Yeremia 3 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Ukahaba wa Israeli

1Mume akiachana na muke wake,

naye muke akijiendea,

na kuolewa na mwingine,

mume yule anaweza kumurudilia muke huyo?

Kufanya hivyo hakutaichafua inchi kabisa?

Wewe Israeli, umefanya ukahaba na wapenzi wengi,

sasa unataka kunirudilia mimi?

–Ni ujumbe wa Yawe.–

2Inua macho, uangalie vilele vya vilima!

Kuna nafasi ambapo hawajalala nawe?

Uliwangoja wapenzi wako kando ya njia,

kama mubedui anavyovizia watu katika jangwa.

Umeichafua inchi

kwa ukahaba wako mubaya sana.

3Ndiyo maana manyunyu yamezuizwa kuanguka,

wala mvua za mwisho hazijanyesha.

Hata hivyo unakausha macho kama kahaba,

wala hauna haya hata kidogo.

4Na sasa hivi tu unanililia, ukisema:

Wewe ni baba yangu,

ulinipenda tangu utoto wangu?

5Utanikasirikia siku zote?

Utachukizwa nami milele?

Israeli, vile ndivyo unavyosema;

na kumbe umetenda uovu wote ulioweza.

6Katika siku ya utawala wa mufalme Yosia, Yawe aliniambia hivi: Umeona jinsi yule Israeli asiyekuwa mwaminifu alivyofanya? Aliniacha, akapanda juu ya kila kilima kirefu na kwenda chini ya kila muti wenye majani mabichi, akafanya ukahaba wake kule!

Sherti watu wa Israeli na Yuda wakubali makosa yao

7Mimi nilizani kwamba nyuma ya kufanya hayo yote, atanirudilia. Lakini hakunirudilia. Yuda, dada yake mudanganyifu, alishuhudia hayo yote.

8Zaidi ya hayo, Yuda alishuhudia kwamba niliachana na Israeli kwa sababu ya ukahaba wake na kwa kukosa uaminifu kwangu. Lakini hata hivyo, Yuda, dada yake mudanganyifu, hakuogopa; naye vilevile alikwenda na kufanya ukahaba!

9Aliona kwamba ukahaba ni jambo dogo sana kwake. Aliichafua inchi kwa kufanya ukahaba, akiabudu mawe na miti.

10Pamoja na hayo yote, Yuda, dada mudanganyifu wa Israeli hakunirudilia kwa moyo wote, lakini kwa unafiki tu.

–Ni ujumbe wa Yawe.

11Yawe akaendelea kuniambia hivi: Muasi Israeli amejionyesha kuwa wa haki kuliko Yuda mudanganyifu.

12Basi, kwenda umutangazie Israeli maneno haya:

Rudi, ewe Israeli usiyekuwa mwaminifu.

–Ni ujumbe wa Yawe.–

Nami sitakuangalia kwa hasira

maana mimi ni mwema.

–Ni ujumbe wa Yawe.–

Kweli, sitakukasirikia milele.

13Wewe, kubali tu kosa lako:

kwamba umeniasi mimi Yawe, Mungu wako;

kwamba chini ya kila muti wenye majani,

umeonyesha mapenzi yako kwa miungu mingine,

wala haukuitii sauti yangu.

–Ni ujumbe wa Yawe.

14Murudi, enyi watoto musiokuwa na uaminifu,

maana, mimi ndimi Bwana wenu.

Nitawatwaa mumoja kutoka kila muji,

na wawili kutoka katika kila ukoo,

niwapeleke mpaka kwenye mulima Sayuni.

–Ni ujumbe wa Yawe.

15Nitawapa wachungaji wanaopendeza moyo wangu, watakaowakulisha kwa akili.

16Siku hizo, wakati mutakapokuwa mumeongezeka na kuwa wengi katika inchi, watu hawatalitajataja tena Sanduku langu la Agano.

–Ni ujumbe wa Yawe.–

Hawatalifikiri juu yake kabisa, wala hawatalikumbuka tena; hawatalihitaji, wala hawatatengeneza lingine.

17Wakati huo, Yerusalema utaitwa “Kiti cha Kifalme cha Yawe”, na mataifa yote yatakusanyika humo mbele yangu. Hawatafuata tena ugumu wao unaotokana na matendo yao mabaya.

18Siku hizo, watu wa Yuda wataungana na watu wa Israeli, na wote kwa pamoja watatoka katika inchi ya kaskazini na kurudi katika inchi niliyowapa babu zenu ikuwe urizi wao.

Watu wa Mungu walidanganyika kwa kutambikia sanamu

19Yawe anasema:

Wewe Israeli, mimi niliwaza hivi:

heri ningekuhesabia kati ya wana wangu,

na kukupa inchi nzuri ajabu,

ndio urizi unaopita inchi zote za mataifa.

Nilizani utaniita Baba Yako,

na kwamba haungeacha kunifuata.

20Lakini kama muke asiyekuwa mwaminifu anavyomwacha mume wake,

ndivyo ulivyokosa uaminifu kwangu.

–Ni ujumbe wa Yawe.

21Kelele linasikilika juu ya vilima:

Waisraeli wanalia na kuomboleza,

kwa sababu wamepotoka katika njia zao,

wamenisahau mimi Yawe, Mungu wao.

22Murudi, enyi watoto musiokuwa na uaminifu,

mimi nitawaponyesha ukosefu wenu wa uaminifu.

Nanyi munasema: Sisi tunarudi kwako,

maana wewe ndiwe Yawe, Mungu wetu.

23Kweli tumedanganyika sana kwa kutambikia huko kwenye vilima,

hakika wokovu wa Israeli

unatoka kwake Yawe, Mungu wetu.

24Tangu ujana wetu, tendo hili la haya limeangamiza kila kitu babu zetu walichokitoshea jasho: makundi yao ya kondoo na ngombe, wana wao na wabinti zao.

25Sherti tujilaze chini kwa ajili ya haya, na kujiachilia kufunikiwa na haya yetu. Tangu ujana wetu mpaka leo hii, sisi wenyewe, kama vile babu zetu, tumetenda zambi mbele ya Yawe, Mungu wetu, wala hatukumutii Yawe, Mungu wetu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help