
8Heri wale wanaokuwa na moyo safi,
maana watamwona Mungu!
9Heri wale wanaoleta amani,
maana wataitwa watoto wa Mungu!
10Heri wale wanaoteswa kwa ajili ya haki,
maana Ufalme wa mbinguni ni kwao!
11“Heri ninyi, wakati watu wanapowatukana na kuwatesa na kuwasingizia kila namna ya ubaya kwa sababu yangu.
12Mufurahi na kushangilia, kwa sababu munawekewa zawadi kubwa mbinguni. Ni hivi walivyowatesa manabii walioishi mbele yenu.
Chumvi na mwangaza(Mk 9.50; Lk 14.34-35)13“Ninyi ni kama chumvi kwa watu wote. Lakini kama chumvi ikipoteza onjo lake, itatiwa nini ipate tena kukolea? Haifai tena hata kidogo, inabakilia kutupwa na kukanyagwa na watu.
14“Ninyi ni kama mwangaza katika dunia. Muji unaojengwa juu ya mulima hauwezi kufichama.
15Hakuna mutu anayewakisha taa na kuiweka chini ya kitunga, lakini anaiweka juu ya kinara kusudi iwaangazie wote wanaokuwa ndani ya nyumba.
16Vilevile, mwangaza wenu unapaswa kuangaza mbele ya watu, kusudi waone matendo yenu mazuri, nao wamutukuze Baba yenu anayekuwa mbinguni.
Mafundisho juu ya Sheria17“Musizani kama nilikuja kuvunja Sheria ya Musa au mafundisho ya manabii. Mimi sikukuja kuvunja, lakini kukamilisha.
18Kweli ninawaambia: kwa muda wote mbingu na dunia vitakapokuwa vingali, hakuna hata herufi moja wala nukta moja ya Sheria itakayoondoshwa mpaka yote yatimie.
19Ni kwa hiyo mutu yeyote atakayevunja hata amri moja inayokuwa ndogo kuliko zingine zote, na kuwafundisha watu wengine kufanya kama yeye, huyu atahesabiwa kuwa mudogo katika Ufalme wa mbinguni. Lakini yule atakayezishika na kuzifundisha wengine, huyu atahesabiwa kuwa mukubwa katika Ufalme wa mbinguni.
20Basi ninawaambia: musipokuwa wenye haki kuliko walimu wa Sheria na Wafarisayo hamutapokelewa katika Ufalme wa mbinguni.
Mafundisho juu ya kasirani21“Mumesikia kwamba babu zenu waliambiwa: ‘Usiue; mutu yeyote anayeua anapaswa kuhukumiwa.’
22Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayemukasirikia ndugu yake anapaswa kuhukumiwa. Naye anayemwambia ndugu yake: ‘Hauna akili wewe!’ anapaswa kupelekwa kwenye tribinali kubwa. Naye anayemwambia: ‘Uko mwenda-wazimu!’ anastahili kutupwa katika jehenamu.
23Basi kama ukienda kumutolea Mungu sadaka juu ya mazabahu na pale ukikumbuka kwamba ndugu yako yuko na neno juu yako,
24uache sadaka yako pale mbele ya mazabahu na uende kwanza kusikilizana naye. Na kisha urudie na kutoa sadaka yako.
25“Kama mutu akikushitaki, upatane naye upesi wakati mungali katika njia kwenda kwenye tribinali. Kama si vile, yule anayekushitaki atakutoa kwa mwamuzi, naye mwamuzi atakupeleka kwa askari, nawe utatupwa katika kifungo.
26Kweli ninakuambia: hautatoka mule mpaka utakapomaliza kulipa sengi ya mwisho.
Mafundisho juu ya uzinzi27“Mumesikia kwamba imesemwa: ‘Usizini.’
28Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayemwangalia mwanamuke kwa kumutamani, amekwisha kuzini naye ndani ya moyo wake.
29Basi kama jicho lako la kuume likikukosesha, uliongoe na kulitupa mbali. Ni heri kwako kupoteza kiungo chako kimoja kuliko mwili wako wote muzima kutupwa katika jehenamu.
30Na kama mukono wako wa kuume ukikukosesha, uukate na kuutupa mbali. Ni heri kwako kupoteza kiungo chako kimoja kuliko mwili wako wote muzima kutupwa katika jehenamu.
31“Na zaidi ya hii imesemwa: ‘Kila mutu anayemufukuza muke wake amupe barua ya kuachana naye.’
32Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayeachana na muke wake, isipokuwa tu kwa sababu ya uzinzi, anamufanya muke yule kuwa muzinzi kama akiolewa tena. Na mutu anayemwoa yule muke aliyefukuzwa, anazini vilevile.
Mafundisho juu ya kiapo33“Mumesikia vilevile kwamba babu zenu waliambiwa hivi: ‘Usifanye viapo vya uongo, lakini sherti utimize viapo vyako mbele ya Bwana.’
34Lakini mimi ninawaambia: musiape hata kidogo kwa jina la mbingu, kwa maana ni kiti cha kifalme cha Mungu;
35wala kwa jina la dunia, kwa maana ni kiti chake cha kupumzishia miguu; wala kwa jina la Yerusalema, kwa maana ni muji wa Mufalme mukubwa.
36Mutu asiape akitaja hata kichwa chake mwenyewe, kwa maana hawezi kugeuza hata unywele wake mumoja kuwa mweupe au mweusi.
37Lakini munaposema, museme tu: ‘Ndiyo,’ au ‘Hapana,’ kwa maana maneno yanayosemwa zaidi ya hayo yanatoka kwa yule mwovu Shetani.
Mafundisho juu ya kulipiza kisasi(Lk 6.29-30)38“Mumesikia kwamba imesemwa hivi: ‘Jicho kwa jicho, na jino kwa jino.’
39Lakini mimi ninawaambia: musirudishe mabaya kwa mabaya. Kama mutu akikupiga kofi kwa shavu la kuume, umugeuzie shavu la kushoto vilevile.
40Kama mutu akitaka kukushitaki kusudi akunyanganye shemizi yako, umwachie koti yako vilevile.
41Kama mutu anayetumwa na wakubwa akikulazimisha kubeba muzigo kilometre moja, uubebe hata kilometre mbili.
42Mutu akikuomba kitu, umupe. Na mutu akitaka umukopeshe, usimugeuzie mugongo.
Kupenda adui(Lk 6.27-28,32-36)43“Mumesikia kwamba imesemwa hivi: ‘Umupende mwenzako, lakini umuchukie adui yako.’
44Lakini mimi ninawaambia: muwapende waadui zenu na muwaombee wale wanaowatesa.
45Mufanye vile kusudi mupate kuwa kweli watoto wa Baba yenu anayekuwa mbinguni. Kwa maana yeye anawaangazia waovu na wema jua lake, naye anawanyeshea mvua wenye haki na wasiokuwa wenye haki.
46Zawadi gani mutapata kutoka kwa Mungu, kama mukiwapenda tu wenye kuwapenda? Hata walipishaji wa kodi wanaokuwa wakorofi wanatendeana vile!
47Na kama mukiwasalimia wandugu zenu tu, munatenda tendo gani la kupita wengine? Hata wapagani wanatendeana vile!
48Basi mukuwe wakamilifu, kama vile Baba yenu wa mbinguni anavyokuwa mukamilifu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.