1Kama mutu yeyote akitakiwa kutoa ushuhuda kwenye baraza juu ya jambo aliloona au kusikia naye akikataa kusema kitu, basi, huo ni uovu na atabeba azabu ya zambi ile.
2Au kama mutu yeyote kati yenu akijichafua bila kukusudia kwa kugusa kitu chochote kichafu, ikuwe ni muzoga wa nyama wa pori au wa kufugwa au wadudu, atakuwa na kosa.
3Au mutu akigusa kitu chochote toka kwa mwanadamu kinachohesabiwa kuwa kichafu, kikuwe kile ambacho kinamufanya mutu kuwa muchafu bila kujua, basi, atakapojua atakuwa na kosa.
4Au, kama mutu akiapa kufanya kitu chochote, chema au kibaya, kama vile watu wanavyofanya bila kufikiri, atakapojua atakuwa na kosa.
5Basi, mutu akiwa na kosa juu ya mambo hayo lazima akubali zambi yake aliyotenda
6na kumuletea Yawe sadaka yake kwa ajili ya kosa. Kwa ajili ya zambi aliyotenda ataleta kondoo dike au mbuzi dike kutoka kundi lake amutoe sadaka kwa ajili ya zambi. Naye kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake.
7Lakini kama hawezi kutoa mwana-kondoo wa sadaka ya kosa kwa ajili ya zambi aliyotenda, basi atamuletea Yawe hua wawili au vitoto viwili vya njiwa, mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa moto.
8Atawaleta kwa kuhani, naye kuhani atamutoa mumoja akuwe sadaka kwa ajili ya zambi kwa kumukongonyoa shingo yake bila kuachanisha kichwa chake.
9Sehemu ya damu yake ataipakaa pembeni ya mazabahu na ile ingine ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi.
10Kisha atamutoa yule wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa kulingana na maagizo. Kuhani atamufanyia yule mutu ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake, naye atasamehewa.
11Ikiwa hawezi kutoa hua wawili au vitoto viwili vya njiwa kama vile sadaka yake kwa ajili ya zambi aliyotenda, basi, ataleta unga kilo moja. Lakini hatautia mafuta wala ubani maana ni sadaka kwa ajili ya zambi.
12Atamuletea kuhani, naye atatwaa unga huo mukono mumoja na kuuteketeza juu ya mazabahu kama sehemu ya ukumbusho, pamoja na sadaka Yawe anazotolewa kwa moto. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi.
13Basi, kuhani atamufanyia yule mutu ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi, naye atasamehewa. Unga unaobaki utakuwa wa kuhani kama vile inavyofanyika juu ya sadaka ya ngano.
Sadaka za malipo ya kosa14Yawe akamwambia Musa:
15Kama mutu yeyote akikosa kwa kutenda zambi bila kujua juu ya kutokutoa vitu vitakatifu Yawe anavyotolewa, atamuletea kondoo dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake. Wewe utapima bei yake kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya kosa.
16Zaidi ya hayo, yule mutu atalipa hasara yote aliyosababisha juu ya vitu vitakatifu kwa kuongeza sehemu moja ya tano ya bei yake na kumupatia kuhani yote. Basi, kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi kwa huyo kondoo dume anayekuwa sadaka kwa ajili ya kosa, naye atasamehewa.
17Mutu yeyote akitenda zambi bila kujua, kwa kuvunja amri yoyote ya Yawe, yeye ana kosa, na atalipa azabu ya kosa lake.
18Atamuletea kuhani kondoo dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake ikiwa na bei sawa na ile ya sadaka ya kosa. Na kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa kosa alilofanya, naye atasamehewa.
19Hiyo ni sadaka ya kosa; yeye ana kosa mbele ya Yawe.
20Yawe akamwambia Musa:
21Ikiwa mutu yeyote ametenda zambi na kumwasi Yawe kwa kumudanganya mwenzake juu ya kitu alichomuwekesha au juu ya mapatano au juu ya kumunyanganya au kumwiba mwenzake,
22au amepata kitu cha mwenzake kilichopotea, akisema kwamba hakukiona, au ameapa uongo juu ya kitu chochote ambacho watu wanafanya na kuwa na kosa,
23mutu yule akitenda zambi na kuwa na kosa, anapaswa kurudisha kile alichoiba au alichonyanganya, au alichowekeshwa, au kitu cha mwenzake kilichopotea akakipata,
24au kitu chochote alichoapa kwa uongo. Atalipa kila kitu kikamilifu na kuongeza sehemu moja ya tano ya bei yake. Mara tu atakapojua kosa lake atamurudishia mwenyeji.
25Kisha atamuletea kuhani kondoo dume au mbuzi dume asiyekuwa na kilema amutolee Yawe sadaka kwa ajili ya kosa. Bei ya nyama huyo itakuwa ile ya kawaida kwa ajili ya kosa.
26Kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho mbele ya Yawe, naye atasamehewa kosa ambalo alikuwa amefanya.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.