Muhubiri 11 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Jambo mwenye akili analopaswa kufanya

1Tupa chakula chako juu ya maji.

Nyuma ya siku nyingi utakipata tena!

2Gawa sehemu moja kwa watu saba hata wanane,

maana, haujui hasara itakayofika katika dunia.

3Mawingu yakijaa maji, mvua inanyesha.

Muti ukiangukia upande wa kusini au wa kaskazini,

pale unapoangukia ndipo unapolala.

4Anayechunguza upepo hatapanda mbegu,

anayeangalia mawingu yatoweke, hatavuna kitu.

5Kama vile hauwezi kujua jinsi uzima unavyoingia katika mifupa ya mutoto katika tumbo la mama yake, vilevile hauwezi kuelewa matendo ya Mungu, aliyefanya kila kitu.

6Panda mbegu asubui na usiache kupanda mpaka magaribi, maana, haujui mbegu gani zitaota; za asubui, za magaribi, au zote zitakuwa nzuri.

7Mwangaza ni muzuri, na kuona jua kunapendeza macho.

8Mutu akiishi miaka mingi, afurahie miaka hiyo yote; lakini akumbuke kwamba siku mbaya zitakuwa nyingi, na kwamba yote yatakayofuata ni bure.

Maonyo kwa vijana

9Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako ukuwe na raha wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na tamaa ya macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.

10Ondoa mahangaiko ndani ya moyo wako, ujikinge usipate maumivu katika mwili kwa sababu ujana na nguvu vinapita mbio.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help