Waebrania 5 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Kila Kuhani Mukubwa aliyechaguliwa kati ya watu amesimikwa kwa kumutumikia Mungu kwa ajili ya watu kusudi atolee matoleo na sadaka kwa ajili ya zambi.

2Kwa kuwa yeye mwenyewe ni muzaifu, anaweza kuwavumilia wale waliopotoka bila kujua.

3Na kwa sababu yeye mwenyewe ni muzaifu, anapaswa kutolea sadaka, si kwa sababu ya zambi za watu tu, lakini kwa sababu ya zambi zake mwenyewe vilevile.

4Hakuna mutu anayejipatia heshima hii ya kuwa Kuhani Mukubwa yeye mwenyewe. Lakini anapaswa kuitwa na Mungu, kama vile Haruni alivyoitwa.

5Hivi vilevile, Kristo hakujipatia yeye mwenyewe utukufu wa kuwa Kuhani Mukubwa, lakini ni Mungu ndiye aliyemwambia:

“Wewe ni mwana wangu,

mimi leo nimekuwa baba yako.”

6Vilevile alisema pahali pengine katika Maandiko:

“Wewe ni kuhani hata milele

kwa mufano wa Melkisedeki.”

7Wakati Yesu alipoishi katika dunia, aliomba na kusihi kwa malalamiko makubwa pamoja na kutoa machozi kwa Mungu ambaye angeweza kumwokoa toka katika kifo. Mungu alimusikia Yesu kwa sababu yeye alimuheshimu.

8Ijapokuwa alikuwa Mwana wa Mungu, alijifunza kutii kwa njia ya mateso yale aliyopata.

9Na alipokwisha kufanywa kuwa mukamilifu, akawaongoza watu wote wanaomutii wapate kuokolewa kwa milele.

10Basi, Mungu alitangaza kwamba yeye ni Kuhani Mukubwa kwa mufano wa Melkisedeki.

Hatari ya kuacha imani

11Tuna maneno mengi ya kusema juu ya jambo hili, lakini ni vigumu kuyaeleza kwenu kwa sababu ninyi mumekuwa na masikio magumu.

12Kweli, kwa wakati huu, ninyi mungepaswa sasa kuwa walimu, lakini mungali munahitaji kufundishwa tena mafundisho ya mwanzo ya neno la Mungu. Mumegeuka tena wenye kuhitaji kunywa maziwa, wala si chakula kigumu.

13Kwa maana kila mutu anayeishi kwa kunyonya maziwa tu hawezi kufahamu mafundisho ya haki, maana yeye ni mutoto muchanga.

14Lakini chakula kigumu ni kwa ajili ya watu wazima, ndio wale waliozoeza mafikiri yao hata wapate kutambua mema na mabaya.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help