Isaya 1 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Haya ni maono Isaya mwana wa Amozi, aliyoyaona juu ya inchi ya Yuda na Yerusalema, katika nyakati za utawala wa wafalme hawa wa Yuda: Ahazi na Hezekia. Mungu anawakaripia watu wake

2Yawe anasema hivi:

Sikiliza enyi mbingu,

tega sikio ee dunia.

Mimi nimewalea watoto wangu na kuwakomalisha,

lakini sasa wameniasi!

3Ngombe anamufahamu mwenye naye,

punda anajua kibanda cha bwana wake;

lakini Waisraeli hawajui,

watu wangu, hawaelewi!

4Ole kwako wewe taifa lenye zambi,

watu waliolemewa na uovu,

kizazi cha watenda mabaya,

watoto wanaoishi kwa udanganyifu!

Ninyi mumemwacha Yawe,

mumemuzarau Mutakatifu wa Israeli,

mumerudi nyuma.

5Niwapige wapi tena,

ninyi munaoendelea kuasi?

Kichwa chote kinajaa vidonda,

na moyo unaumia kabisa!

6Tokea kwenye muguu mpaka kwenye kichwa

hakuna chenye kuwa kizima;

ni machubuko, alama za mapigo na vidonda vinavyovuja damu,

vilivyokosa kusafishwa, kufungwa wala kutulizwa kwa mafuta.

7Inchi yenu imeharibiwa kabisa;

miji yenu imeteketezwa kwa moto.

Wageni wamebeba mazao ya inchi yenu mbele ya macho yenu,

imeharibiwa kama vile Sodoma.

8Sayuni umeachwa kama kibanda katika shamba la mizabibu,

kama kibanda cha mulinzi katika shamba la maboga,

kama muji uliozungukwa kwa vita.

9Yawe wa majeshi asingetuachia watu wachache,

tungekwisha kuwa kama watu wa Sodoma

tungekuwa na hali ileile ya Gomora.

10Musikilize neno la Yawe,

enyi watawala waovu kama wa Sodoma!

Musikilize mafundisho ya Mungu wetu,

enyi watu waovu kama wa Gomora!

11Yawe anasema hivi:

Uwingi wa sadaka zenu ni kitu gani kwangu?

Nimechoka na sadaka zenu za kondoo wenye kuteketezwa

na mafuta ya nyama wenu wenye kunona.

Sipendezwi na damu ya ngombe dume,

wala ya wana-kondoo, wala ya beberu.

12Munapokuja mbele yangu kuniabudu,

nani aliyewaambia mukanyagekanyage ndani ya viwanja vyangu?

13Musiniletee tena matoleo yenu yasiyokuwa na maana;

ninachukizwa na sadaka yenu ya ubani.

Muache kufanya sikukuu za mwandamo wa mwezi,

Sabato na mikutano ya ibada;

sikubali ibada zilizochanganyika na maovu.

14Sipendezwi na sikukuu zenu za mwandamo wa mwezi,

pamoja na sikukuu zenu zingine.

Zimekuwa muzigo muzito kwangu,

nami nimechoka kuzivumilia.

15Munapoinua mikono yenu kwa kuomba,

nitauficha uso wangu nisiwaone.

Hata mukiomba sana sitawasikia,

maana mikono yenu imejaa damu.

16Mujisafishe, mujitakase;

muondoe matendo yenu maovu mbele yangu.

Muache kutenda mabaya,

17mujifunze kutenda mema.

Mufuate sheria ya Mungu,

mumusaidie mwenye kuteswa,

mumupatie yatima haki yake,

mutetee haki za wajane.

18Yawe anasema hivi:

Mukuje basi, tukate shauri.

Zambi zenu zikionekana kuwa nyekundu,

zitakuwa nyeupe kama teluji;

zikionekana kuwa nyekundu sana,

zitakuwa nyeupe kama sufu.

19Mukiwa tayari kunitii,

mutakula mazao mema ya inchi.

20Lakini mukikataa na kuniasi,

mutaangamizwa kwa upanga.

Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.

Muji uliojaa zambi

21Namna gani muji uliokuwa mwaminifu

sasa umegeuka kuwa kahaba!

Wakati mumoja sheria ya Mungu ilifuatwa kabisa,

haki ilikaa ndani yake.

Sasa, ni muji wa wauaji.

22Feza yako imekuwa kama takataka;

divai yako imechanganyika na maji.

23Wakubwa wako ni waasi;

wanashirikiana na wizi.

Kila mumoja anapenda kituliro,

na kukimbilia zawadi.

Hawamupatii yatima haki yake,

haki za wajane si kitu kwao.

24Kwa hiyo,

nitawamwangia waadui zangu hasira yangu,

nitawalipiza kisasi wapinzani wangu.

–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi, Mwenye Nguvu wa Israeli.–

25Nitapigana nawe;

nitayeyusha uchafu wako kabisa,

na kuondoa takataka yako yote.

26Nitakupatia waamuzi wanaokuwa sawa wale wa kwanza

na washauri wanaokuwa sawa wale wa zamani.

Halafu, Yerusalema utaitwa Muji wa Haki,

Muji Mwaminifu.

27Muji Sayuni utakombolewa kwa njia ya kufuata sheria ya Mungu,

nao wakaaji wake waliogeuka toka zambi zao kwa njia ya haki.

28Lakini waasi na wenye zambi

wote wataangamizwa pamoja;

wanaomwacha Yawe watateketezwa.

29Mutapata haya kwa ajili ya miti ya mialo muliyoipenda sana;

mutafezeheka kwa sababu ya bustani mulizofurahia.

30Mutakuwa kama mialo ambayo majani yake yamekauka;

kama shamba lisilokuwa na maji.

31Wenye nguvu watakuwa kama majani yenye kukauka,

matendo yao yatakuwa kama cheche za moto.

Watateketea pamoja na matendo yao,

wala hakutakuwa mutu wa kuwaokoa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help