1Nyuma ya mambo hayo, majeshi ya Wamoabu na Waamoni pamoja na sehemu ya Wameuni wakashambulia inchi ya Yuda.
2Watu wamoja wakakuja kumwambia mufalme Yosafati: “Jeshi kubwa limekuja kukushambulia kutoka Edomu, ngambo ya bahari ya Chumvi. Tayari wamekwisha kufika Hazazoni-Tamari.” (Hili ni jina lingine la Engedi).
3Yosafati akashikwa na woga, akamwomba Yawe amwongoze. Akatangaza kwamba watu wote katika inchi ya Yuda wafunge kula.
4Watu wakakuja Yerusalema kutoka miji yote ya Yuda, wakakusanyika kwa kumwomba Yawe awasaidie.
5Yosafati akasimama katikati ya kusanyiko la watu wa Yuda na Yerusalema mbele ya kiwanja kipya cha nyumba ya Yawe,
6akaomba kwa sauti akisema: “Ee Yawe, Mungu wa babu zetu, wewe ndiwe Mungu unayekuwa mbinguni! Wewe unatawala falme zote katika dunia, una uwezo na nguvu, wala hakuna anayeweza kukupinga.
7Si wewe, ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa inchi hii wakati watu wako Waisraeli walipoingia katika inchi hii, ukawapa wazao wa Abrahamu rafiki yako, ikuwe yao milele?
18Kisha mufalme Yosafati akainama uso mpaka chini pamoja na watu wote wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema na kumwabudu Yawe.
19Walawi na ukoo wa Kohati na Kora, wakasimama na kumusifu Yawe, Mungu wa Israeli, kwa sauti kubwa sana.
20Kesho yake, wakaamuka asubui mapema, wakaenda mpaka katika jangwa la Tekoa. Walipokuwa wanaondoka, Yosafati akasimama, akawaambia: “Musikilize, enyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema! Mumwamini Yawe, Mungu wenu, nanyi mutakuwa imara. Muwaaminie manabii wake, nanyi mutashinda.”
21Nyuma ya kushauriana na watu, mufalme akachagua waimbaji kwa kumwimbia Yawe wavae nguo zao takatifu kisha watangulie mbele ya jeshi, wakiimba:
“Mumushukuru Yawe,
maana wema wake unadumu milele!”
22Wakati walipoanza kuimba na kusifu, Yawe akawavuruga akili waaskari Waamoni, Wamoabu na watu wa mulima Seiri waliokuja kupigana na Yuda. Na waaskari wale wakashindwa.
23Waamoni na Wamoabu wakawashambulia wenyeji wa mulima Seiri, na kuwaangamiza kabisa. Kisha kuwaangamiza wakaaji wa mulima Seiri wakaanza kushambuliana wao kwa wao, wakaangamizana.
24Jeshi la Yuda lilipofika kwenye munara wa ulinzi kule katika jangwa, wakaangalia upande wa waadui, wakaona maiti zimesambaa kila pahali. Hakuna mutu yeyote aliyeponyoka.
25Yosafati na waaskari wake wakaenda kukamata vitu. Wakakuta ngombe wengi, mali, nguo na vitu vingine vya bei kali. Iliwachukua muda wa siku tatu kusomba vitu hivyo, na hata hivyo, hawakuvimaliza maana vilikuwa vingi sana.
26Siku ya ine wakakusanyika katika Bonde la Sifa, na kumusifu Yawe kwa yote aliyowafanyia. Hii ndiyo sababu bonde hilo linaitwa Bonde la Sifa mpaka hivi leo.
27Kisha Yosafati akawaongoza waaskari wake mpaka Yerusalema kwa shangwe, kwa sababu Yawe aliwashinda waadui zao.
28Walipofika Yerusalema, walikwenda moja kwa moja mpaka kwenye nyumba ya Yawe, wakipiga vinanda, vinubi na baragumu.
29Falme zote zikaingiwa na hofu ziliposikia jinsi Yawe alivyowashinda waadui za Israeli.
30Basi, Yosafati akatawala kwa amani, na Mungu akamupa amani pande zote.
Mwisho wa utawala wa Yosafati(1 Fal 22.41-50)31Yosafati alikuwa na umri wa miaka makumi tatu na mitano alipoanza kutawala inchi ya Yuda. Alitawala kutoka Yerusalema kwa muda wa miaka makumi mbili na tano. Jina la mama yake ni Azuba binti ya Silihi.
32Yosafati alitenda mema mbele ya Yawe kama vile Asa baba yake alivyofanya.
33Lakini hakuharibu pahali pa kutambikia sadaka juu ya kilima. Watu walikuwa wangali hawajamugeukia na kumwabudu Mungu wa babu zao kwa mioyo yao.
34Matendo mengine ya Yosafati, kutoka mwanzo wa utawala wake mpaka mwisho, yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Yehu mwana wa Hanani, ambacho kiko katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli.
35Nyuma ya hayo, Yosafati mufalme wa Yuda, akajiunga na Ahazia mufalme wa Israeli, aliyetenda mambo maovu.
36Walishirikiana kutengeneza mashua za kusafiri mpaka Tarsisi, walizitengenezea kule Esioni-Geberi.
37Lakini Eliezeri mwana wa Dodawa, kutoka muji wa Maresa, akatoa unabii juu ya Yosafati, akisema: “Kwa sababu umejiunga na Ahazia, Yawe atavunja mashua zote mulizotengeneza.” Na mashua zile zilivunjikavunjika; kwa hiyo hazikuweza kusafiri mpaka Tarsisi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.