1Kwa kuwa mumefufuliwa pamoja na Kristo, mutafute mambo yanayokuwa juu, pahali Kristo anapoikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu.
2Mushugulikie sana mambo yanayokuwa juu, lakini musishugulikie mambo yanayokuwa katika dunia.
3Kwa maana ninyi mumekufa na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
4Kristo ndiye uzima wenu wa kweli, naye atakapoonekana tena, basi ninyi mutaonekana pamoja naye katika utukufu wake.
Maisha ya zamani na maisha ya sasa5Basi mutupilie mbali mambo yote ya kidunia yanayokuwa ndani yenu: uasherati, uchafu, nia mbaya, tamaa mbaya na tamaa ya mali inayokuwa sawa vile kuabudu sanamu.
6Kwa sababu ya makosa haya, kasirani ya Mungu itawaangukia wale wanaomwasi.
7Zamani, ninyi muliishi kwa namna ile mulipokuwa mukitawaliwa na mambo hayo ya zambi.
8Lakini sasa mutupilie mbali mambo haya yote: kasirani, chuki, uovu, masingiziano na musiseme neno lolote baya.
9Musiambiane uongo ninyi kwa ninyi, kwa maana mumeondoa utu wenu wa zamani pamoja na matendo yake
10na kuvaa utu mupya. Utu ule unaendelea kufanywa upya kila mara kufuatana na mufano wa Mungu anayekuwa muumba wake, kusudi mupate kumujua hakika.
11Kwa hiyo hakuna tena tofauti kati ya watu wa mataifa mengine na Wayuda, wenye kutahiriwa na wasiotahiriwa, wageni, washenzi, watumwa na watu huru. Lakini Kristo ni yote naye yuko katika wote.
12Ninyi ni watu wa Mungu, yeye amewapenda na kuwachagua kwa ajili yake mwenyewe. Kwa hiyo, mukuwe na moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
13Muvumiliane na kusameheana ninyi kwa ninyi wakati wowote mutu anapokuwa na neno la kumushitaki mwingine. Munapaswa kusameheana kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi.
14Zaidi ya mambo haya yote, mukuwe na upendo, maana upendo unaunganisha kila kitu katika umoja unaokuwa mukamilifu.
15Amani ya Kristo itawale katika mioyo yenu; maana ni kwa ajili ya hiyo ninyi mumeitwa kuwa katika mwili mumoja. Mukuwe wenye shukrani.
16Habari za Kristo zikae ndani yenu kwa uwingi. Mufundishane na mushauriane kwa hekima. Mumwimbie Mungu kwa moyo wenu wote na kumushukuru kwa zaburi na nyimbo za kiroho.
17Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.
Maonyo katika maisha mapya18Wake muwatii waume wenu kama vile inavyostahili mbele ya Bwana.
19Waume muwapende wake wenu nanyi musiwatendee kwa ukali.
20Watoto muwatii wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana jambo hili linamupendeza Bwana.
21Ninyi wababa musiwakasirikishe watoto wenu, kusudi musiwavunje moyo.
22Ninyi watumwa, muwatii wabwana wenu katika mambo yote hapa katika dunia. Musiwatii tu wakati wanapowaangalia ninyi kama mungetaka tu kujipendeza mbele yao, lakini muwatii kwa moyo mwema, kwa sababu munamuheshimu Bwana.
23Na kila kitu munachofanya, mukifanye kwa moyo wenu wote, kama vile wenye kumutumikia Bwana wala si watu.
24Mukumbuke kwamba Bwana atawapa ninyi zawadi ile anayowawekea watu wake. Kwa maana Kristo ndiye Bwana wa kweli munayemutumikia.
25Lakini yule anayefanya mabaya, atalipwa kufuatana na mabaya aliyotenda, kwa sababu Mungu hana upendeleo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.