1Barua hii inatoka kwangu mimi muzee. Ninakuandikia wewe Gayo, mupendwa wangu, ninayekupenda hakika.
2Mupendwa wangu, ninakutakia maendeleo mazuri katika kila jambo; ninakutakia afya njema katika mwili, kama vile unavyokuwa nayo katika roho.
3Nilifurahi sana wakati wandugu wamoja walipofika na kunielezea juu ya ukweli unaokuwa ndani yako na kwamba unaishi katika ukweli.
4Hakuna jambo linalonifurahisha kuliko lile la kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.
Uaminifu wa Gayo5Mupendwa wangu, wewe ni mwaminifu kwa kazi unayofanya kwa ajili ya wandugu, hata kwa wale wanaokuwa wageni.
6Wandugu hawa walishuhudia upendo wako mbele ya kanisa. Ninakusihi uwasaidie wapate kuendelea na safari yao kwa namna inavyomupendeza Mungu.
7Kwa maana hawa walianza safari yao kwa ajili ya kazi ya Kristo bila kupokea musaada wowote toka kwa watu wasioamini.
8Basi sisi tunapaswa kuwasaidia watu kama hawa tupate kushiriki pamoja nao katika kazi ya kutangaza ukweli.
9Nimeandikia kanisa maneno machache lakini Diotrefe, anayependa kuwa musimamizi wao, anakataa kututii.
10Kwa sababu hiyo wakati nitakapokuja, nitaonyesha wazi mambo yote anayotenda akitusingizia sisi maneno mabaya. Lakini hatosheki na mambo yale, yeye mwenyewe anakataa kukaribisha wandugu wale wanaokuwa katika safari. Na wale wanaotaka kuwakaribisha, anawakataza na kuwafukuza katika kanisa.
11Mupendwa wangu, usifuate mufano mubaya, lakini ufuate mufano muzuri. Mutu anayetenda mema ni mutoto wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hashirikiani na Mungu.
12Watu wote wameshuhudia Demetrio vizuri; hakika ukweli wenyewe unahakikisha jambo lile. Sisi vilevile tunamushuhudia, nawe unajua kwamba ushuhuda wetu ni wa kweli.
Salamu za mwisho13Nina maneno mengi ya kukuambia lakini sitaki kuyaandika ndani ya barua.
14Ninatumaini kwamba nitakuona sasa hivi na wakati ule tutasemezana pamoja uso kwa uso.
15Ninakutakia amani.
Warafiki zako wanakusalimia. Utusalimie warafiki zetu, kila mutu kwa upekee.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.