1Katika mwaka wa makumi tatu na sita wa utawala wa mufalme Asa, Basha, mufalme wa Israeli, alishambulia inchi ya Yuda na kuanza kujenga muji wa Rama kusudi apate kuzuia mutu yeyote asitoke wala asiingie kwa Asa, mufalme wa Yuda.
2Kwa hiyo mufalme Asa akatwaa feza na zahabu kutoka katika hazina ya nyumba ya Yawe na ya nyumba ya kifalme, akazituma Damasiki kwa Beni-Hadadi, mufalme wa Suria, na ujumbe akasema:
3“Tufanye mapatano ya ushirikiano kati yangu na wewe kama vile baba yangu na baba yako walivyofanya. Angalia ninakutumia zawadi ya feza na zahabu, kwenda uvunje mapatano ya ushirikiano unaokuwa kati yako na mufalme Basha wa Israeli kusudi aache mashambulizi juu yangu.”
4Hapo mufalme Beni-Hadadi akakubali pendekezo la mufalme Asa. Akawatuma majemadari wake na majeshi yake kwenda kushambulia miji ya Israeli. Nao wakateka miji ya Iyoni, Dani, Abeli-Maimu, na miji yote ya Nafutali iliyokuwa na hazina.
5Mufalme Basha alipopata habari za mashambulizi hayo, akaacha kujenga muji wa Rama, akasimamisha kazi yake.
6Kisha mufalme Asa aliwapeleka watu wote wa inchi ya Yuda, wakahamisha mawe ya Rama na mbao, vifaa ambavyo Basha alitumia kwa kujenga. Kisha Asa akatumia vifaa hivyo kwa kujenga miji ya Geba na Misipa.
Nabii Hanani7Kwa wakati ule, nabii Hanani akamwendea mufalme Asa wa Yuda, akamwambia: “Kwa sababu ulimutegemea mufalme wa Suria kuliko kumutegemea Yawe, Mungu wako, jeshi la mufalme wa Suria limekuponyoka.
8Wale Waetiopia na Walibia hawakukuwa jeshi kubwa na magari na waaskari wapanda-farasi wengi? Lakini kwa vile ulimutegemea Yawe, yeye aliwatia katika mikono yako.
9Yawe anachunga kwa uangalifu ulimwengu wote, kwa kuwapa nguvu wale wanaokuwa waaminifu kwake. Umetenda jambo la kipumbafu, kwa hiyo tangu sasa, utakuwa na vita kila mara.”
10Kwa hiyo, Asa akamukasirikia sana nabii Hanani, hata akamuweka katika kifungo; maana amekuwa na hasira kubwa naye juu ya maneno yale. Wakati uleule, Asa akaanza kuwatesa vikali wamoja kati ya watu.
Mwisho wa utawala wa Asa(1 Fal 15.23-24)11Matendo ya Asa, toka mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Yuda na Israeli.
12Katika mwaka wa makumi tatu na kenda wa utawala wake, Asa akashikwa na ugonjwa wa miguu. Ugonjwa ule ukazidi sana kuongezeka. Lakini hata wakati ule, Asa hakumugeukia Yawe amusaidie, lakini alijitafutia musaada kutoka kwa waganga.
13Asa akakufa katika mwaka wa makumi ine na moja wa utawala wake.
14Akazikwa katika kaburi alilokuwa amejichimbia yeye mwenyewe, katika muji wa Daudi. Walimulalisha juu ya kitanda kilichokuwa kimejazwa marasi ya kila aina yaliyotayarishwa na wafundi wa kutengeneza marasi, wakawasha moto mukubwa sana kwa heshima yake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.