1Wakati ule, Hezekia aligonjwa sana karibu kufa. Halafu nabii Isaya, mwana wa Amozi akamwendea, akamwambia: “Yawe amesema hivi: ‘Panga mambo yako sawasawa katika nyumba yako kwa sababu utakufa, hautapona.’ ”
2Hezekia akageukia upande wa ukuta na kumwomba Yawe, akisema:
3“Ee Yawe, ninakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote na kutenda mazuri mbele yako.” Hezekia akalia kwa uchungu sana.
4Lakini mbele Isaya hajapita kiwanja cha katikati, Yawe akamutolea ujumbe kusema:
5“Rudi umwambie Hezekia, mukubwa wa watu wa Yawe, na kumwambia: Mimi, Yawe, Mungu wa babu yako Daudi, nimesikia ombi lako na nimeona machozi yako. Nitakuponyesha na nyuma ya siku tatu utaenda katika nyumba ya Yawe.
6Nitakuongezea miaka kumi na mitano ya kuishi. Nitakuokoa wewe pamoja na muji huu toka katika mikono ya mufalme wa Asuria. Nitaulinda muji huu kwa ajili ya heshima yangu mimi na kwa ajili ya mutumishi wangu Daudi.”
7Basi Isaya akasema: “Mulete mukate wa tini halafu muutwae na kuuweka kwenye jipu lake, kusudi apate kupona.”
8Hezekia akamwuliza Isaya: “Ni kitambulisho gani ambacho kitanionyesha kwamba kweli Yawe ataniponyesha na katika siku ya tatu nitaweza kwenda kwa nyumba ya Yawe?”
9Isaya akamujibu: “Hiki kitakuwa kitambulisho kwako kutoka kwa Yawe, kwamba Yawe atafanya kama alivyoahidi: Unataka kivuli kiende hatua kumi mbele au nyuma?”
10Hezekia akamujibu: “Ni vyepesi zaidi kivuli kwenda mbele hatua kumi! Basi kirudi nyuma hatua kumi.”
11Isaya akamwomba Yawe, naye Yawe akafanya kivuli kirudi hatua kumi kwenye ngazi iliyojengwa na Ahazi.
Wajumbe kutoka Babeli(Isa 39.1-8)12Wakati ule, mufalme Berodaki-Baladana mwana wa Baladani mufalme wa Babeli alisikia kwamba Hezekia alikuwa amegonjwa na sasa amepona, alimutumia ujumbe pamoja na zawadi.
13Basi, Hezekia akawakaribisha na kuwaonyesha mali yake: nyumba yake ya hazina, feza, zahabu, viungo vya kukolezea chakula, mafuta ya bei kali na nyumba ya vifaa vyake vyote vya kiaskari na vitu vyote vilivyokuwa katika akiba zake. Hakukukuwa kitu chochote katika nyumba yake, au inchi yake ambacho hakuwaonyesha.
14Halafu nabii Isaya akamwendea mufalme Hezekia na kumwuliza: “Watu hawa wamesema nini? Na, wamekujia kutoka wapi?”
Naye Hezekia akamujibu: “Wamenifikia kutoka inchi ya mbali.”
15Halafu akamwuliza: “Wameona nini katika nyumba yako?”
Hezekia akamujibu: “Wameona yote yanayokuwa katika nyumba yangu. Hakuna kitu chochote katika akiba zangu ambacho sikuwaonyesha.”
16Halafu Isaya akamwambia Hezekia: “Sikia neno la Yawe:
17Siku zinakuja ambapo vyote vinavyokuwa katika nyumba yako na vitu vyote babu zako walivyokusanya mpaka leo, vitapelekwa Babeli. Hakuna kitu chochote kitakachobaki. –Ni Yawe anayesema hivyo.–
18Tena wamoja kati ya watoto wako wanaume watapelekwa, nao watakuwa matowashi katika nyumba ya mufalme wa Babeli.”
19Naye Hezekia akamwambia Isaya: “Neno la Yawe ulilosema ni zuri.” Alisema hivyo maana alifikiri: “Kutakuwa amani na salama muda wote wa maisha yangu.”
Mwisho wa utawala wa Hezekia(2 Sik 32.32-33)20Matendo mengine ya Hezekia, ushujaa wake na maelezo juu ya jinsi alivyojenga kisima na kuchimba mufereji wa kuleta maji katika muji, yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.
21Hezekia akakufa, naye mwana wake Manase akatawala kwa pahali pake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.