Waroma 11 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mungu hakuwatupilia Waisraeli

1Basi ninauliza: Mungu amewatupilia watu wake? Hapana hata kidogo! Maana kwa ngambo yangu, mimi ni Mwisraeli wa uzao wa Abrahamu, toka kabila la Benjamina.

2Mungu hakuwakataa watu wake aliojichagulia tangu mbele. Munakumbuka Maandiko Matakatifu yanayosema juu ya mashitaki ya Elia mbele ya Mungu juu ya Waisraeli? Yeye alisema:

3“Bwana, wamewaua manabii wako na kubomoa mazabahu zako; nami nimebaki peke yangu, nao wanatafuta kuniua.”

4Lakini Mungu alimujibu namna gani? Alimwambia: “Nimejiwekea watu elfu saba waliokataa kupiga magoti mbele ya mungu Bali.”

5Ni hivi vilevile kwa wakati huu wa sasa kunabaki wamoja ambao Mungu alichagua kwa neema yake.

6Na ikiwa walichaguliwa kwa neema ya Mungu, si kufuatana na matendo. Ingekuwa vile, neema isingekuwa neema tena.

7Nini basi? Taifa la Waisraeli halikupata kile walichokitafuta. Ni wachache tu ambao Mungu aliwachagua ndio waliokipata. Lakini wengine waliobaki, walifanywa kuwa wagumu,

8kama vile ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Mungu ameifanya mioyo yao kuwa migumu, macho yao yasipate kuona na masikio yao yasipate kusikia, na ni hivi wanavyokuwa hata leo.”

9Daudi anasema vilevile:

“Karamu ziwageukie kama mitego ya kuwanasa,

waanguke na kuazibiwa.

10Macho yao yatiwe giza wasione,

na migongo yao ikunjame siku zote.”

11Basi ninauliza: Waisraeli wamejikwaa hata wakaanguka kabisa? Hapana hata kidogo! Lakini kutokana na kosa la Waisraeli, watu wa mataifa mengine wamepata kuokolewa, kusudi wayasikilie wivu.

12Kosa lao limeiletea dunia baraka nyingi, na upungufu wao umeleta baraka nyingi kwa watu wa mataifa mengi. Basi haitaleta baraka zaidi sana wakati Waisraeli wote watakapookoka?

Kuokolewa kwa mataifa mengine

13Sasa ninasema na ninyi watu wa mataifa mengine. Nami ninafurahia kazi yangu, kwa kuona nimetumwa kuwa muhubiri wa watu wa mataifa.

14Kwa sababu hii ninaweza kuwafanya watu wa taifa langu wawasikilie wivu, hata nipate kuwaokoa wamoja kati yao.

15Kwa maana ikiwa kukataliwa kwao na Mungu kumeleta upatanisho kati yake na dunia, basi si hakika kwamba kukubaliwa kwao na Mungu kutaleta uzima kwa wale waliokufa.

16Donge la kwanza la unga wenye kupondwa likitolewa kwa Mungu, mikate itakuwa yake vilevile. Na kama shina la muti likitolewa kwa Mungu, matawi yatakuwa yake vilevile.

17Matawi mamoja ya muzeituni uliopandwa yamekatwa, na chipukizi la muzeituni uliojiotesha katika pori umepandikizwa kwenye nafasi yao. Na sasa unafaidia vilevile utomvu unaotoka ndani ya shina la yule muzeituni uliopandwa.

18Basi musizarau yale matawi yaliyokatwa. Ninyi hamuna cha kujivunia, kwa maana si ninyi munaoshikilia shina, lakini ni shina linalowashikilia.

19Labda utaweza kuniambia: “Matawi yale yalikatwa kusudi mimi nipandikizwe kwenye nafasi yao.”

20Unasema ukweli. Yamekatwa kwa sababu yalikataa kuamini na wewe unasimama imara katika imani yako. Sasa usijivune, lakini uogope!

21Kwa maana ikiwa Mungu hakuachilia yale matawi ya asili kuendelea kukomaa, namna gani atakuachilia wewe?

22Basi ufikiri juu ya wema wa Mungu na ukali wake vilevile. Yeye ni mukali kwa wale walioanguka, lakini yeye ni mwema kwako, ikiwa utaendelea katika wema wake. Kama si vile, wewe vilevile utakatwa.

23Na kama Wayuda wasipoendelea kukataa kuamini, watapandikizwa kwenye nafasi ile walipokuwa mbele, kwa maana Mungu yuko na uwezo wa kuwapandikiza tena.

24Ninyi watu wa mataifa mengine ni kama tawi la muzeituni wa pori lililokatwa na kisha likapandikizwa ndani ya muzeituni uliopandwa, umbalimbali na kawaida. Wayuda ni kama muzeituni huu uliopandwa; na si neno gumu basi kwa Mungu kupandikiza tena matawi yaliyokatwa katika muti wao wenyewe.

Huruma ya Mungu kwa mataifa yote

25Wandugu zangu, sitaki mukose kujua siri hii, kusudi musijione kuwa wenye akili sana. Siri ile ni hii: Waisraeli wamoja wataendelea kuwa wagumu mpaka watu wa mataifa mengine kwa jumla watakapokuja kwa Mungu.

26Na halafu taifa lote la Israeli litaokolewa kama vile inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu:

“Mukombozi atatokea Sayuni,

atakomesha uovu kati ya wazao wa Yakobo.

27Na hili ndilo agano nitakalofanya nao,

wakati nitakapowasamehe zambi zao.”

28Wayuda wamegeuka waadui za Mungu kwa sababu ya kukataa Habari Njema, na jambo hilo limekuwa faida kwenu ninyi watu wa mataifa mengine. Lakini wao ni wapendwa wake kufuatana na vile wamechaguliwa naye, kwa njia ya babu zao.

29Kwa maana Mungu habadilishi mafikiri juu ya zawadi anazotoa, wala juu ya wale anaowachagua.

30Zamani ninyi mulimwasi Mungu, lakini sasa amewahurumia kutokana na uasi wa Wayuda.

31Ni hivi vilevile, kutokana na vile mulivyohurumiwa, sasa wao wanamwasi Mungu, kusudi wao vilevile wapate kuhurumiwa na Mungu.

32Maana Mungu amewafanya watu wote kama wafungwa kwa sababu ya kuasi kwao, kusudi awahurumie wote.

Ukubwa wa ajabu wa Mungu

33Utajiri wa Mungu, hekima na ufahamu wake ni vikubwa kupita kipimo! Hakuna anayeweza kuvumbua kusudi lake wala kuelewa mipango yake!

34Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema:

“Ni nani anayejua mafikiri ya Bwana?

Ni nani anayeweza kuwa mushauri wake?

35Ni nani anayeweza kumupa Mungu kitu kwanza,

kusudi naye apate kumurudishia?”

36Kwa maana vitu vyote vinatoka kwake, navyo viko kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Atukuzwe hata milele! Amina.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help