Yobu 25 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Kisha Bildadi wa inchi ya Suhi akajibu:

2Mungu ni mwenye uwezo mukubwa,

watu wote wamwogope.

Yeye anaweka amani mpaka juu kwake mbinguni.

3Nani anayeweza kuhesabu majeshi yake?

Ni nani asiyeangaziwa na mwangaza wake?

4Mutu anaweza basi namna gani kuwa mwenye haki mbele ya Mungu?

Mwanadamu tu anaweza namna gani kujidai kuwa safi?

5Kwake Mungu, hata mwezi hauangai vya kutosha,

nyota nazo si safi mbele yake;

6ni nini sasa mutu ambaye ni kidudu,

mwanadamu ambaye ni nondo tu!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help