Zaburi 43 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Maombi ya mukimbizi yanaendelea

1Unipatie haki yangu, ee Mungu;

uyatetee maneno yangu mbele ya watu wabaya;

uniokoe na watu waongo na waovu.

2Ninakimbilia kwako, ee Mungu;

kwa nini umenitupilia mbali?

Kwa nini niende huko na huko nikiomboleza

kwa kuteswa na adui yangu?

3Utumie mwangaza na ukweli wako viniongoze,

vinipeleke kwenye mulima wako mutakatifu,

kwenye makao yako.

4Hapo, ee Mungu, nitakwenda kwenye mazabahu yako;

nitakuja kwako, ee Mungu, wewe furaha yangu kubwa.

Nitakusifu kwa zeze, ee Mungu, Mungu wangu.

5Mbona ninahuzunika hivyo katika moyo?

Kwa nini ninahangaika hivyo ndani mwangu?

Nitamutumainia Mungu,

nitamusifu tena

yeye anayekuwa musaada wangu na Mungu wangu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help