1Siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili, ni kusema mwezi wa Adari, ilipofika, siku ambayo tangazo la mufalme lingetimizwa, na waadui za Wayuda walitarajia kuwashinda Wayuda, ikageuzwa kuwa siku ya ushindi kwa Wayuda juu ya waadui zao.
2Katika kila muji wa kila jimbo wa mufalme Ahasuero, Wayuda walijitayarisha vizuri kumushambulia mutu yeyote ambaye angejaribu kuwazuru.
3Nao viongozi wote wa majimbo, watawala, wakubwa na wakubwa wa mufalme vilevile waliwasaidia Wayuda, maana wote walimwogopa Mordekayi.
4Mordekayi sasa akakuwa mutu mwenye madaraka makubwa katika nyumba ya kifalme, na habari zake zikaenea katika majimbo yote kwamba uwezo wake ulikuwa unazidi kuongezeka.
5Basi, Wayuda wakawashambulia waadui zao kwa upanga, wakawachinja, wakawaangamiza na kuwatendea kama walivyopenda.
6Kule katika muji wa Susani, Wayuda waliwaua watu mia tano.
7Vilevile waliwaua Parsandata, Dalfoni, Asipata,
8Porata, Adalia, Aridata,
9Parmasta, Arisayi, Aridayi na Wayezata,
10wana kumi wa Hamani mwana wa Hamedata, adui ya Wayuda. Hata hivyo, hawakunyanganya mali zao.
11Siku ileile, mufalme akajulishwa jumla ya watu waliouawa katika muji mukubwa wa Susani.
12Halafu mufalme akamwambia malkia Esteri: “Katika muji mukubwa peke yake Wayuda wamewaua watu mia tano, pamoja na wana kumi wa Hamani. Unafikiri wamefanya nini kule katika majimbo! Unataka nini sasa? Maana utatimiziwa. Uniambie, unataka nini zaidi, nawe utapewa.”
13Esteri akasema: “Ikikupendeza, ewe mufalme, kesho uwaruhusu Wayuda wanaokuwa Susani wafanye kama agizo la leo lilivyokuwa. Tena, uamuru wana kumi wa Hamani watundikwe kwenye miti.”
14Mufalme akaamuru hayo yatimizwe, na tangazo likatolewa katika muji Susani. Wana kumi wa Hamani wakatundikwa juu ya muti.
15Siku ya kumi na ine ya mwezi wa Adari, Wayuda wakakusanyika tena, wakawaua watu mia tatu zaidi katika muji wa Susani. Lakini hawakunyanganya mali za watu.
16Wayuda waliokuwa katika majimbo nao vilevile wakajitayarisha kuyalinda maisha yao. Wakaokolewa kutoka kwa waadui zao, wakawaua watu yapata elfu kumi na tano, lakini hawakunyanganya mali zao.
17Siku hiyo ilikuwa ya kumi na tatu ya mwezi wa Adari. Siku iliyofuata ya kumi na ine, wakapumzika, wakaifanya kuwa siku ya karamu na sherehe.
18Lakini Wayuda wa muji mukubwa wa Susani wakakusanyika vilevile siku ya kumi na ine lakini hawakupumzika. Walisherehekea siku ya kumi na tano kwa furaha na shangwe.
19Kutokana na sababu hii, Wayuda wanaokaa katika vijiji na katika miji midogo wanasherehekea siku ya kumi na ine ya mwezi wa Adari kuwa sikukuu ya furaha, na kupelekeana zawadi wakati wale wanaoishi katika miji mikubwa wanasherehekea siku ya kumi na tano ya mwezi wa Adari kama siku ya mapumziko, na kupelekeana vilevile zawadi.
Sikukuu ya Purimu20Mordekayi aliandika mambo haya yote. Kisha akaandika barua kwa Wayuda wote waliokuwa katika utawala wa Ahasuero.
21Aliwaonya kila mwaka washike sikukuu, siku ya kumi na ine na siku ya kumi na tano ya mwezi wa Adari.
22Wayuda walishinda waadui zao katika siku hizo, na katika mwezi huo huzuni yao iligeuzwa kuwa furaha, na kilio chao kuwa sikukuu. Waliagizwa wakuwe wanazikumbuka siku hizo kwa kufanya karamu na sherehe, kupelekeana zawadi za chakula na kuwapa wamasikini vitu.
23Basi, Wayuda wakakubaliana kufanya kama walivyoanza na kama vile Mordekayi alivyowaandikia.
24Hamani mwana wa Hamedata wa ukoo wa Agagi na adui wa Wayuda alikuwa amefanya mupango juu ya Wayuda kwa kuwaangamiza, vilevile alikuwa amepiga purimu, ni kusema kura, kwa kuamua siku ya kuwaponda na kuwaangamiza Wayuda.
25Lakini Esteri alipomwendea mufalme, naye mufalme akatoa amri kwa waandishi kwamba lile shauri baya ambalo Hamani alikuwa amefanya juu ya Wayuda, limurudilie yeye mwenyewe; na ya kuwa yeye na wana wake wauawe kwa kutundikwa kwenye muti.
26Kwa hiyo, wakaita siku hizo Purimu, kutokana na neno puri maana yake kura. Kwa sababu ya barua ya Mordekayi na mambo waliyoyaona wenyewe na yale yaliyowapata,
27Wayuda wakaifanya kuwa sheria kwao, kwa wazao wao na kwa mutu yeyote ambaye angejiunga nao, kwamba katika wakati uliopangwa kila mwaka, bila kukosa, siku hizo mbili zishikwe kulingana na maagizo ya Mordekayi.
28Vilevile walikubaliana kwamba kila jamaa ya Kiyuda, kizazi kwa kizazi, katika kila jimbo na muji, sharti ikumbuke siku za Purimu na kuzisherehekea siku zote.
29Halafu malkia Esteri, binti ya Abihaili, akaandika barua kwa mamlaka yake yote, pamoja na Mordekayi Muyuda kuhakikisha ile Mordekayi aliyoiandika pale mbele juu ya Purimu.
30Barua ile iliandikwa kwa Wayuda wote, na mifano ya barua zile kupelekewa katika majimbo yote mia moja makumi mbili na saba ya ufalme wa Ahasuero. Barua ile iliwatakia Wayuda amani na usalama,
31na kuwaamuru wao na wazao wao washike sikukuu za Purimu kwa wakati wake uliopangwa, kama vile walivyokuwa wanazikumbuka sheria za kufunga wakati wa kuomboleza. Maagizo haya yalitolewa na Mordekayi, Muyuda, pamoja na malkia Esteri.
32Amri ya Esteri ikahakikisha mambo hayo ya Purimu; ikaandikwa katika kitabu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.