Ezekieli 9 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kuazibiwa kwa Yerusalema

1Kisha nikamusikia Yawe akisema kwa sauti kubwa: Mujongee karibu ninyi mutakaouazibu muji huu. Mukuje na silaha zenu za kuangamiza.

2Watu sita wakakuja kutoka upande wa mulango wa juu unaoelekea upande wa kaskazini, kila mumoja na silaha yake ya kuangamiza katika mukono wake. Pamoja nao, kulikuwa mutu mumoja ambaye alikuwa amevaa nguo ya kitani, naye ana chupa la wino. Wakaingia ndani ya hekalu, wakasimama pembeni ya mazabahu ya shaba.

3Kisha utukufu wa Mungu wa Israeli uliondoka pale juu ya makerubi na kupanda juu mpaka kwenye kizingiti cha nyumba ya Yawe. Yawe akamwita mutu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani, mwenye chupa la wino,

4akamwambia hivi: Pita katikati ya Yerusalema, upate kutia kitambulisho kwenye vipaji vya nyuso za watu wanaohuzunika na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika muji huu. Ang. Ufu 7.3; 14.1

5Kisha akawaambia wale wengine mimi nikiwa ninasikia: Mupite katika muji, muue watu; musimwachilie mutu yeyote wala kuwa na huruma.

6Muwaue wazee palepale, vijana wanaume na wabinti, watoto na wanawake; lakini kila mumoja mwenye kuwa na kitambulisho, musimuguse. Muanzie katika hekalu langu. Basi, wakaanza na wazee waliokuwa mbele ya nyumba ya Yawe.

7Akawaambia: Muchafue nyumba ya Yawe kwa kuvijaza viwanja vyake maiti, kisha musonge mbele. Basi, wakaenda, wakawaua watu katika muji.

8Wakati walipokuwa wakiwaua, mimi niliachwa peke yangu, nikaanguka uso mpaka chini, nikalia: Ee Bwana wangu Yawe, utaangamiza watu wote wa Israeli waliobaki, ukitimiza kasirani yako juu ya Yerusalema?

9Naye akaniambia: Uovu wa Waisraeli na watu wa Yuda ni mukubwa sana. Inchi imejaa umwagaji wa damu na katika muji hakuna haki, kwa maana wanasema: Yawe ameiachilia inchi; Yawe haoni.

10Kwa upande wangu, sitawaachilia wala kuwahurumia; nitawatendea kufuatana na matendo yao.

11Kisha mutu yule aliyevaa nguo ya kitani, mwenye chupa la wino, akarudi na kutoa habari hii: Nimefanya kama ulivyoniamuru.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help