1Kisha nikasikia sauti kubwa ikitoka katika hekalu ikiwaambia wale wamalaika saba: “Mwende kumwanga vile vikombe saba vya kasirani ya Mungu juu ya dunia!”
2Malaika wa kwanza akamwanga kikombe chake katika dunia. Halafu majipu mabaya na yenye kuumiza sana yakaota juu ya watu waliokuwa na chapa ya yule nyama na walioabudu sanamu yake.
3Malaika wa pili akamwanga kikombe chake katika bahari. Maji yakageuka na kuwa kama damu ya mufu, na viumbe vyote vyenye uzima vilivyokuwa ndani ya bahari vikakufa.
4Malaika wa tatu akamwanga kikombe chake katika mito na chemichemi za maji, na maji yao yakageuka damu.
5Nikasikia malaika anayekuwa na uwezo wa kuamuru maji akisema: “Ewe Mutakatifu unayekuwa na uliyekuwa, wewe unahukumu kufuatana na haki.
6Watu hawa walimwanga damu ya watu wako na ya manabii wako, kwa sababu hiyo sasa umewakunywesha damu, nao wanastahili kutendewa vile!”
7Kisha nikasikia sauti ikitoka kwenye mazabahu, ikisema: “Hakika, ewe Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, wewe unatoa hukumu za kweli na za haki!”
8Malaika wa ine akamwanga kikombe chake juu ya jua, nalo likapewa uwezo wa kuwaunguza watu kwa joto lake.
9Watu wakaunguzwa na lile joto kali, hata wakatukana jina la Mungu anayekuwa na uwezo wa kuamuru mapigo yale. Wakakataa kugeuka toka zambi zao na kumutukuza Mungu.
10Malaika wa tano akamwanga kikombe chake juu ya kiti cha kifalme cha yule nyama wa ajabu, na ufalme wake ukafunikwa na giza. Watu wakaanza kutafuna ndimi zao kwa sababu ya maumivu.
11Wakamutukana Mungu wa mbinguni kwa sababu ya maumivu yao na yale majipu yao, lakini hawakuacha matendo yao mabaya.
12Malaika wa sita akamwanga kikombe chake katika muto mukubwa Furati. Maji yake yakakauka kusudi njia itengenezwe kwa ajili ya wafalme wanaotoka mashariki.
13Halafu nikaona pepo wachafu watatu wanaofanana na vyura wakitoka ndani ya kinywa cha yule nyoka mukubwa, na ndani ya kinywa cha yule nyama wa ajabu na cha yule nabii wa uongo.
14Hawa ndio pepo wanaoonyesha vitambulisho. Nao ndio wanaokwenda kwa wafalme wote wa dunia na kuwakusanya kwa kupigana vita Siku ile kubwa ya Mungu Mwenye Uwezo.
15“Sikiliza, ninakuja kwa saa isiyozaniwa kama vile mwizi. Heri yule anayekesha na kutunza nguo zake vizuri kusudi asitembee uchi na kujifezehesha mbele ya watu.”
16Na wale pepo wakawakusanya wale wafalme kwenye nafasi inayoitwa katika Kiebrania “Harmagedoni.”
17Malaika wa saba akamwanga kikombe chake katika anga. Halafu sauti kubwa ikasikilika kutoka katika hekalu kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa ni mwisho!”
18Kukatokea umeme, makelele, ngurumo ya radi na tetemeko kubwa la inchi lisilotokea bado tangia watu walipoanza kuishi katika dunia. Kweli tetemeko lile lilikuwa kubwa sana!
19Na ule muji mukubwa ukagawanyika katika sehemu tatu, na miji ya mataifa yote ikabomoka. Mungu hakusahau muji mukubwa Babeli, akaukunywesha kikombe kinachokuwa na divai ya kasirani yake kali.
20Visanga vyote vikatoweka na milima haikuonekana tena.
21Kisha mvua ya mawe makubwa yenye uzito wa zaidi ya kilo makumi ine ikanyesha juu ya watu. Nao wakamutukana Mungu kwa sababu ya hilo pigo la mvua ya mawe, kwa maana pigo lile lilileta hasara kubwa sana.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.