1Haya ndiyo makundi ya Walawi waliofanya kazi za ulinzi.
Kutoka katika ukoo wa Kora, kulikuwa Meselemia mwana wa Kora wa jamaa ya Asafu.
2Meselemia alikuwa na wana saba: Zekaria muzaliwa wake wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yatinieli wa ine,
3Elamu wa tano, Yohanani wa sita na Eliehoenai wa saba.
4Vilevile kulikuwa Obedi-Edomu, ambaye Mungu alimubariki kwa kumupa wana wanane: Semaya muzaliwa wake wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa ine, Netaneli wa tano, Ang. 2 Sam 6.11; 1 Sik 13.14
5Amieli wa sita, Isakari wa saba na Peuletayi wa nane.
6Mwana wake Semaya alizaa wana. Walikuwa na mamlaka juu ya jamaa ya baba yao kwa sababu walikuwa wanaume wenye uwezo mukubwa.
7Wana wa Semaya walikuwa: Otini, Refaeli, Obedi, Elizabadi, wandugu zake walikuwa mashujaa, Elihu na Semakia.
8Hao wote walikuwa wana wa Obedi-Edomu; wao na wana wao na wandugu zao, walikuwa watu hodari katika utumishi wao. Wazao wote wa Obedi-Edomu walikuwa makumi sita na wawili.
9Naye Meselemia alikuwa na wana na wandugu zake; watu wenye uwezo kumi na wane.
10Hosa mumoja kati ya wana wa Merari alikuwa na wana wane: Simuri (aliyefanywa kiongozi na baba yake hata ingawa hakukuwa muzaliwa wa kwanza),
11Hilkia wa pili, Tebalia wa tatu na Zekaria wa ine. Wana wote wa Hosa pamoja na wandugu zao walikuwa kumi na watatu.
12Hao walinzi wa milango waligawanyika katika makundi kulingana na jamaa zao, nao vilevile walipangiwa kazi kwenye nyumba ya Yawe kama wale Walawi wengine.
13Kila jamaa, bila kujali wingi ilipiga kura kwa kuchagua mulango watakaosimamia.
14Kura ya kuchagua wa kulinda mulango wa upande wa mashariki ikamwangukia Selemia. Wakapiga kura vilevile kwa ajili ya mwana wake Zekaria, aliyekuwa mushauri mwenye hekima, ikamwangukia kura ya mulango wa upande wa kaskazini.
15Obedi-Edomu akaangukiwa na kura ya mulango wa upande wa kusini. Wana wake wakaangukiwa na kura ya gala.
16Supimu na Hosa wakaangukiwa na kura ya kulinda mulango wa upande wa magaribi kwenye mulango wa Saleketi kwenye barabara ya juu. Ulinzi ulifanywa kwa zamu.
17Kila siku upande wa mashariki kulikuwa walinzi sita, kaskazini wane, na kusini wane, vilevile kwenye gala kuliwekwa walinzi wawili wawili;
18na kwenye banda zuri lililokuwa upande wa magaribi, kulikuwa walinzi wane katika barabara na wawili kwenye banda lenyewe.
19Haya ndiyo makundi ya walinzi kati ya ukoo wa Kora na ya wazao wa Merari waliofanya kazi ya ulinzi wa milango.
Kazi nyingine za hekalu20Kati ya Walawi, Ahia alielekea uangalizi wa hazina ya nyumba ya Mungu, na hazina na vitu vitakatifu.
21Ladani, mumoja wa ukoo wa Gersoni, alikuwa babu wa jamaa nyingi, kati yao kukiwa jamaa ya mwana wake Yehieli.
22Wana wengine wawili wa Ladani, Zetamu na Yoeli, walikuwa wachungaji wa hazina ya nyumba ya Yawe.
23Vilevile kazi ziligawanywa kwa watu wa ukoo za Waamuramu, Waisihari, Wahebroni na Wauzieli.
24Sebueli mwana wa Gersoni, mujukuu wa Musa, alikuwa musimamizi mukubwa wa hazina zile.
25Na ndugu yake, alikuwa Eliezeri, aliyekuwa baba ya Rehabia. Rehabia alikuwa baba ya Yesaya, aliyemuzaa Yoramu, Yoramu alizaa Zikiri, Zikiri alizaa Selomoti.
26Selomoti na wandugu zake, ndio waliokuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vitakatifu ambavyo mufalme Daudi alitoa kwa Mungu, viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu na mamia na majemadari wa jeshi.
27Walichunga sehemu ya vitu walivyonyanganya katika vita kwa ajili ya kutengeneza nyumba ya Yawe.
28Vilevile vitu vyote vilivyotolewa kwa Mungu na nabii Samweli na Saulo mwana wa Kisi, na Abeneri, na Yoabu mwana wa Zeruya, vilikuwa chini ya uangalizi wa Selomiti na wandugu zake.
Kazi za Walawi wengine29Kati ya watu wa ukoo wa Isiari, Kenania na wana wake walipewa kazi za utawala kama kusimamia watu na waamuzi, kwa ajili ya Waisraeli.
30Kati ya watu wa ukoo wa Hebroni, Hasabia na wandugu zake elfu moja na mia saba, wote watu mashujaa walipewa kazi ya kusimamia sehemu za inchi ya Israeli zilizokuwa upande wa magaribi wa muto Yordani. Walisimamia kazi yote ya Yawe na kazi za mufalme Daudi.
31Kati ya watu wa ukoo wa Hebroni, Yeria alikuwa kiongozi wa ukoo na jamaa zote, na katika mwaka wa makumi ine wa utawala wa mufalme Daudi, uchunguzi ulifanywa na wanaume wenye uwezo mukubwa wakapatikana kule Yezeri katika jimbo la Gileadi.
32Mufalme Daudi alimuchagua Yeriya na wandugu zake elfu mbili na mia saba, mashujaa na viongozi wa ukoo, kwa kusimamia mambo yote yaliyoelekea Mungu na mufalme Daudi katika sehemu za watu wa ukoo wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, zilizokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.