1Yawe alimwambia Musa kule juu ya mulima Sinai:
2Uwaambie Waisraeli hivi: Mutakapofika katika inchi ninayowapa mimi Yawe, kila mwaka wa saba inchi itapumzishwa isilimwe kwa heshima ya Yawe.
3Kwa muda wa miaka sita mutalima udongo, mutapanda, mutakata matawi ya mizabu yenu na kuvuna mazao yenu.
4Lakini mwaka wa saba utakuwa ni Sabato ya mapumziko, ni Sabato ya Yawe. Musipande chochote wala kukata matawi ya mizabibu yenu.
5Chochote kinachoota peke yake musikivune wala kuchuma zabibu kutoka miti isiyokatwa matawi. Huo utakuwa mwaka wa kupumzisha udongo.
6Hata hivyo mwaka huo wa mapumziko ya inchi utawapatia chakula ninyi wenyewe, watumwa wenu na wajakazi, watumishi na wageni wanaokaa kati yenu.
7Inchi itakulisha nyama wenu wa kufugwa na nyama wa pori wanaokaa kati yenu.
Sikukuu ya miaka makumi tano8Mutahesabu miaka saba mara saba na jumla yake ni miaka makumi ine na tisa.
9Kisha, katika siku ya kumi ya mwezi wa saba ambayo ni siku ya kufanyiwa upatanisho mutatuma mutu kupiga baragumu katika inchi yote.
10Mwaka wa makumi tano mutauheshimu kwa kutangaza uhuru kwa watumwa wote katika inchi. Mwaka huo utakuwa ni sikukuu ya ukumbusho wa miaka makumi tano. Kila mumoja wenu atarudilia mali yake na jamaa yake.
11Kwa sababu mwaka huo ni wa sikukuu ya ukumbusho wa miaka makumi tano, musipande mbegu au kuvuna chochote kinachoota chenyewe wala kuchuma zabibu kutoka miti musiyokata matawi.
12Mwaka huo ni wa sikukuu kwenu, utakuwa mwaka mutakatifu. Hivyo mutakula yale yanayoota yenyewe katika mashamba.
13Katika mwaka huo chochote ambacho kiliuzishwa kinapaswa kirudishwe kwa mwenyeji.
14Unaponunua au kuuzisha shamba kwa mwenzako usimupunje.
15Bei ya shamba inapaswa kulingana na miaka mbele ya kurudishwa kwa mwenyeji.
16Kama miaka ni mingi utaongeza bei na kama miaka hiyo ni michache utapunguza bei, maana bei yake itapimwa kulingana na mazao anayokuuzishia.
17Musipunjane, lakini, mutamwogopa Mungu wenu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
18Kwa hiyo, mutafuata masharti yangu na kutimiza maagizo yangu, kusudi mupate kuendelea kuishi kwa usalama katika inchi.
19Inchi itatoa mazao yake nanyi mutakula na kushiba na kuishi mule kwa usalama.
20Lakini labda mutafikiri: Tutakula nini katika mwaka wa saba ijapokuwa haturuhusiwi kupanda wala kuvuna mazao yetu?
21Basi! Mimi nitabariki inchi katika mwaka wa sita nayo itawapa mazao ya kuwatoshelea kwa miaka mitatu.
22Mutakapopanda katika mwaka wa nane mutakuwa munakula mazao ya zamani na mutaendelea kula tu hata mwaka wa tisa mutakapoanza tena kuvuna.
Madaraka ya kukomboa shamba23Musiuzishe mashamba kabisa, maana hiyo ni mali yangu na ninyi ni wageni na wasafiri katika inchi yangu.
24Ndiyo maana katika inchi yote mutakuwa na utaratibu wa kukomboa mashamba.
25Kama ndugu yako anakuwa masikini, akiuzisha shamba lake, basi, ndugu yake wa karibu mwenye madaraka ya kulikomboa, atalikomboa.
26Ikiwa mutu yule hana ndugu mwenye madaraka ya kulikomboa, lakini nyuma akakuwa tajiri na kupata uwezo wa kulikomboa shamba lake,
27basi, atahesabu miaka tangu alipoliuzisha na kulipa garama zake. Yule mutu aliyelinunua anapaswa kumurudishia.
28Lakini ikiwa hana uwezo wa kulikomboa, basi, litabaki katika mikono ya yule aliyelinunua mpaka mwaka wa sikukuu ya ukumbusho wa miaka makumi tano. Katika mwaka huo, mali hiyo iachiliwe na kurudishiwa kwa yule mutu aliyeiuzisha.
29Kama mutu akiuzisha nyumba yake ya kukaa inayokuwa ndani ya muji uliojengewa ukuta, ataweza kuikomboa katika kipindi cha mwaka mumoja tangu alipoiuzisha. Kwa mwaka huo muzima atakuwa na haki ya kuikomboa.
30Kama nyumba inayokuwa katika muji uliojengewa ukuta haikukombolewa kwa muda wa mwaka mumoja, basi, itakuwa mali ya yule aliyeinunua milele katika vizazi vyao vyote, wala haitarudishwa katika mwaka wa sikukuu ya kukumbuka miaka makumi tano.
