1 Mambo ya Siku 9 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Watu waliorudi toka katika utumwa

1Hivi, Waisraeli wote walihesabiwa kufuatana na vizazi vyao na kuandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli.

Watu wa Yuda wamepelekwa katika utumwa mpaka Babeli kwa sababu ya kutokuwa waaminifu.

2Watu wa kwanza kurudia katika miji ya inchi yao walikuwa Waisraeli wa kawaida, makuhani, Walawi na watumishi wa hekalu. wa upande wa mashariki. Zamani, walikuwa walinzi wa viingilio vya makambi ya Walawi.

19Salumu mwana wa Kore mwana wa Ebiasafu, pamoja na wandugu zake wa ukoo wa Kora, walikuwa na kazi ya kutunza viingilio vya hema la mukutano, kama vile babu zake walivyokuwa wakati wa ulinzi wa kambi ya Yawe.

20Finehasi mwana wa Eleazari, alikuwa musimamizi wao, zamani, Yawe alikuwa pamoja naye.

21Zekaria mwana wa Meselemia, alikuwa vilevile mulinzi wa viingilio vya hema la mukutano.

22Kwa jumla, watu mia mbili na kumi na wawili walichaguliwa kuwa walinzi wa viingilio vya hekalu. Waliandikwa kulingana na vijiji walimoishi. Mufalme Daudi na nabii Samweli ndio waliowaweka kwa kazi zao kwa sababu ya uaminifu wao.

23Basi, watu hao na wazao wao, waliendelea kulinda milango ya nyumba ya Yawe.

24Kila upande, ni kusema mashariki, magaribi, kaskazini na kusini, kulikuwa mulango uliokuwa na walinzi.

25Walinzi hawa walisaidiwa na wandugu zao waliokuwa wakiishi katika vijiji, ambao walilazimishwa kushika zamu ya ulinzi kwa muda wa siku saba, mara kwa mara,

26kwa maana wale walinzi wakubwa wane, ambao walikuwa Walawi, walikuwa na kazi ya kusimamia vyumba na hazina ya nyumba ya Mungu.

27Wao waliishi karibu na nyumba ya Mungu kwa sababu ilikuwa ni kazi yao kulinda na kufungua milango yake kila siku asubui.

28Walawi wengine walisimamia vyombo vilivyotumika wakati wa ibada. Walihitajika kuvihesabu wakati vilipotolewa na wakati viliporudishwa.

29Wengine walichaguliwa kusimamia vifaa vya hekalu, na vyombo vyote vitakatifu, na unga safi, divai, mafuta ya mizeituni, ubani na marasi.

30Lakini kazi ya kuchanga marasi ilifanywa na makuhani.

31Metitia, mumoja wa Walawi aliyekuwa muzaliwa wa kwanza wa Salumu, wa ukoo wa Kora, alisimamia utengenezaji wa sadaka ya mikate nyembamba.

32Nao wandugu zao wengine wa ukoo wa Kohati walikuwa na kazi ya kutayarisha mikate iliyotolewa kwa Mungu kila siku ya Sabato.

33Jamaa zingine za Walawi zilisimamia kazi ya nyimbo katika hekalu. Waliishi katika vyumba vimoja vya majengo ya nyumba ya Mungu na hawakuhitajika kufanya kazi ingine yoyote kwa maana walikuwa wakitumika usiku na muchana.

Babu na wazao wa mufalme Saulo(8.29-38)

34Watu wote hawa waliotajwa walikuwa viongozi wa kabila la Walawi, kulingana na ukoo zao. Wao ndio viongozi walioishi Yerusalema.

35Yeieli alikuwa babu ya wakaaji wa muji wa Gibeoni ambamo aliishi yeye pamoja na muke wake aliyeitwa Maka.

36Muzaliwa wake wa kwanza aliitwa Abudoni, naye alifuatiwa na Zuri, Kisi, Bali, Neri, Nadabu,

37Gedori, Ahio, Zekaria na Mikloti.

38Mikiloti alizaa Simeamu. Wazao wao waliishi Yerusalema karibu na jamaa zingine za ukoo zao.

39Neri alizaa Kisi, naye Kisi alizaa Saulo. Saulo alikuwa na wana wane: Yonatani, Malikisua, Abinadabu na Esibali.

40Yonatani alizaa Meribu-Bali, Meribu-Bali alizaa Mika.

41Mika alikuwa na wana wane: Pitoni, Meleki, Tarea na Ahazi.

42Ahazi alizaa Yara, Yara alizaa Alemeti, Azimaweti na Zimuri, naye Zimuri alizaa Moza,

43Moza alizaa Binea, Binea alizaa Refaya, Refaya alizaa Eleasa, naye Eleasa alizaa Aseli.

44Aseli alikuwa na wana sita: Azirikamu, Bokeru, Isimaeli, Searia, Obadia na Hamani. Hawa wote walikuwa wana wa Aseli.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help