1“Ninyi ni watoto wa Yawe, Mungu wenu; musijichanje wala kunyoa nywele upande wa mbele kwa ajili ya mutu aliyekufa.
2Ninyi ni watakatifu wa Yawe, Mungu wenu. Yawe amewachagua ninyi kuwa watu wake kati ya watu wote katika dunia yote.
Nyama safi na chafu(Law 11.1-47)3“Musikule kitu kinachokuwa chukizo kwa Mungu.
4Munaweza kula nyama hawa: ngombe, kondoo, mbuzi,
5kulungu, paa, kongoni, mbuzi wa pori, paa mweupe, pofu na mbuzi wa mulima,
6na kila nyama mwenye kwato zinazogawanyika sehemu mbili na mwenye kucheua.
7Lakini musikule nyama yeyote ambaye kwato zake hazigawanyiki sehemu mbili na hacheui. Musikule ngamia, sungura na pelele, ingawa wanacheua lakini kwato zao hazigawanyiki sehemu mbili; hao ni wachafu kwenu.
8Vilevile musikule nguruwe, maana ijapokuwa kwato zake zinagawanyika sehemu mbili, yeye hacheui; hao ni wachafu kwenu. Musikule nyama zao wala musiguse mizoga yao.
9“Munaweza kula kila aina ya samaki wenye mapezi na magamba.
10Lakini kiumbe chochote kinachoishi ndani ya maji kisichokuwa na mapezi wala magamba musikule; hivyo ni vichafu kwenu.
11“Munaweza kula ndege wote wanaokuwa safi.
12Lakini musikule ndege hawa: furukombe, kipungu,
13kengewa, kozi, mwewe na aina zake,
14kibombobombo na aina zake,
15mbuni, kirukanjia, dudumizi, kipanga na aina zake,
16bundi, mumbi, bundi mukubwa,
17mwari, nderi, munandi,
18membe, koikoi na aina zake, hudihudi na popo.
19Na wadudu wote wenye mabawa ni wachafu kwenu; musiwakule.
20Munaweza kula viumbe vyote vyenye mabawa vinavyokuwa safi.
21Musikule nyamafu yeyote lakini munaweza kumupa mugeni anayeishi katika miji yenu, akule, au munaweza kumwuzishia mutu wa taifa lingine. Musipike mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
“Ninyi ni watakatifu na Yawe ni Mungu wenu.
Sheria juu ya sehemu moja ya kumi22“Mutoe sehemu ya kumi ya mazao yenu yote ya shamba kila mwaka.
23Halafu muende pahali ambapo Yawe, Mungu wenu amepachagua kwa kuweka jina lake, na mukiwa mbele yake mutakula sehemu ya kumi ya ngano yenu, ya divai yenu na ya mafuta, na ya wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu. Mufanye hivi kusudi mujifunze kumwogopa Yawe, Mungu wenu siku zote.
24Ikiwa safari ni ndefu kwa sababu Yawe, Mungu wenu, amechagua pahali pa kuweka jina lake ambapo ni mbali sana na nyumba, nanyi hamuwezi kubeba sehemu ya kumi za mazao yenu ambayo Yawe amewajalia kupata, basi, mufanye hivi:
25“Muuzishe mazao yenu na kupeleka feza hiyo mpaka pahali Yawe, Mungu wenu, alipochagua,
26muzitumie hizo feza kwa kitu chochote mutakachopenda - nyama ya ngombe, nyama ya kondoo, divai au kinywaji kikali. Mutavikula na kufurahi hapo mbele ya Yawe, Mungu wenu, pamoja na jamaa zenu.
27“Musiwasahau Walawi wanaoishi kati yenu; wao hawana fungu wala urizi wao kati yenu.
28Kila mwisho wa mwaka wa tatu mutoe sehemu ya kumi ya mazao yenu yote na kuyaweka akiba katika miji yenu.
29Hiyo itakuwa kwa ajili ya Walawi, kwa sababu hawana fungu wala urizi wao kati yenu, nao wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu, watakuja kula na kushiba. Mufanye hivi naye Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika kazi zenu zote munazofanya kwa mikono yenu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.