2 Mambo ya Siku 28 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mufalme Ahazi wa Yuda(2 Fal 16.1-4)

1Ahazi alianza kutawala akiwa na umri wa miaka makumi mbili, alitawala kwa muda wa miaka kumi na sita kule Yerusalema. Yeye, hakufuata mufano muzuri wa Daudi babu yake, lakini alitenda maovu mbele za Yawe,

2na kufuata mienendo ya wafalme wa Israeli. Vilevile, alitengeneza hata sanamu za Mabali za madini yenye kuyeyushwa,

3akafukiza ubani kwenye Bonde la mwana wa Hinomu na kuwateketeza wana wake kama sadaka, akiiga desturi za kuchukiza za watu ambao walifukuzwa na Yawe wakati Waisraeli walipokuwa wanaingia katika inchi.

4Alitoa sadaka na kufukiza ubani pahali pa kuabudia miungu mingine, juu ya vilima na chini ya kila muti wenye majani mabichi.

Vita kati ya Suria na Israeli(2 Fal 16.5)

5Yawe, Mungu wake akamwacha mufalme Ahazi ashindwe na mufalme wa Suria ambaye vilevile akawapeleka watu wake wengi, akarudi nao Damasiki. Vilevile, alimufanya ashindwe na mufalme wa Israeli ambaye alimushinda na kuua watu wengi sana.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help