1“Umwandikie malaika wa kanisa la Efeso hivi:
“Ujumbe huu unatoka kwa yule anayeshika nyota saba katika mukono wake wa kuume na anayetembea katikati ya vinara saba vya taa vya zahabu.
2Ninajua matendo yako na taabu yako na uvumilivu wako. Ninajua kwamba hauwezi kuwakubali watu waovu. Umewapima wale wanaojiita mitume, kumbe si mitume, nawe ukatambua kwamba ni wasema uongo.
3Wewe ni muvumilivu; umeteswa kwa ajili ya jina langu, lakini haukuregea.
4Lakini niko na neno moja juu yako: wewe hauna tena upendo kwangu kama vile mbele.
5Basi kumbuka jinsi ulivyokuwa ulipokuwa haujaanguka, ugeuke toka zambi zako na kurudilia yale matendo yako ya kwanza. Kama usipogeuka toka zambi zako, nitakuja kwako na kuongoa kinara chako toka pahali pake.
6Lakini uko na neno hili zuri: unachukia matendo ya Wanikolayi kama vile ninavyoyachukia.
7“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa!
“Yule atakayeshinda nitamupa ruhusa ya kula matunda ya muti wa uzima unaokuwa katika bustani ya Mungu!
Ujumbe kwa kanisa la Smurna8“Umwandikie malaika wa kanisa la Smurna hivi:
“Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa wa kwanza na wa mwisho, aliyekuwa amekufa lakini sasa ni muzima.
9Ninajua mateso yako na umasikini wako, lakini wewe ni tajiri! Vilevile ninajua jinsi unavyotukanwa na wale wanaojidai kuwa Wayuda lakini si Wayuda; wao ni kikundi cha wenye kuabudu Shetani!
10Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.
11“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoambia makanisa!
“Yule atakayeshinda hatapatwa na kifo cha pili.
Ujumbe kwa kanisa la Pergamo12“Umwandikie malaika wa kanisa la Pergamo hivi:
“Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa na upanga wenye makali ngambo zote mbili.
13Ninajua pahali pale unapokaa, ile ndiyo nafasi ya utawala wa Shetani. Wewe unashikamana na jina langu, wala haukuikana imani unayokuwa nayo kwangu, hata wakati Antipa, mushuhuda wangu mwaminifu, alipouawa kati yenu kule kwenye makao ya Shetani.
14Lakini niko na neno hili juu yako: kati yako kuna watu wamoja wanaoshika mafundisho ya Balama. Huyu ndiye aliyemufundisha Balaka kwamba awapime Waisraeli, kusudi wakule vyakula vya kutambikia sanamu za miungu na kufanya uasherati.
15Na zaidi ya hii kati yako kuna watu wanaoshika mafundisho ya Wanikolayi vilevile.
16Basi ugeuke toka zambi zako, kwa maana kama si vile nitakuja kwako upesi, nami nitapigana na watu wale kwa upanga unaotoka ndani ya kinywa changu.
17“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa!
“Yule atakayeshinda, nitamupa ile mana iliyofichwa. Na nitamupa vilevile jiwe dogo jeupe, na juu yake kumeandikwa jina jipya ambalo hakuna mutu yeyote anayelijua, isipokuwa tu yule anayelipewa.
Ujumbe kwa kanisa la Tuatera18“Umwandikie malaika wa kanisa la Tuatera hivi:
“Ujumbe huu unatoka kwa Mwana wa Mungu, anayekuwa na macho yanayometameta kama ndimi za moto, na miguu inayongaa kama shaba iliyosafishwa vizuri sana.
19Ninajua matendo yako, upendo wako, imani yako, kazi yako na uvumilivu wako. Ninajua kwamba sasa unajitolea kwa kunitumikia kuliko mbele.
20Lakini niko na neno hili juu yako: unamuvumilia yule mwanamuke Yezebeli, anayejiita kuwa nabii wa Mungu. Yeye anawapotosha watumishi wangu akiwafundisha kufanya uasherati na kula nyama za kutambikia sanamu za miungu.
21Nimemwachia wakati wa kugeuka toka zambi zake, lakini hataki kuacha uasherati wake.
22Basi nitamupiga kwa ugonjwa na kuleta mateso makubwa vilevile kwa wale wanaozini pamoja naye ikiwa hawaachi matendo yao.
23Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.
24“Lakini ninyi watu wengine wa kanisa la Tuatera musiofuata hayo mafundisho ya Yezebeli, na ambao hamujui ile wanayoita ‘Siri za Shetani’, ninawaambia ninyi kama sitawabebesha muzigo mwingine.
25Lakini ninawaomba tu mushikamane na kile munachokuwa nacho mpaka nitakapokuja.
26Na yule atakayeshinda na kuendelea kufuata mapenzi yangu mpaka mwisho, nitamupa mamlaka ya kutawala mataifa.
27Atayatawala kwa fimbo ya chuma na kuyaponda kama vile mutungi,
28akiwa na uwezo sawa ule uliopewa na Baba yangu. Na zaidi ya ile nitamupa nyota ya asubui.
29“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.