1Mujongee musikilize enyi mataifa,
musikilize enyi watu.
Sikiliza, ee dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake,
ulimwengu na vyote vinavyotoka humo!
2Yawe amekasirikia mataifa yote,
amekasirikia majeshi yao yote.
Ameyapangia mwisho wao,
ameyatoa yaangamizwe.
3Maiti zao zitatupwa inje;
harufu ya maiti zao itasambaa;
damu yao itatiririka juu ya milima.
4Jeshi lote la anga litaharibika,
anga zitakunjamana kama karatasi.
Jeshi lake lote litanyauka,
kama vile majani ya mizabibu au mitini yanavyonyauka.
5Upanga wa Mungu uko tayari juu mbinguni.
Angalia, unashuka kuwaazibu Waedomu,
watu ambao ameamua kuwaangamiza.
6Upanga utajaa damu na mafuta:
damu ya kondoo na mbuzi,
na mafuta ya figo za kondoo dume.
Maana Yawe ana sadaka huko Bosira,
kutakuwa mauaji makubwa katika inchi ya Edomu.
7Mbogo wataangamizwa pamoja nao,
wana-ngombe pamoja na ngombe dume.
Inchi italewa na damu,
udongo utashiba kwa mafuta yao.
8Maana Yawe yuko na siku ya kulipiza kisasi;
mwaka wa kulipiza waadui za Sayuni.
9Vijito vya Edomu vitatiririsha kabulimbo,
udongo wake utakuwa kiberiti;
inchi yake itakuwa kabulimbo inayowaka.
10Itawaka usiku na muchana bila kuzimika,
moshi wake utapanda juu milele.
Inchi itakuwa jangwa siku zote,
hakuna atakayepitia huko milele.
11Itakuwa makao ya ndege za jangwa:
kozi, bundi na kibombobombo.
Yawe atawaletea muvurugano,
na timazi la fujo kwa wakubwa wake.
12Inchi itaitwa Inchi bila Mufalme;
wakubwa wake wote wametoweka.
13Miiba itaota katika pango zake,
miiba na michongoma ndani ya kuta zake.
Itakuwa makao ya imbwa wa pori,
nafasi ya mbuni.
14Paka wa pori na fisi watakuwa humo,
mapepo wataitana humo;
sulukutu atatulia humo
na kupata nafasi ya kupumzika.
15Humo bundi watataga mayai na kuyaatamia,
watatotoa vitoto na kuviweka chini ya kivuli chao.
Humo tai watakutanana,
kila mumoja na mwenzake.
16Musome katika kitabu cha Yawe:
Hakuna hata kiumbe kimoja kitakachokosekana,
kila kimoja kitakuwa na mwenzake.
Maana kinywa cha Yawe kimeamuru hivyo.
Roho yake itawakusanya hao wote.
17Yawe amepanga sehemu ya kila mumoja wao,
ametumia kamba kuwapimia inchi hiyo;
watairizi milele na milele,
wataishi mule kizazi hata kizazi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.