1Mufalme Daudi akawaambia wale watu wote waliokusanyika: “Solomono mwana wangu, ambaye peke yake amechaguliwa na Mungu, angali bado mudogo, hana maarifa mengi na kazi hii ni kubwa. Nyumba atakayojenga si ya mwanadamu, lakini ni ya Mungu, Yawe. Ang. 1 Sik 22.5
2Basi nimejitia kwa kadiri ya uwezo wangu wote kwa kuwekea nyumba ya Mungu wangu, akiba ya zahabu ya kutengeneza vitu vya zahabu, feza ya kutengeneza vitu vya feza, shaba ya kutengeneza vitu vya shaba, chuma cha kutengeneza vitu vya chuma, na miti ya kutengeneza vitu vya miti. Zaidi ya hayo, nimetayarisha kwa wingi mawe ya rangi na mawe ya kupamba, mawe ya kuchorwa, mawe ya bei kali ya kila namna na marumaru.
3Tena zaidi ya vyote nilivyotoa kwa ajili ya nyumba takatifu, nina hazina yangu ya pekee ya zahabu na feza, na kwa sababu ninapenda nyumba ya Mungu wangu ninaitoa kwa nyumba ya Mungu wangu;
4ni toni mia moja za zahabu kutoka Ofiri, toni yapata mia mbili za feza safi ya kuzifunikia kuta za nyumba,
5na kwa ajili ya kutengeneza vitu vya kila aina vitakavyotengenezwa na wafundi kwa mikono. Nimeweka zahabu kwa ajili ya vyombo vya zahabu, na feza kwa ajili ya vyombo vya feza. Ni nani basi atakayemutolea Yawe kwa mapenzi yake kusudi ajitoe hivi leo kwa Yawe?”
6Basi wakubwa wa ukoo, viongozi wa makabila ya Israeli, majemadari wa maelfu na wa mamia; vilevile na wakubwa wasimamizi wa kazi za mufalme walipotoa kwa mapenzi yao,
7walitoa kwa ajili ya kazi za nyumba ya Mungu: toni mia moja makumi saba za zahabu, vikoroti elfu kumi vya zahabu, na zaidi ya toni mia tatu za feza, yapata toni mia sita za shaba, na zaidi ya toni elfu mia tatu za chuma.
8Wale ambao walikuwa na mawe ya bei kali wakayatoa kusudi yawekwe katika hazina ya nyumba ya Yawe, chini ya uangalizi wa Yehieli, Mugersoni.
9Halafu watu wakafurahi kwa sababu walitoa kwa mapenzi yao, maana kwa moyo wao wote walimutolea Yawe kwa mapenzi yao, naye mufalme Daudi akafurahi sana.
Daudi anamusifu Mungu10Halafu Daudi akamutukuza Yawe mbele ya mukutano wote, akisema: “Utukuzwe milele na milele, ee Yawe, Mungu wa baba yetu Israeli.
11Ukubwa ni wako, ee Yawe, una nguvu, utukufu, ushindi na mamlaka. Vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia ni vyako. Ee Yawe, ufalme ni wako, nawe umetukuzwa, uko mukubwa juu ya vitu vyote. Ang. Mat 6.13
12Utajiri na heshima vinatoka kwako, vyote unavitawala. Uwezo na nguvu viko katika mukono wako, nawe unawatukuza wale unaowapenda, na kuwaimarisha wote.
13Sasa, ee Mungu wetu, tunakushukuru na kusifu jina lako tukufu.
14“Lakini, mimi ni nani, na watu wangu ni nani, hata tuweze kutoa kwa mapenzi yetu hivi? Kwa maana vitu vyote vinatoka kwako, tumekutolea vitu vinavyokuwa vyako wewe mwenyewe.
15Sisi tuko wageni mbele yako, na wasafiri kama vile babu zetu walivyokuwa wote. Siku zetu katika dunia ni kama kivuli kinachopita, hapa hakuna tumaini la kukaa.
16Ee Yawe, Mungu wetu, wingi wote huu tuliotoa kwa kukujenga nyumba kwa ajili ya utukufu wa jina lako takatifu, unatoka katika mukono wako na yote ni yako.
17Ninajua, Mungu wangu, kwamba wewe unapima moyo, nawe unapendezwa na uaminifu. Nami, katika uaminifu wa moyo wangu nimetoa vitu hivi vyote kwa mapenzi yangu, na sasa ninaona watu wako wanaokuwa hapa, wakikutolea kwa mapenzi yao na furaha.
18Ee Yawe, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Israeli, babu zetu, ulinde mupango wa namna hiyo na mafikiri ya namna hiyo ndani ya mioyo ya watu wako, na uelekeze mioyo ya watu wako kwako.
19Umujalie Solomono mwana wangu kusudi kwa moyo wote ashike amri zako, ushuhuda na maagizo yako, atimize yote na apate kujenga nyumba hii ya utukufu niliyoifanyia matayarisho.”
20Kisha, mufalme Daudi akawaambia wote waliokusanyika: “Mumusifu Yawe, Mungu wenu.” Na wote waliokusanyika wakamutukuza Yawe, Mungu wa babu zao, wakainama mbele yake na kumwabudu Yawe na kumutolea mufalme Daudi heshima.
21Wakamutolea Yawe sadaka. Kesho yake wakamutolea sadaka za kuteketezwa kwa moto: ngombe dume elfu moja, wana-kondoo elfu moja, pamoja na sadaka zao za vinywaji na sadaka nyingi kwa ajili ya Waisraeli wote.
22Basi siku ile wakakula na kunywa kwa furaha kubwa mbele ya Yawe.
Kwa mara ya pili wakamuweka Solomono mwana wa Daudi kuwa mufalme. Wakamupakaa mafuta apate kuwa mutawala katika jina la Yawe, na Zadoki akuwe kuhani.
23Halafu Solomono akaikaa katika kiti cha kifalme cha Yawe, kwa pahali pa baba yake Daudi. Naye akafanikiwa; na taifa lote la Waisraeli likamutii. 29.23 Ang. 1 Fal 2.12
24Viongozi wote na mashujaa vilevile na wana wote wa mufalme Daudi, wakaahidi kuwa watiifu kwa mufalme Solomono.
25Yawe akamupa Solomono sifa nzuri mbele ya Waisraeli wote, akamupa utukufu wa kifalme unaopita utukufu wa mufalme yeyote aliyeitawala inchi ya Israeli mbele yake.
Kifupi cha utawala wa Daudi26Basi Daudi, mwana wa Yese, akakuwa mufalme juu ya inchi yote ya Israeli.
27Na muda aliotawala juu ya inchi ya Israeli ulikuwa miaka makumi ine; miaka saba alitawala akiwa Hebroni na miaka makumi tatu na mitatu alitawala akiwa Yerusalema. Ang. 2 Sam 5.4-5; 1 Sik 3.4
28Alikufa akiwa muzee sana, alishiba siku, akiwa na mali na heshima. Mwana wake Solomono akakuwa mufalme kwa pahali pake.
29-30Habari za mufalme Daudi toka mwanzo mpaka mwisho juu ya mambo ya utawala wake, uwezo wake, na mambo yaliyomupata yeye, Waisraeli, na falme zote katika inchi zimeandikwa katika vitabu vya nabii Samweli, katika vitabu vya nabii Natani, vilevile katika vitabu vya nabii Gadi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.