Yeremia 31 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kurudi kwa Waisraeli kwao

1Kutakuja siku ambazo nitakuwa Mungu wa jamaa zote za Waisraeli, nao watakuwa watu wangu.

–Ni ujumbe wa Yawe.

2Yawe anasema hivi:

Watu walioponyoka kuuawa,

nilionyesha neema yangu kwao katika jangwa.

Wakati Israeli alipotafuta kwenda kupumzika,

3mimi Yawe nilimutokea kwa mbali.

Nami nimekupenda kwa mapendo ya milele,

kwa hiyo nimeendelea kuwa mwema kwako.

4Nitakurudisha katika hali mupya,

ewe binti Israeli!

Utazitwaa tena ngoma zako,

nawe utajitokeza tena kwa kucheza na wenye shangwe.

5Utapanda tena mizabibu

juu ya milima ya Samaria;

walimaji watapanda mbegu

na kuyafurahia mazao yake!

6Maana kutakuja siku ambapo walinzi watalalamika hivi

katika vilima vya Efuraimu:

Musimame, tupande kwenda Sayuni

kwa Yawe, Mungu wetu.

7Maana Yawe anasema hivi:

Mushangilie kwa furaha kwa ajili ya Yakobo,

mupige vigelegele kwa ajili ya taifa kubwa,

mutangaze, musifu na kusema:

Yawe ameokoa watu wake,

ameleta ukombozi kwa wale waliobaki kati ya Waisraeli!

8Nitawarudisha kutoka inchi ya kaskazini,

nitawakusanya kutoka miisho ya dunia.

Wote watakuwa pale;

hata vipofu na vilema,

wanawake wenye mimba na wanaosikia maumivu ya kuzaa;

kundi kubwa sana la watu litarudi hapa.

9Watarudi wakiwa wanatoa machozi,

nami nitawaongoza nikiwafariji;

nitawapitisha kando ya vijito vya maji,

katika njia iliyonyooka ambamo hawatajikwaa;

maana mimi nimekuwa baba wa Israeli,

Efuraimu ni muzaliwa wangu wa kwanza.

10Enyi mataifa, musikilize neno langu mimi Yawe,

mulitangaze katika visanga vya mbali,

museme hivi: Aliyemusambaza Israeli, atamukusanya,

atamutunza kama muchungaji anavyotunza kondoo wake.

11Maana mimi Yawe nimemukomboa Yakobo,

nimemwokoa kutoka kwa wenye nguvu kuliko yeye.

12Watakuja na kuimba kwa sauti juu ya mulima Sayuni,

watapata utukufu juu ya wema wangu mimi Yawe,

kwa ajili ya ngano, divai na mafuta ninavyowapa,

kwa ajili ya kondoo na ngombe vilevile;

maisha yao yatakuwa kama bustani iliyotiliwa maji,

wala hawataregea tena.

13Halafu wabinti zao watafurahi na kucheza,

vijana na wazee watashangilia kwa furaha.

Nitageuza maombolezo yao kuwa furaha,

nitawafariji na kuwapa furaha pahali pa huzuni.

14Nitawashibisha makuhani kwa nyama wenye kunona,

watu wangu watatosheka kwa wema wangu.

–Ni ujumbe wa Yawe.

Huruma ya Mungu kwa Israeli

15Yawe anasema hivi:

Sauti imesikilika katika muji wa Rama,

maombolezo na kilio cha uchungu.

Rakeli anawalilia watoto wake,

wala hataki kufarijiwa kwa ajili yao,

maana wote hawako tena.

16Yawe anasema hivi:

Acha kulia,

panguza machozi yako,

maana utapata malipo kwa kazi yako.

–Ni ujumbe wa Yawe.–

Watoto wenu watarudi kutoka inchi ya waadui zenu.

17Kuna matumaini kwa siku zenu zinazokuja,

maana watoto wenu watarudia katika inchi yao.

–Ni ujumbe wa Yawe.

18Nimesikia Efuraimu akilalamika hivi:

Umeniazibu vikali,

maana nilikuwa kama mwana-ngombe asiyezoea nira.

Unigeuze nami nitakugeukia,

maana wewe ndiwe Yawe, Mungu wangu.

19Maana kisha kukuasi, niligeuka toka zambi zangu,

na kisha kufundishwa, nilijilaumu,

nikapata haya na kufezeheka,

maana nilibeba haya za ujana wangu.

