1Yeremia alipomaliza kuwaambia watu wote maneno yote ambayo Yawe, Mungu wao, alimwamuru awatangazie,
2Azaria mwana wa Hosaya, Yohana mwana wa Karea na watu wote wenye kiburi, walimwambia Yeremia: Yawe, Mungu wetu, hakukutuma wewe utuambie tusiende Misri, tuishi huko.
3Baruku mwana wa Neria, amekuchochea juu yetu kusudi tutiwe katika mikono ya Wakaldea watuue au watupeleke katika uhamisho kule Babeli.
4Basi, Yohana mwana wa Karea na wakubwa wote wa waaskari pamoja na watu wote hawakutii maneno ya Yawe, kwamba wabaki katika inchi ya Yuda.
5Halafu Yohana mwana wa Karea na wakubwa wote wa waaskari waliwapeleka watu wote wa Yuda waliobaki ambao walikuwa wamerudi katika inchi ya Yuda kutoka katika mataifa yote ambako walikuwa wamesambazwa:
6wanaume, wanawake, watoto, wabinti wa mufalme na kila mutu ambaye Nebuzaradani mukubwa wa waaskari alikuwa amemwachia Gedalia mwana wa Ahikamu mujukuu wa Safanu. Wakamupeleka vilevile nabii Yeremia na Baruku mwana wa Neria.
7Wakaenda katika inchi ya Misri, wakafika katika muji wa Tapanesi. Ndivyo walivyokataa kutii maneno ya Yawe.
8Wakati Yeremia alipokuwa Tapanesi, neno la Yawe lilimufikia Yeremia kusema hivi:
9Twaa mawe makubwa, uyafiche ndani ya udongo kwenye matofali mbele ya mulango wa nyumba ya kifalme ya Tapanesi mbele ya Wayuda.
10Kisha uwaambie hivi:
Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Muangalie, mimi nitamutuma na kumuleta Nebukadneza, mufalme wa Babeli, mutumishi wangu, naye ataweka kiti chake cha kifalme juu ya mawe haya ambayo nimeyaficha hapa, na kutandaza paa la kifalme juu yake.
11Atakapofika ataiangamiza inchi ya Misri. Kwa hiyo waliopangiwa kufa kwa ugonjwa watakufa kwa ugonjwa, waliopangiwa kukamatwa mateka, watakamatwa mateka; waliopangiwa kufa kwa vita watakufia katika vita.
12Mimi nitawasha moto katika mahekalu ya miungu ya Misri; naye Nebukadneza ataiteketeza miungu hiyo kwa moto au kuikamata mateka mpaka Babeli. Ataisafisha inchi ya Misri kama muchungaji anavyoondoa vidudu katika nguo yake na kuondoka Misri akiwa mushindi.
13Ataivunja minara ya mungu wao inayokuwa huko Heliopoli katika inchi ya Misri, na atateketeza mahekalu ya miungu ya Misri kwa moto.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.