1Wana wa Yuda walikuwa: Peresi, Hesironi, Karmi, Huri na Sobali.
2Raya mwana wa Sobali, alizaa Yahati, aliyekuwa baba ya Ahumai na Lahadi, hizo ndizo jamaa za Wazorati.
3Wana wa Etamu walikuwa: Yezereheli, Isima na Idubasi. Walikuwa na dada mumoja aliyeitwa Hasilelponi.
4Penueli alizaa Gedori na Ezeri, na Ezeri alizaa Husa. Hawa ndio wazao wa Huri muzaliwa wa kwanza wa Efurata, watu wa muji wa Betelehemu.
5Asuri, mwanzilishi wa muji wa Tekoa, alikuwa na wake wawili: Hela na Nara.
6Nara akamuzalia wana wane: Ahuzamu, Heferi, Temeni na Ahastari.
7Hela akamuzalia wana watatu: Zereti, Izihari na Etinani.
8Hakosi alizaa Anubu na Zobeba, na ndiye aliyekuwa baba wa jamaa za wazao wa Aharheli mwana wa Harumu.
9Kulikuwa mutu mumoja jina lake Yabesi, aliyeheshimiwa kuliko wandugu zake wote. Mama yake alimupa jina la Yebesi kwa sababu alizaa kwa maumivu.
10Lakini Yebesi alimwomba Mungu wa Israeli akisema: “Ee Mungu, ninakusihi unibariki na kupanua mipaka yangu. Mukono wako ukuwe pamoja nami na unilinde kutokana na jambo lolote ovu, na mateso yasinipate.” Naye Mungu akamupa yale aliyoomba.
11Kelubi, ndugu ya Sua, alizaa Mehiri.
Mehiri alizaa Estoni.
12Estoni alizaa: Beti-Rafa, Pasea na Tehina. Tehina alikuwa mwanzilishi wa muji wa Iri-Nahasi. Wazao wa watu hawa waliishi Reka.
13Wana wa Kenasi walikuwa: Otieli na Seraya.
Wana wa Otieli walikuwa: Hatati na Meonotai.
14Meonotai alizaa Ofura.
Seraya alizaa Yoabu, mwanzilishi wa Bonde la Wafundi, lililopewa jina hilo kwa sababu wote waliokuwa mule walikuwa wafundi kabisa.
15Wana wa Kalebu, mwana wa Yefune, walikuwa: Iru, Ela na Nama.
Mwana wa Ela alikuwa Kenasi.
16Wana wa Yehaleli walikuwa: Zifu, Sifa, Tiria na Asareli.
17Wana wa Ezra walikuwa: Yeteri, Meredi, Eferi na Yaloni.
Meredi akamwoa Bitia, binti ya Mufalme wa Misri, na hawa ndio wana aliomuzalia Meredi: Miriamu, Samai na Isiba, mwanzilishi wa muji wa Estemoa.
18Meredi alikuwa na muke mwingine Muyuda. Huyu akamuzalia: Yeredi, mwanzilishi wa muji wa Gedori, Heberi, mwanzilishi wa muji wa Soko, na Yekutieli, mwanzilishi wa muji wa Zanoa.
19Hodia akaoa dada ya Nahamu ambaye wazao wake ndio waanzilishi wa: kabila la Garmi, lililoishi katika muji wa Keila; na kabila la Makati, lililoishi katika muji wa Estemoa.
20Wana wa Simoni walikuwa: Amunoni, Rina, Beni-Hanani na Tiloni.
Isi alikuwa na wana wawili: Zoheti na Beni-Zoheti.
Wazao wa Sela21Wana wa Sela mwana wa Yuda, walikuwa: Eri, mwanzilishi wa muji wa Leka; Lada, mwanzilishi wa muji wa Maresa, ukoo wa wafuma nguo za kitani waliokuwa wakiishi katika muji wa Beti-Asibea;
22Yokimu na watu walioishi katika muji wa Kozeba; na Yoasi na Sarafu waliotawala kule Moabu na wakarudia Lehemu. (Habari hizi ni za zamani sana.)
23Hawa ndio wafinyanzi walioishi katika miji ya Netaimu na Gedera, wakimutumikia mufalme.
Wazao wa Simeoni24Simeoni alikuwa na wana watano: Nemueli, Yamina, Yaribu, Zera na Saulo.
25-26Saulo alizaa Salumu,
Salumu alizaa Mibusamu,
Mibusamu alizaa Misma.
Misma alizaa Hamueli,
Hamueli alizaa Zakuri,
Zakuri alizaa Simei.
27-33Simei alikuwa na wana kumi na sita na wabinti sita, lakini wandugu zake hawakukuwa na wana wengi, na jamaa yake vilevile haikuongezeka kama kabila la Yuda. Miji walimokuwa wakiishi mpaka wakati wa utawala wa mufalme Daudi ilikuwa: Beri-Seba, Molada, Hasari-Suali, Biliha, Ezemi, Toladi, Betueli, Horma, Ziklagi, Beti-Makaboti, Hasari-Susimu, Beti-Biri na Sarayimu, Etamu, Aini, Rimoni, Tokeni na Asani, pamoja na vijiji kandokando ya miji hiyo mpaka Bali. Hayo ndiyo yaliyokuwa makao yao, nao wakaandika majina yao katika vitabu vya vizazi vyao.
34-38Watu hawa ndio walikuwa wakubwa wa ukoo zao: Mesobabu, Yamleki, Yosa mwana wa Amazia, Yoeli, Yehu (mwana wa Yosibia, mujukuu wa Seraya, mwana wa Asieli), Eliyoenai, Yakoba, Yesohaya, Asaya, Adieli, Yesimieli, Benaya, Ziza (mwana wa Sifi, mujukuu wa Aloni, wa uzao wa Yedaya, wa Simuri na wa Semaya).
Jamaa zao waliongezeka kwa wingi sana.
39Walitawanyika mpaka kwenye mulango wa muji wa Gedori, upande wa mashariki wa bonde, kwa kuwatafutia kondoo wao malisho.
40Kule, walipata malisho tele, tena mazuri sana na tena inchi ilikuwa wazi, tulivu na yenye amani, maana wenyeji wa inchi hiyo wa zamani walikuwa wazao wa Hamu.
41Katika siku za utawala wa mufalme Hezekia wa Yuda, watu wale waliotajwa majina yao walikwenda kule Gedori, wakaharibu hema za Wameuni waliokuwa wakiishi kule na kuwafukuza kabisa mpaka leo. Wakafanya makao yao ya kudumu kule kwa sababu kulikuwa malisho tele kwa ajili ya kondoo wao.
42Watu wengine wa kabila la Simeoni yapata mia tano walikwenda mpaka kwenye mulima Seiri. Waliongozwa na Pelatia, Nearia, Refaya na Usieli, wana wa Isi.
43Kule wakawaua Waamaleki waliobaki kisha kuponyoka nao wakaishi kule mpaka leo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.