1Katika mwaka wa ine wa utawala wa mufalme Yoyakimu wa Yuda mwana wa Yosia, ujumbe huu wa Yawe ukatolewa kwa Yeremia:
2Twaa kizingo cha kitabu uandike humo maneno yote niliyokuambia juu ya Israeli, juu ya Yuda na mataifa yote, tangu siku nilipoanza kusema nawe, wakati Yosia alipokuwa mufalme mpaka leo.
3Labda watu wa Yuda watasikia juu ya hasara zote ambazo nimekusudia kuwatendea, kusudi kila mumoja wao auache mwenendo wake mubaya, nami nipate kuwasamehe makosa yao na zambi yao.
4Halafu Yeremia akamwita Baruku mwana wa Neria. Naye Baruku akaandika katika kitabu maneno yote yaliyotoka katika kinywa cha Yeremia sawa vile Yawe alivyokuwa amemwambia.
5Kisha, Yeremia akamupa Baruku maagizo haya: Mimi siruhusiwi kwenda katika nyumba ya Yawe.
6Lakini kwa siku ya kwanza ya kufunga kula chakula, wewe utakwenda mbele ya watu wote, ndani ya nyumba ya Yawe, usome kitabu chenye maneno ya Yawe uliyoyaandika kutoka katika kinywa changu. Utayasoma maneno hayo mbele ya watu wote wa Yuda waliofika kutoka miji yao vilevile.
7Labda maombi yao yatamufikia Yawe na kila mumoja wao ataacha mwenendo wake mubaya kwa maana hasira na kasirani ambavyo Yawe amesema juu ya watu hawa ni kubwa sana.
8Basi, Baruku mwana wa Neria alitimiza yote aliyoamuriwa na nabii Yeremia juu ya kusoma maneno ya Yawe ndani ya nyumba ya Yawe kutoka katika kitabu hicho.
9Katika mwaka wa tano wa utawala wa mufalme Yoyakimu wa Yuda mwana wa Yosia, katika mwezi wa kenda, wakaaji wote wa Yerusalema na watu wote waliofika Yerusalema kutoka miji ya Yuda, walitangaza siku ya kufunga kula chakula mbele ya Yawe.
10Basi, Baruku alisoma maneno ya Yeremia kutoka katika kile kitabu mbele ya watu wote, ndani ya nyumba ya Yawe, katika chumba cha Gemaria mwana wa Safanu aliyekuwa katibu. Chumba hicho kilikuwa katika baraza la juu, kwenye mulango mupya wa nyumba ya Yawe.
Wakubwa wanasomewa kitabu kilichoandikwa11Mikaya mwana wa Gemaria, mujukuu wa Safanu, aliposikia maneno yote ya Yawe ambayo yalisomwa kutoka kile kitabu,
12alikwenda kwenye nyumba ya kifalme na kuingia katika chumba cha katibu. Mule mulikuwa wakubwa wote: katibu Elisama, Delaya mwana wa Semaya, Elnatana mwana wa Akibori, Gemaria mwana wa Safanu, Zedekia mwana wa Hanania, na wakubwa wote.
13Mikaya aliwaambia maneno yote aliyoyasikia wakati Baruku aliposoma kitabu mbele ya watu.
14Kisha, wakubwa wakamutuma Yehudi mwana wa Netania, mujukuu wa Selemia, kijukuu cha Kusi, amwambie Baruku hivi: Twaa kile kitabu ulichosoma mbele ya watu ukuje nacho hapa. Basi, Baruku mwana wa Neria akatwaa kitabu katika mukono wake, akawaendea.
15Nao wakamwambia: Ikaa, ukisome. Baruku akawasomea.
16Waliposikia maneno hayo yote, waliangaliana kwa hofu. Wakamwambia Baruku: Tunapaswa kumwelezea mufalme maneno haya yote.
17Kisha wakamwuliza Baruku: Basi utuambie, umepata namna gani kuandika maneno haya yote? Yeremia alisema, nawe ukayaandika?
18Baruku akawajibu: Yeye alisema, nami nikayaandika kwa wino katika kitabu hiki.
19Kisha wakubwa hao wakamwambia Baruku: Wewe uende ujifiche pamoja na Yeremia, na kusikuwe mutu yeyote atakayejua pahali munapokuwa.
Mufalme anachoma kitabu20Wale wakubwa walipokwisha kuweka kitabu kile katika chumba cha Elisama katibu wa mufalme, walimwendea mufalme ndani ya kiwanja, wakamujulisha mambo yote.
21Kisha, mufalme alimutuma Yehudi aende kuleta kile kitabu. Yehudi alikitwaa kutoka ndani ya chumba cha katibu Elisama, akamusomea mufalme na wakubwa wote waliokuwa wamesimama karibu na mufalme.
22Wakati huo ulikuwa mwezi wa kenda, na mufalme alikuwa ndani ya nyumba yake ya nyakati za baridi. Mbele yake kulikuwa moto wa makaa.
23Yehudi alipokuwa amekwisha kusoma vipindi vitatu au vine hivi vya kitabu kile, mufalme alivikatakata kwa kisu na kuvitupa katika moto wa makaa. Aliendelea kufanya hivyo mpaka kitabu chote kikateketezwa.
24Lakini, ingawa mufalme na watumishi wake wote waliyasikia maneno hayo yote, hawakuogopa wala kurarua nguo zao kwa huzuni.
25Ijapokuwa Elnatana, Delaya na Gemaria walimusihi mufalme asikichome kile kitabu, mufalme hakuwasikiliza.
26Mufalme alimwamuru mwana wake Yerameli, Seraya mwana wa Azirieli na Selemia mwana wa Abudieli, wamukamate katibu Baruku na nabii Yeremia. Lakini Yawe aliwaficha.
Yeremia anaandika barua ingine27Mufalme alipokwisha kuchoma kwa moto kile kitabu ambacho Baruku aliandika kwa maagizo ya Yeremia, neno la Yawe lilimufikia Yeremia kusema hivi:
28Twaa kitabu kingine, uandike maneno yote yaliyokuwa katika kile cha kwanza ambacho Yoyakimu, mufalme wa Yuda, amechoma kwa moto.
29Nawe utamwambia huyo Yoyakimu mufalme wa Yuda kwamba:
Yawe anasema hivi: Umekichoma kwa moto kitabu hicho na kuuliza kwa nini Yeremia ameandika kwamba mufalme wa Babeli atakuja kuiharibu inchi hii na kuwaangamiza watu na nyama!
30Basi, Yawe anasema hivi juu yake yeye Yoyakimu mufalme wa Yuda: Yeye hatakuwa na mutu wa uzao wake atakayeikalia kiti cha kifalme cha Daudi, na maiti yake itatupwa inje kwenye joto muchana na baridi kali usiku.
31Nami nitamwazibu yeye na wazao wake pamoja na watumishi wake kwa sababu ya uovu wao. Nitawaletea wao na wakaaji wote wa Yerusalema pamoja na watu wote wa Yuda hasara yote niliyosema juu yao na ambayo hawakuijali.
32Kisha, Yeremia alitwaa kitabu kingine, akamupa katibu Baruku mwana wa Neria, ambaye aliandika humo maneno yote aliyoambiwa na Yeremia ambayo yalikuwa katika kile kitabu cha mbele ambacho Yoyakimu, mufalme wa Yuda, alichoma kwa moto. Maneno mengine ya namna hiyo yaliongezwa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.