1Watu wote wanaokuwa watumwa wanapaswa kuwaheshimu wabwana wao kabisa, kusudi watu wasitukane jina la Mungu na kuzarau mafundisho yetu.
2Na wale wanaokuwa na wabwana waamini, wasiwakosee heshima kwa sababu wao ni wandugu. Wanapaswa kuwatumikia vizuri zaidi, kwa maana wao ni wandugu waamini na wapendwa, nao wanashiriki faida ya kazi yao.
Mashauri juu ya mafundisho ya uongo na tamaa ya maliHayo ndiyo maneno unayopaswa kufundisha na kuhubiri.
3Kama mutu akifundisha mafundisho mengine, naye hakubali maneno ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo wala mafundisho yanayolingana na dini yetu,
4yeye anajaa majivuno wala hajui kitu. Yeye yuko na ulema wa kubishana na kugombezana juu ya maana ya maneno. Na hayo yanaleta wivu, makelele, matukano, masingiziano
5na magomvi yasiyokuwa na mwisho ya watu wenye akili iliyokwisha kupotoka hata wamesahau ukweli kabisa. Ndio wale wanaozani kwamba dini ni njia ya kupata utajiri.
6Hakika, dini ni pato kubwa kwa mutu kama anafurahia vitu anavyokuwa navyo.
7Kwa maana hatukuleta kitu katika dunia wala hatuwezi kurudia na kitu.
8Basi kama tukiwa na chakula na nguo, vile vinatosha.
9Lakini wale wanaotaka kuwa watajiri wanaanguka katika majaribu na mitego, na katika tamaa nyingi za upumbafu na mabaya zinazowatumbukiza katika anguko na uharibifu.
10Kwa maana kupenda feza ni shina la mabaya yote. Kwa ajili ya kuzitamani watu wamoja wanaanguka katika imani yao, na wanajiumiza mioyo wakijiletea huzuni nyingi.
Maagizo mbalimbali ya pekee11Lakini wewe mutu wa Mungu, uepuke mambo haya, ushikamane na haki, ibada, imani, upendo, uvumilivu na upole.
12Upigane vita nzuri kwa kuchunga imani yako, upate kujitwalia uzima wa milele Mungu aliokuitia wakati ulipoitikia imani yako mbele ya washuhuda wengi.
13Mbele ya Mungu anayevipatia vitu vyote uzima, na mbele ya Kristo Yesu aliyetoa ushuhuda wa kweli mbele ya Pontio Pilato, ninakuagiza maneno haya:
14ushike mambo uliyoagizwa kwa uaminifu bila kosa mpaka Siku Bwana wetu Yesu Kristo atakapotokea.
15Kutokea kwake kutafanywa na Mungu kwa wakati aliopanga. Yule ndiye Mungu anayestahili kutukuzwa, anayekuwa peke yake mutawala, mufalme wa wafalme na Bwana wa wabwana.
16Ni yeye tu asiyeweza kufa na anayekaa katika mwangaza ambao mutu hawezi kukaribia. Hakuna mutu aliyemwona wala hakuna mutu anayeweza kumwona. Ndiye mwenye heshima na uwezo wa milele! Amina.
17Uwaagize wale wanaokuwa watajiri katika dunia hii ya sasa wasijivune, vilevile wasiweke matumaini yao katika mali inayotoweka upesi. Lakini wamutumainie Mungu anayetupatia vitu vyote kwa uwingi kusudi tufurahiwe navyo.
18Uwaagize watende mema, wakuwe watajiri katika matendo mazuri, nao wasaidiane kwa moyo safi na kushiriki mali yao na wengine.
19Kwa njia hii, watajiwekea akiba nzuri na yenye kudumu kwa ajili ya siku zitakazokuja kusudi wapate uzima wa kweli.
20Timoteo, uchunge vizuri kile ulichopewa kwa kulinda, ukiepuka maneno ya kidunia na mabishano yasiyokuwa na maana juu ya ile watu wengine wanayoita kuwa ni elimu lakini ni uongo.
21Kwa ajili ya kufuata elimu ile, watu wamoja wamepotoka katika imani yao.
Ninawatakia neema kutoka kwa Mungu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.