31Lakini nyumba za vijiji ambavyo havikuzungushiwa ukuta zitakuwa chini ya sheria ileile ya mashamba. Nyumba hizo zinaweza kukombolewa katika mwaka mumoja lakini ni lazima zirudishwe kwa wenyeji katika mwaka wa kukumbuka miaka makumi tano.
32Hata hivyo, nyumba zinazokuwa katika miji Walawi wanayorizi zinaweza kukombolewa wakati wowote.
33Ikiwa mumoja wa Walawi hatumii haki yake ya kukomboa, basi, nyumba iliyouzishwa ni lazima irudishwe kwa mwenyeji katika mwaka wa kukumbuka miaka makuni tano, maana nyumba zinazokuwa katika miji Walawi wanayorizi wamepewa kama sehemu yao kutoka kwa watu wa Israeli.
34Lakini mashamba Walawi wanayorizi kwa pamoja, yasiuzishwe, maana huo ni urizi wao wa kudumu.
Kuwakopesha wamasikini35Kama ndugu yako amekuwa masikini hata asiweze kujitunza mwenyewe akiwa pamoja nawe, unapaswa kumutunza aendelee kuishi nawe ndivyo utakavyomutendea mugeni au musafiri anayekuwa kwako. Ang. Kumb 15.7-8
36Usimwombe akulipe faida ya namna yoyote. Lakini umwogope Mungu, naye ndugu yako apate kuishi pamoja nawe.
37Usimukopeshe feza kwa kupata faida au kumupa chakula kusudi akulipe faida. Ang. Kut 22.25; Kumb 23.19-20
38Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyekutoa kutoka inchi ya Misri kwa kukupa inchi ya Kanana, na kusudi nami nikuwe Mungu wako.
39Kama ndugu yako anayeishi karibu nawe amekuwa masikini, akijiuzisha kwako, usimufanye akutumikie kama mutumwa. Ang. Kut 21.2-6; Kumb 15.12-18
40Atakaa nawe kama mutumishi wa kulipwa au kama musafiri. Atakutumikia mpaka kwa mwaka wa kukumbuka miaka makumi tano.
41Kwa mwaka huo unapaswa kumupa uhuru wake arudi kwa jamaa yake na urizi wa wazee wake, umwache pamoja na jamaa yake.
42Kwa sababu Waisraeli ni watumishi wangu ambao niliwatoa katika inchi ya Misri, basi, wasiuzishwe kama watumwa.
43Usimukamate ndugu yako kwa kinguvu, lakini utamwogopa Mungu wako.
44Juu ya watumwa na wajakazi, unaweza kuwanunua kutoka kwa watu wa mataifa mengine jirani.
45Unaweza vilevile kununua watumwa kutoka kwa wageni wanaokaa pamoja nawe na jamaa zao waliozaliwa katika inchi yenu, nao watakuwa mali yako.
46Hao watumwa unaweza kuwapatia watoto wako wakuwe mali yao milele. Hao unaweza kuwafanya watumwa wako, lakini kuelekea ndugu yako Mwisraeli, usimutawale kwa kinguvu.
47Kama mugeni au musafiri anayekaa kati yenu amekuwa tajiri na ndugu yako akiwa masikini na kujiuzisha kwa huyo mugeni au huyo musafiri au kwa mumoja wa jamaa zao,
48anaweza kukombolewa kisha kujiuzisha, mumoja wa wandugu zake anaweza kumukomboa.
49Mujomba wake anaweza vilevile kumukomboa, au binamu yake au ndugu wa karibu katika ukoo wake. Anaweza vilevile kujikomboa yeye mwenyewe kama akiwa tajiri.
50Yeye akishirikiana na yule aliyemununua, atahesabu miaka tangu alipojiuzisha mpaka mwaka wa kukumbuka miaka makumi tano. Malipo ya kuachiliwa huru kwake italingana na miaka aliyomutumikia. Muda ambao amekuwa mutumwa wa bwana wake utapimwa kama muda wa mutumishi wa kulipiwa.
51Kama hesabu ya miaka mpaka mwaka wa ukumbusho wa miaka makumi tano ni kubwa zaidi, basi atarudisha sehemu kubwa ya bei aliyolipiwa.
52Kama miaka michache imepunguka mbele ya kufikia kwa sikukuu ya ukumbusho wa miaka makumi tano, atahesabu sehemu ya bei iliyobaki kulingana na miaka hiyo na kumulipa hayo malipo.
53Muda wote anapokuwa kwa bwana wake anapaswa kutendewa kama mutumishi wa mushahara kila mwaka. Huyo aliyemununua asimutendee kwa kinguvu.
54Lakini ikiwa mutu huyu na jamaa yake hakukombolewa kwa njia hizo, basi apewe uhuru wake katika mwaka wa ukumbusho wa miaka makumi tano.
55Waisraeli ni watumishi wangu, maana niliwatoa katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.