1Wimbo wa safari za kidini.
Ee Yawe, umukumbuke Daudi,
kumbuka taabu zote alizopata.
2Ukumbuke ahadi aliyokupa, ee Yawe,
ndicho kiapo alichokuapia, ewe Mwenye Nguvu wa Yakobo.
Alisema:
3“Sitaingia ndani ya nyumba yangu,
wala kulala ndani ya kitanda changu,
4sitakubali kulala usingizi,
wala kusinzia,
5mpaka nikutayarishie wewe Yawe nafasi ya kukaa,
ndiyo makao yako, ewe Mwenye Nguvu wa Yakobo!”
6Tulisikia wakisema: “Sanduku la Agano ni kule Efurata,
tulilikuta katika mashamba ya Yearimu.”
7Basi! Tuende kwa nyumba ya Mungu,
tuabudu mbele ya kiti chake cha kifalme!
8Simama sasa, ee Yawe, ukuje kwenye pumziko lako,
pamoja na Sanduku la Agano la uwezo wako!
9Makuhani wako wakuwe watu wa haki siku zote;
na waaminifu wako wapige vigelegele vya furaha!
10Kwa ajili ya Daudi, mutumishi wako,
usimukatae huyo mufalme uliyemuchagua.
11Yawe alimwapia Daudi kiapo cha hakika,
kiapo hiki ambacho hatakivunja:
“Nitamuweka mumoja wa wazao wako mwenyewe,
kuwa mufalme nyuma yako.
12Watoto wako wakishika agano langu,
na kufuata maagizo nitakayowapa,
watoto wao pia watakuwa wafalme kama wewe milele.”
13Yawe ameuchagua Sayuni,
ametaka ukuwe makao yake.
14Yeye anasema: “Hapa ndipo nitakapokaa milele,
ndipo makao yangu, maana nimepachagua.
15Nitaubariki Sayuni kwa mahitaji yake;
nitawashibisha chakula wamasikini wake.
16Nitawavalisha makuhani wake katika wokovu,
waaminifu wake watapiga vigelegele vya furaha.
17Humo nitamuchipukiza mufalme shujaa wa ukoo wa Daudi.
Kama vile taa inayowaka, nitamwimarisha mufalme niliyemuchagua.
18Waadui zake nitawavalisha haya;
lakini yeye nitamuvalisha utukufu wa kifalme.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.