1Katika mwezi wa saba, Isimaeli mwana wa Netania, mujukuu wa Elisama, wa ukoo wa kifalme, mumoja wa wasimamizi wa mufalme alifika Misipa kwa Gedalia pamoja na watu kumi. Wakati walipokuwa wakikula chakula kule Misipa,
2Isimaeli mwana wa Netania pamoja na wale watu kumi, wakasimama na kumushambulia kwa upanga Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu, wakamwua. Gedalia ndiye aliyekuwa amesimikwa na mufalme wa Babeli kuwa mutawala wa inchi.
3Isimaeli aliwaua vilevile Wayuda wote waliokuwa pamoja na Gedalia huko Misipa na waaskari Wakaldea waliokuwa pahali pale.
4Siku moja kisha kumwua Gedalia,
5mbele hata mutu yeyote hajajua habari hizo, kulifika watu makumi nane kutoka Sekemu, Shilo na Samaria. Walikuwa wamenyoa ndevu zao na wamevaa nguo zilizotatuka na miili yao imechanjwachanjwa. Walileta sadaka ya ngano na ubani vitolewe katika nyumba ya Yawe.
6Isimaeli mwana wa Netania, alitoka inje ya muji kukutana na watu hao akiwa analia. Alipokutana nao, akawaambia: Karibu ndani ya nyumba kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.
7Walipoingia katika muji, Isimaeli mwana wa Netania, pamoja na wale watu kumi waliokuwa pamoja naye, waliwaua watu hao na kuzitupa maiti zao ndani ya kisima.
8Lakini kulikuwa watu kumi katika kundi hilo waliomwambia Isimaeli hivi: Tafazali usituue, maana tuna akiba kubwa ya ngano, shayiri, mafuta na asali ambayo tumeificha katika pori. Basi hao akawaacha wazima.
9Kisima ambamo Isimaeli alitupa maiti za wale watu aliowaua ni kile kikubwa ambacho mufalme Asa alikuwa amekichimba kwa kujikinga na Basha, mufalme wa Waisraeli. Isimaeli mwana wa Netania alikijaza kisima hicho maiti za wale watu aliowaua.
10Kisha, Isimaeli aliwakamata wabinti wa mufalme mateka na watu wote waliobaki kule Misipa, watu ambao Nebuzaradani, mukubwa wa walinzi, alikuwa amewaweka chini ya ulinzi wa Gedalia mwana wa Ahikamu. Isimaeli mwana wa Netania, aliwakamata mateka hao, akaondoka, akaenda kwa Waamoni.
11Lakini Yohana mwana wa Karea, pamoja na wakubwa wote wa waaskari, waliposikia juu ya uovu ambao Isimaeli mwana wa Netania, alikuwa ameufanya,
12waliwakusanya watu wao wote, wakaenda kupigana na Isimaeli. Walimukuta kwenye kisima kikubwa cha Gibeoni.
13Watu wote waliotekwa na Isimaeli walipomwona Yohana mwana wa Karea, pamoja na wakubwa wote wa waaskari, walifurahi sana.
14Basi, watu hao wote ambao Isimaeli alikuwa amewakamata mateka kutoka Misipa, waligeuka, wakarudi nyuma, wakamwendea Yohana mwana wa Karea.
15Lakini Isimaeli mwana wa Netania, pamoja na watu wanane waliponyoka kutoka kwa Yohana, wakakimbilia kwa Waamoni.
16Kisha, Yohana mwana wa Karea pamoja na wakubwa wote wa waaskari waliokuwa pamoja naye, waliwakamata watu wote waliobaki, ambao Isimaeli mwana wa Netania, alikuwa amewakamata mateka kutoka Misipa kisha kumwua Gedalia mwana wa Ahikamu, ni kusema: waaskari, wanawake, watoto na matowashi wa nyumba ya mufalme. Yohana aliwarudisha wote kutoka Gibeoni.
17Basi, wakajiendea, wakakaa huko Geruti–Kimuhamu karibu na Betelehemu. Wakikusudia kuingia katika inchi ya Misri, kwa sababu
18walikuwa wanawaogopa Wakaldea tangu wakati Isimaeli mwana wa Netania, alipomwua Gedalia mwana wa Ahikamu ambaye mufalme wa Babeli alikuwa amemusimika kuwa mutawala wa inchi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.