20Efuraimu ni mwana wangu mupendwa;

yeye ni mutoto wangu ninayemupenda sana.

Ndiyo maana kila mara ninapomutisha,

ninaendelea kumukumbuka.

Moyo wangu unamwelekea kwa wema;

hakika nitamuhurumia.

–Ni ujumbe wa Yawe.

21Weka kitambulisho katika njia zako,

simika nguzo za kukuongoza,

ukumbuke vema ile njia kubwa,

barabara uliyopita ndani yake ukienda.

Ewe Israeli rudi,

rudi kwa nyumba katika miji yako.

22Utasitasita mpaka wakati gani,

ewe binti usiyekuwa mwaminifu?

Maana, mimi nimefanya kitu kipya katika dunia;

mwanamuke anamulinda mwanaume.

Baraka katika siku zinazokuja

23Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nitakapowafanikisha tena watu wa Israeli, wao watatangaza tena katika inchi ya Yuda na katika miji yake wakisema:

Yawe akubariki, ewe makao ya haki;

akubariki, ee mulima mutakatifu!

24Halafu watu wa Yuda na miji yake yote, walimaji na wachungaji wanaopitapita na makundi yao watakaa huko pamoja.

25Waliochoka nitawachangamusha, na waregevu nitawapa nguvu.

26Ndiyo maana mutu ataweza kusema hivi: Niliamuka nikatambua kwamba usingizi wangu ulinifalia sana.

27Siku zinakuja ambapo nitaijaza inchi ya Israeli na inchi ya Yuda watu na nyama kama vile mulimaji anavyopanda mbegu.

28Na kadiri nilivyokuwa mwangalifu kuwaongoa, kuwabomoa, kuwaangusha, kuwaharibu na kuwatesa, ndivyo nitakavyokuwa mwangalifu kwa kuwapanda na kuwajenga.

–Ni ujumbe wa Yawe.

29Siku hizo watu hawatasema tena:

Wazee walikula matunda mabichi ya mizabibu,

na meno ya watoto ndiyo yanaumizwa.

30Lakini kila mumoja atakufa kwa sababu ya zambi zake mwenyewe; ni yule tu atakayekula matunda mabichi ya mizabibu ndiye meno yake yataumizwa.

31Siku zinakuja ambapo nitafanya agano jipya na watu wa Israeli na watu wa Yuda.

32Agano hili halitakuwa kama lile nililofanya na babu zao nilipowatoa kwa mukono wangu kutoka Misri; agano hilo walilivunja, ingawa mimi nilikuwa Bwana wao.

33Kisha siku hizo, nitafanya agano hili na Waisraeli. Nitaiweka sheria yangu ndani yao, na kuiandika katika mioyo yao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.

34Wala hawatafundishana tena kila mutu na jirani yake, na kila mutu na ndugu yake na kusema “Mumujue Yawe”, kwa sababu wote, wadogo kama vile wakubwa, watanijua mimi Mungu. Maana nitawasamehe makosa yao, wala sitazikumbuka tena zambi zao.

35Yawe, yule aliyepanga jua liangaze muchana, mwezi na nyota viangaze usiku, na anayevumisha mawimbi ndani ya bahari, yule ambaye jina lake ni Yawe wa majeshi, anasema hivi:

36Ikiwa itanifikia kuvunja mipango ile, halafu nitaweza vilevile kukomesha kizazi cha Waisraeli, wasiitwe tena taifa langu siku zote.

–Ni ujumbe wa Yawe.

37Yawe anasema hivi: Kama mbingu zinaweza kupimwa, na misingi ya dunia kuchunguzwa, basi, nitawatupilia wazao wa Israeli, kwa sababu ya mambo yote waliyotenda.

38Siku zinakuja ambapo muji huu wa Yerusalema utajengwa upya kwa ajili ya Yawe, kutokea kwenye munara wa Hananeli mpaka kwenye mulango wa Pembe.

39Nayo kamba ya kupima itanyooshwa moja kwa moja mpaka kwenye mulima Garebu, kisha itazungushwa mpaka Goa.

40Bonde lote walimozikwa wafu na kutupiwa majivu, mashamba yote, mpaka kijito cha Kidroni, mpaka pembe ya mulango wa Farasi kuelekea upande wa mashariki, litakuwa eneo takatifu kwa Yawe. Hakuna kitakachoharibiwa humo wala kubomolewa tena milele.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help