1Mizani danganyifu ni chukizo kwa Yawe, lakini matumizi ya vipimo vya haki ni furaha kwake.
2Kiburi kinazaa haya, lakini kwa watu wanyenyekevu kuna hekima.
3Ukamilifu wa watu wa usawa unawaongoza. Upotovu wa wadanganyifu unawaangamiza.
4Utajiri haufai kitu siku ya kasirani, lakini haki inaokoa kutoka kifo.
5Haki ya watu wakamilifu inanyoosha njia yao, lakini waovu wanaanguka kwa uovu wao wenyewe.
6Haki ya watu wa usawa inawaokoa na hatari, lakini wafitini wananaswa kwa tamaa zao wenyewe.
7Mwovu akikufa, tumaini lake nalo linatoweka. Tumaini la asiyemwogopa Mungu ni la bure.
8Mutu wa haki anaokolewa katika shida, na mwovu anaingia mule kwa pahali pake.
9Asiyemwogopa Mungu anaangamiza wengine kwa kinywa chake, lakini mwenye haki anaokolewa kwa maarifa yake.
10Watu wa haki wakipata fanaka, muji unashangilia. Waovu wakiangamia, watu wanapiga vigelegele.
11Muji unafanikishwa kwa baraka za watu wa usawa, lakini unaangamizwa kwa kinywa cha waovu.
12Anayemuzarau jirani yake hana akili; mutu mwenye ufahamu anakaa kimya.
13Anayepitapita akichongea anatoa siri, lakini anayeaminiwa anaficha siri.
14Pasipo uongozi taifa linaanguka; kwenye kuwa washauri wengi kuna usalama.
15Anayejitoa kulipia mugeni deni yake atajuta, lakini anayechukia mapatano yale ana usalama.
16Mwanamuke mwema anaheshimiwa; wanaume wenye nguvu wanatajirika.
17Mutu mwema anafaidika yeye mwenyewe, lakini mutu mukali anajiumiza mwenyewe.
18Faida mwovu anayopata ni ya uongo, lakini anayetenda mema, hakika atapata faida.
19Mutu anayekusudia kuwa mwenye haki ataishi, lakini anayechagua kutenda maovu atakufa.
20Wenye nia mbaya ni chukizo kwa Yawe, lakini wenye mwenendo mukamilifu ni furaha yake.
21Hakika mwovu hataepuka kuazibiwa, lakini wenye haki wataokolewa.
22Mwanamuke muzuri asiyekuwa na akili ni kama pete ya zahabu kwenye pua la nguruwe.
23Matazamio ya wenye haki yana matokeo mazuri; tamaa za waovu zinaleta kasirani.
24Kuna watu wanaotoa mali yao kwa wingi na kuzidi; lakini wachoyo wanazilinda na kuendelea katika umasikini.
25Mutu anayetoa kwa moyo safi atafanikishwa. Mutu anayekunywesha mwingine maji, naye atakunyweshwa.
26Watu wanamulaani mutu anayeficha ngano, lakini wanamutakia baraka mwenye kuiuzisha.
27Anayetafuta kutenda mazuri anapata upendeleo, lakini anayetafuta kutenda maovu atapatwa na maovu.
28Anayetegemea mali zake ataanguka, lakini mwenye haki atastawi kama jani bichi.
29Anayevunja nyumba yake, atavuna upepo. Mupumbafu atakuwa mutumwa wa wenye hekima.
30Tunda la mwenye haki ni muti wa uzima, na mwenye hekima anavuta watu.
31Ikiwa mwenye haki anapata malipo hapa katika dunia, hakika mwovu na mwenye zambi watalipwa!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.