2 Wafalme 8 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mwanamuke wa Sunemu anarudi

1Elisha alikuwa amemwambia mwanamuke aliyeishi Sunemu ambaye alikuwa amemufufua mwana wake: “Ondoka na jamaa yako, uhamie katika inchi ya kigeni kwa sababu Yawe ameleta njaa itakayokuwa katika inchi kwa muda wa miaka saba.”

2Yule mwanamuke akaondoka, akafanya kama vile mutu wa Mungu alivyosema. Akaenda pamoja na jamaa yake na kukaa kama mugeni katika inchi ya Wafilistini kwa miaka saba.

3Miaka saba ilipokwisha, alitoka katika inchi ya Wafilistini akarudi Israeli na kwenda kwa mufalme kuomba arudishiwe nyumba yake na shamba lake.

4Akamukuta mufalme akiongea na Gehazi, akisema: “Tafazali, uniambie miujiza ambayo inatendwa na Elisha.”

5Gehazi alipokuwa anamwambia mufalme jinsi Elisha alivyofufua mutu aliyekufa, mwanamuke yule alitoa ombi lake kwa mufalme. Gehazi akasema: “Ee mufalme; huyu ndiye mwanamuke ambaye Elisha alimufufua mwana wake!”

6Mufalme alipomwuliza mwanamuke yule, yeye alimwelezea. Mufalme akamwita mukubwa wa waaskari wake na kumwamuru amurudishie mwanamuke yule mali yake yote, pamoja na mapato yote ya mashamba yake katika muda ule wote wa miaka saba.

Elisha na mulfame Beni-Hadadi wa Aramu

7Kisha Elisha alikwenda Damasiki. Wakati ule mufalme Beni-Hadadi alikuwa mugonjwa na alipoambiwa kwamba Elisha alikuwa Damasiki,

8alimwambia Hazaeli mukubwa wa waaskari wake: “Mumupelekee yule mutu wa Mungu zawadi umwambie aombe shauri kwa Yawe kama nitapona au hapana.”

9Hazaeli akapakia zawadi za kila aina ya mazao ya Damasiki kipimo cha mizigo ya ngamia makumi ine na kumupelekea Elisha. Alipofika kwa Elisha alimwambia: “Mutumishi wako, Beni-Hadadi, mufalme wa Aramu amenituma kwako. Yeye anauliza: ‘Nitapona ugonjwa huu?’ ”

10Basi Elisha akamujibu: “Umwambie kwamba atapona. Lakini Yawe amenionyesha kwamba atakufa.”

11Halafu Elisha akamukazia macho hata Hazaeli akashikwa na wasiwasi. Kwa rafla, Elisha mutu wa Mungu akaanza kulia.

12Hazaeli akamwuliza: “Bwana wangu, mbona unalia?”

Elisha akamujibu: “Kwa sababu ninajua maovu ambayo utawatendea watu wa Israeli. Utateketeza kuta zao kwa moto, na kuwaua vijana wao, utawapondaponda watoto wao na kupasua wanawake wenye mimba tumbo.”

13Hazaeli akauliza: “Lakini mimi mutumishi wako ni kitu kweli? Mimi ninayekuwa sawa na imbwa nitaweza namna gani kutenda mambo hayo makubwa?”

Elisha akamujibu: “Yawe amenionyesha kwamba utakuwa mufalme wa Aramu.”

14Halafu Hazaeli alitoka kwa Elisha, akarudi kwa bwana wake. Mufalme Beni-Hadadi akamwuliza: “Elisha alikuambia nini?”

Hazaeli akamujibu: “Aliniambia kwamba hakika utapona.”

15Lakini kesho yake Hazaeli akatwaa blanketi, akalilowesha ndani ya maji, kisha akamufunika nalo uso mpaka akakufa. Hazaeli akatawala inchi ya Aramu kwa pahali pake.

Mufalme Yehoramu wa Yuda(2 Sik 21.1-20)

16Katika mwaka wa tano wa utawala wa Yoramu mwana wa Ahabu, mufalme wa Israeli, Yehoramu mwana wa Yosafati, mufalme wa Yuda, alianza kutawala.

17Alipoanza kutawala alikuwa na umri wa miaka makumi tatu na miwili. Alitawala kule Yerusalema miaka minane.

18Alifuata mwenendo wa wafalme wa Israeli, kama vile jamaa ya Ahabu ilivyofanya, kwa sababu muke wake alikuwa binti ya Ahabu. Akatenda maovu mbele ya Yawe.

19Lakini Yawe hakutaka kuangamiza Yuda, kwa sababu ya Daudi mutumishi wake, maana aliahidi kwamba wazao wake wataendelea kutawala milele.

20Wakati wa utawala wa Yehoramu, watu wa Edomu waliasi utawala wa Yuda, wakatawalisha mufalme wao.

21Kwa hiyo Yoramu aliondoka na magari yake yote kwenda Sairi. Wakati wa usiku alitoka na waongozi wake wa magari akawashambulia Waedomu waliokuwa wamemuzunguka. Lakini waaskari wake walikimbilia kwao.

22Hivyo watu wa Edomu wakauasi utawala wa Yuda mpaka sasa. Wakati uleule, wakaaji wa Libuna nao wakaasi.

23Mambo mengine ya Yehoramu na yote aliyofanya yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.

24Yehoramu akakufa na kuzikwa katika makaburi ya kifalme katika muji wa Daudi, naye Ahazia mwana wa Yehoramu, akatawala kwa pahali pake.

Mufalme Ahazia wa Yuda(2 Sik 22.1-6)

25Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Yoramu mwana wa Ahabu mufalme wa Israeli, Ahazia mwana wa Yehoramu mufalme wa Yuda alianza kutawala.

26Ahazia alianza kutawala akiwa na umri wa miaka makumi mbili na mbili, akatawala akiwa Yerusalema kwa muda wa mwaka mumoja. Mama yake aliitwa Atalia, mujukuu wa mufalme Omuri mufalme wa Israeli.

27Kwa sababu Ahazia alikuwa mukwe wa jamaa ya Ahabu, naye alifuata mwenendo wa jamaa hiyo ya Ahabu, alitenda maovu mbele ya Yawe, kama vile jamaa ya Ahabu walivyofanya.

28Mufalme Ahazia akaenda na Yoramu mwana wa Ahabu kupigana vita na Hazaeli mufalme wa Aramu kule Ramoti-Gileadi pahali Waaramu walipomwumizia Yoramu.

29Kisha mufalme Yoramu akarudi katika muji Yezereheli kusudi apate kutunzwa vidonda alivyoumizwa na Waaramu kule Rama, alipopigana na Hazaeli mufalme wa Aramu. Naye Ahazia mwana wa Yehoramu, mufalme wa Yuda alimwendea Yoramu mwana wa Ahabu kule Yezereheli, kwa sababu alikuwa mugonjwa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help