1Agripa akamwambia Paulo: “Sasa unaweza kueleza maneno yako.”
Basi Paulo akanyoosha mukono na kuanza kujitetea, akisema:
2“Mufalme Agripa, ninafurahi sana kusimama mbele yako leo kwa kujitetea juu ya mambo yote Wayuda waliyonishitakia.
3Ninafurahi zaidi kwa sababu wewe unajua sana desturi zote za Wayuda na mabishano yao yote. Basi ninakuomba unisikilize kwa uvumilivu.
4“Wayuda wote wanajua maisha yangu tangu mwanzo wa ujana wangu. Wanajua namna nilivyoishi kati ya taifa langu katika Yerusalema.
5Wamenijua tangu zamani na kama wakitaka wanaweza kushuhudia kwamba nilikuwa mushiriki wa chama cha Wafarisayo, kinachotia mukazo sana juu ya kushika desturi za dini yetu.
6Na sasa ninasimama hapa kuhukumiwa kwa sababu ninatumainia ile ahadi Mungu aliyotoa kwa babu zetu.
7Makabila yetu kumi na mawili wanamwabudu Mungu usiku na muchana, kwa maana wanatumaini kuona utimilifu wa ile ahadi. Na ni kwa sababu ya tumaini lile, Ee mufalme, Wayuda wananishitaki.
8Kwa sababu gani ninyi munazani kwamba haiwezekani kwa mutu kusadiki kwamba Mungu anawafufua wafu?
9“Kweli mimi mwenyewe niliwaza kwamba nilipaswa kufanya yote ninayoweza kwa kupinga jina la Yesu wa Nazareti.
10Na ni vile nilivyofanya katika Yerusalema. Nilipata mamlaka toka kwa wakubwa wa makuhani; nami nikawatia watu watakatifu wengi wa Mungu katika kifungo. Na wakati walipowaua mimi nilikubali kwamba wanastahili kuuawa.
11Mara nyingi niliwaazibu katika nyumba za kuabudia na kuwashurutisha wakane imani yao. Niliwakasirikia kupita kipimo, hata nikaenda kuwatesa katika miji ya inchi za kigeni.
Paulo anaeleza namna alivyookoka(Mdo 9.1-19; 22.6-16)12“Basi kufuatana na kusudi, nikaenda katika muji Damasiki kwa amri na mamlaka ya wakubwa wa makuhani.
13Ee mufalme, nilipokuwa katika njia, ilipotimia saa sita ya muchana, nikaona mwangaza unaotoka mbinguni unaopita mwangaza wa jua. Mwangaza ule ukanizunguka pamoja na wenzangu waliosafiri nami.
14Sisi wote tukaanguka chini, na nikasikia sauti iliyoniambia hivi katika luga ya Kiebrania: ‘Saulo, Saulo, kwa sababu gani unanitesa? Unajiumiza bure kama ngombe anayepiga teke kwenye chongo ya fimbo ya mwenyeji wake.’
15Halafu nikauliza: ‘Wewe ni nani, Bwana?’ Na Bwana akajibu: ‘Mimi ni Yesu, unayemutesa.
16Lakini sasa inuka usimame wima. Nimekutokea kusudi nikuweke kuwa mutumishi wangu. Wewe utatoa ushuhuda juu yangu; utawaelezea watu mambo uliyoona leo na yale nitakayokuonyesha nyuma.
17Nitakuokoa toka mikono ya taifa lako la Waisraeli na ya watu wa mataifa mengine. Ninakutuma kwao
18kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’
Paulo anasema juu ya kazi yake19“Kwa sababu hii, Ee mufalme Agripa, mimi nikafanya sawa nilivyoagizwa katika maono yale yaliyotoka mbinguni.
20Lakini kwanza nilihubiri wakaaji wa Damasiki, na wa Yerusalema na wa jimbo lote la Yudea nao watu wa mataifa mengine vilevile. Nilihubiri kwao kwamba wageuke toka zambi zao na kumurudilia Mungu, nao waonyeshe kwa njia ya matendo yao kwamba wamegeuka.
21Ni kwa sababu ya maneno hayo Wayuda walinikamata ndani ya hekalu na kutaka kuniua.
22Lakini kwa ulinzi wa Mungu ningali muzima hata leo. Nami ninatoa ushuhuda kwa wadogo na wakubwa, wala sisemi maneno mengine yanayokuwa mbali na yale manabii na Musa waliyosema kwamba yatatokea.
23Wao walitangaza kwamba Kristo anapaswa kuteswa na kuwa wa kwanza kufufuka kati ya wote waliokufa, naye atahubiri kwa Wayuda na kwa watu wa mataifa mengine kwamba kwa njia ya kuokolewa wataweza kuishi katika mwangaza.”
Paulo anataka Agripa aamini24Paulo alipokuwa akijitetea vile, Festo akamwambia kwa sauti kubwa: “Wewe Paulo, uko na wazimu! Elimu yako nyingi imekuvuruga kichwa.”
25Paulo akamujibu: “Muheshimiwa Festo, mimi si mwenda-wazimu. Maneno ninayosema ni ya kweli nayo ni ya maana.
26Mufalme Agripa anajua vizuri mambo yale yaliyotokea. Nami ninaweza kusema mbele yake pasipo woga kwa maana ninajua hakika kwamba hakuna hata jambo kati ya hayo asilofahamu, kwa sababu hayakufanyika kwa uficho.
27Ee Mufalme Agripa, unaamini maneno manabii waliyosema? Ninajua kama unayaamini!”
28Naye Agripa akamwambia Paulo: “Unazani kwamba kwa wakati kidogo utaweza kunivuta kuwa mukristo?”
29Paulo akajibu: “Ikiwa wakati kidogo au wakati murefu, ninamwomba Mungu, si juu yako wewe mwenyewe tu, lakini hata hawa wote wanaonisikiliza leo wapate kuwa sawa mimi, lakini wasifikie tu kutiwa katika kifungo!”
30Halafu mufalme, liwali, Berenike na wote wengine walioikaa pamoja nao wakasimama.
31Nao walipokwisha kuondoka wakasemezana: “Mutu huyu hakutenda neno linalomupasa kuuawa wala kufungwa.”
32Agripa akamwambia Festo: “Mutu huyu angeweza kufunguliwa, kama isingekuwa ameomba maneno yake yakatwe na Mufalme wa Roma.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.