1Unipatie haki yangu, ee Mungu;
uyatetee maneno yangu mbele ya watu wabaya;
uniokoe na watu waongo na waovu.
2Ninakimbilia kwako, ee Mungu;
kwa nini umenitupilia mbali?
Kwa nini niende huko na huko nikiomboleza
kwa kuteswa na adui yangu?
3Utumie mwangaza na ukweli wako viniongoze,
vinipeleke kwenye mulima wako mutakatifu,
kwenye makao yako.
4Hapo, ee Mungu, nitakwenda kwenye mazabahu yako;
nitakuja kwako, ee Mungu, wewe furaha yangu kubwa.
Nitakusifu kwa zeze, ee Mungu, Mungu wangu.
5Mbona ninahuzunika hivyo katika moyo?
Kwa nini ninahangaika hivyo ndani mwangu?
Nitamutumainia Mungu,
nitamusifu tena
yeye anayekuwa musaada wangu na Mungu wangu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.