Zaburi 13 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kuomba musaada

1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.

2Mpaka wakati gani, ee Yawe,

utaendelea kunisahau?

Mpaka wakati gani utanificha uso wako?

3Mpaka wakati gani

nitakuwa na wasiwasi katika roho

na sikitiko katika moyo siku hata siku?

Mpaka wakati gani waadui zangu watanishinda?

4Uniangalie na kunijibu, ee Yawe, Mungu wangu.

Uyaangazie macho yangu, nisipatwe na usingizi wa kifo.

5Usiwaache waadui zangu waseme: “Tumemushinda huyu!”

Watesaji wangu wasifurahie kuanguka kwangu.

6Lakini mimi ninatumainia wema wako,

moyo wangu ufurahie wokovu wako.

Nitakuimbia wewe, ee Yawe,

kwa vyote ulivyonitendea!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help