Ezekieli 45 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Sehemu ya inchi takatifu kandokando ya hekalu

1Mutakapoigawanya inchi kwa kupiga kura kusudi kila kabila lipate sehemu yake, sehemu moja ya inchi ni lazima itakaswe kwa ajili ya Yawe. Urefu wake utakuwa kilometre kumi na mbili na nusu na upana kilometre kumi. Eneo hilo lote litakuwa takatifu.

2Ndani yake kutakuwa eneo muraba kwa ajili ya patakatifu, kila upande metre mia mbili makumi tano, na litazungukwa na eneo wazi lenye upana wa metre mia mbili makumi tano.

3Katika eneo hilo utapima vilevile sehemu yenye urefu wa kilometre kumi na mbili na nusu kwa kilometre tano; humo kutakuwa hekalu langu, Pahali Patakatifu Sana.

4Eneo hilo litakuwa takatifu katika inchi, na kutengwa kwa ajili ya makuhani wanaomutumikia Yawe katika hekalu lake. Ndani ya eneo hilo kutakuwa nyumba zao na nafasi iliyotakaswa kwa ajili ya hekalu langu.

5Eneo lingine lenye urefu wa kilometre kumi na mbili na nusu kwa kilometre tano, litatengwa kwa ajili ya miji ya Walawi wanaotumika katika hekalu likuwe urizi wao.

6Mutapima eneo la muji karibu na eneo takatifu, lenye urefu wa kilometre kumi na mbili na nusu kwa kilometre mbili na nusu. Hilo litakuwa kwa ajili ya mutu yeyote wa Israeli.

Sehemu ya ufalme wa Waisraeli

7Mukubwa, naye atapewa eneo lake upande wa mashariki na magaribi wa eneo lililotakaswa kwa ajili ya Yawe. Eneo hilo litaenea tangia upande wa magaribi mpaka kwenye bahari ya Mediteranea na upande wa mashariki mpaka upande wa mashariki wa inchi. Litakuwa na urefu sawa na eneo lililopewa kwa kila kabila la Waisraeli.

8Huo ndio urizi wa mufalme katika Israeli. Hivyo mufalme hatawatesa watu wangu, lakini ataacha inchi igawanywe kwa Waisraeli kulingana na makabila ya Israeli.

Mapaswa ya mufalme

9Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninyi wakubwa wa Waisraeli, mumefanya zambi vyakutosha. Muache kutesa watu kwa ukali. Muimarishe sheria yangu na haki. Muache kuwafukuza watu wangu katika inchi.

–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–

10Kila mutu anapaswa kutumia mizani na vipimo vya haki.

12Kwa kupima uzito: gera makumi mbili ni shekeli moja, shekeli makumi tano ni mina moja.

13Vipimo vya matoleo yenu ya vyakula vitakuwa hivi: sehemu moja ya sita ya efa katika homeri moja ya ngano, na moja ya sita ya efa katika homeri moja ya shayiri.

14Kiwango cha mafuta kitakuwa hivi: sehemu moja ya bati ya mafuta kutoka kila kori (kori moja ni sawa na homeri moja ambayo ni sawa na bati kumi).

15Watatoa kondoo mumoja kwa kila kundi la kondoo mia mbili katika jamaa za Waisraeli. Wataleta sadaka za vyakula, sadaka za kuteketezwa kwa moto, na sadaka za amani, kusudi wapate kufanyiwa upatanisho. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–

16Watu wote wa inchi watamupatia mufalme wa Waisraeli sadaka hizo.

17Itakuwa ni mapaswa ya mufalme kuhakikisha kuwa sadaka za kuteketezwa, sadaka za vyakula na sadaka za kinywaji zinazotolewa wakati wa sikukuu ya mwandamo wa mwezi, Sabato, na sikukuu zozote zilizowekwa kwa Waisraeli, zinapatikana. Mufalme yeye mwenyewe atatayarisha sadaka za kusamehewa zambi, sadaka za vyakula, sadaka za kuteketezwa kwa moto, na sadaka za amani kwa kuwafanyia watu wote wa Israeli upatanisho.

Sikukuu(Kut 12.1-20; Law 23.33-43)

18Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, mutatoa sadaka ya mwana-ngombe dume asiyekuwa na kilema kwa kutakasa hekalu langu.

19Kuhani atatwaa sehemu ya damu ya sadaka ya kusamehewa zambi na kuipaka kwenye miimo ya nyumba ya Yawe, pembe za mazabahu, na miimo ya nafasi ya kuingilia kwenye kiwanja cha ndani.

20Atafanya vile vile siku ya saba ya mwezi huo, kwa ajili ya kila mutu aliyetenda zambi bila kukusudia au kwa kutokujua. Kwa njia hiyo mutaitakasa nyumba ya Yawe.

21Siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza, mutafanya sikukuu ya Pasaka. Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help