2 Wafalme 23 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mufalme Yosia anaondoa ibada za kipagani(2 Sik 34.3-7,29-33)

1Kisha mufalme akatuma wajumbe, nao wakamukusanyia viongozi wote wa Yuda na wa Yerusalema.

2Naye mufalme akaenda katika nyumba ya Yawe pamoja na watu wote wa Yuda na wakaaji wote wa Yerusalema, na makuhani pamoja na manabii, watu wote, wadogo kwa wakubwa. Basi, akawasomea maneno ya kitabu cha agano kilichopatikana katika nyumba ya Yawe.

3Halafu mufalme akasimama karibu na nguzo na kufanya agano mbele ya Yawe, kumufuata Yawe, kushika amri zake, maagizo na masharti yake kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, kutenda maneno yote ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hicho; nao watu wote wakaungana katika kufanya agano.

4Kisha Yosia akaamuru Kuhani Mukubwa Hilkia na makuhani wasaidizi wake na walinzi wa mulango watoe katika hekalu la Yawe vitu vilivyotengenezwa kwa ajili ya Bali, Ashera na kwa ajili ya jeshi la mbingu. Aliviteketeza inje ya Yerusalema katika bonde la Kidroni na kupeleka majivu yake kule Beteli.

5Kisha akawaondoa makuhani wote waliobarikiwa na wafalme wa Yuda kwa kufukiza ubani katika pahali pa kuabudia katika miji ya Yuda na kunzunguka Yerusalema, vilevile wale waliofukiza ubani kwa Bali, jua, mwezi, nyota na jeshi la mbingu katika nyumba ya Yawe.

6Naye aliondoa sanamu ya Ashera kutoka katika nyumba ya Yawe, inje ya Yerusalema, akaipeleka mpaka kwenye kijito cha Kidroni. Kule akaiteketeza na kuisaga mpaka ikakuwa mavumbi, nayo mavumbi yake akayatawanya juu ya makaburi ya watu.

7Alibomoa nyumba za makahaba zilizokuwa katika nyumba ya Yawe, pahali wanawake walifuma mapazia ya Ashera.

8Akakusanya makuhani wote kutoka miji ya Yuda na aliharibu pahali pa kuabudia makuhani walipofukiza ubani, kutoka Geba mpaka Beri-Seba. Akabomoa pahali pa kuabudia palipokuwa upande wa kushoto wa mulango wa muji kwenye milango iliyokuwa kwenye njia ya kuingilia kwenye mulango wa Yoshua mutawala wa muji.

9Makuhani hao hawakufikia mazabahu ya Yawe katika Yerusalema, lakini walikula mikate isiyotiwa chachu waliyopewa na makuhani wenzao.

10Mufalme Yosia aliharibu pahali pa kuabudia miungu ya uongo palipoitwa Tofeti katika bonde la wana wa Hinomu, kusudi mutu yeyote asimuteketeze mwana wake au binti yake kama sadaka kwa Moleki.

11Vilevile aliondoa farasi waliotengwa na wafalme wa Yuda kwa ajili ya kuabudu jua kwenye njia ya kuingia katika nyumba ya Yawe, karibu na chumba cha Natani-Meleki, kilichokuwa inje ya muji; naye alichoma kwa moto magari ya jua.

12Mazabahu ambayo wafalme wa Yuda walijenga juu ya paa kwenye chumba cha juu cha Ahazi, pamoja na mazabahu ambayo Manase alijenga katika viwanja viwili vya nyumba ya Yawe, aliyabomoa na kuyapondaponda, kisha alitupa mavumbi yake katika kijito cha Kidroni.

13Vilevile aliharibu pahali pa kuabudia palipokuwa upande wa mashariki ya Yerusalema na kuelekea upande wa mulima wa uharibifu, pahali mufalme wa Israeli alipopajenga kwa ajili ya Astaroti chukizo la Wasidoni, Kemosi chukizo la Moabu na vilevile kwa ajili ya Milkomu chukizo la Waamoni.

14Alivunja nguzo vipandevipande; vilevile alikatakata sanamu za Ashera, na pahali zilipokuwa zinasimama akapajaza mifupa ya watu.

15Zaidi ya hayo aliharibu kule Beteli pahali pa kuabudia palipojengwa na mufalme Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi. Aliharibu mazabahu hayo na kuvunja mawe yake vipandevipande, na kisha akaviponda mpaka vikakuwa mavumbi. Vilevile akachoma sanamu ya Ashera.

16Kisha Yosia alipogeuka akaona makaburi juu ya kilima. Aliagiza mifupa ifukuliwe kutoka makaburi na kuichoma juu ya mazabahu. Basi akachafua mazabahu sawasawa na neno la Yawe ambalo mutu wa Mungu alilitangaza, nabii ambaye alitabiri matukio haya.

17Halafu mufalme akauliza: “Munara ninaouona kule ni wa nini?”

Nao watu wa muji wakamujibu: “Ni kaburi la mutu wa Mungu ambaye alikuja kutoka Yuda na kutabiri mambo ambayo umeyafanya juu ya mazabahu pale Beteli.”

18Naye akaagiza: “Umwache pale, mutu yeyote asiondoe mifupa yake.” Kwa hiyo waliiacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya nabii aliyetoka Samaria.

19Katika kila muji wa Samaria mufalme Yosia aliharibu pahali pa kuabudia miungu ya uongo palipojengwa na wafalme wa Israeli, kwa kumutukana Yawe. Mazabahu hayo yote aliyaharibu kama vile alivyofanya kule Beteli.

20Aliwaua makuhani wote wa miungu ya uongo juu ya mazabahu ambapo walitumikia na kuchoma mifupa yao juu ya mazabahu hayo. Kisha akarudi Yerusalema.

Yosia anasherehekea Pasaka(2 Sik 35.1-19)

21Kisha mufalme akawaamuru watu wote, akisema: “Mumufanyie Yawe, Mungu wenu, Pasaka, kama ilivyoandikwa katika kitabu hiki cha agano.”

22Hakuna Pasaka iliyosherehekewa kama hii tangu wakati wa waamuzi waliowaongoza Waisraeli wala wakati wa wafalme wa Israeli au wa Yuda.

23Lakini, katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yosia, Pasaka ilisherehekewa kwa Yawe katika Yerusalema.

Mabadiliko mengine yaliyofanywa na Yosia

24Tena, kusudi mufalme Yosia atimize sheria zote zilizoandikwa katika kitabu Kuhani Mukubwa Hilkia alichokipata katika nyumba ya Yawe, aliondoa wachawi, watabiri, miungu, sanamu za miungu pamoja na vyombo vingine vilivyotumika kwa kuabudu miungu ya uongo kutoka inchi ya Yuda na kutoka Yerusalema.

25Mbele ya Yosia au nyuma yake hakuna mufalme yeyote aliyekuwa kama yeye, ambaye alimutumikia Yawe kwa moyo wake wote, kwa nguvu zake zote na kwa roho yake yote kulingana na Sheria ya Musa.

26Hata hivyo, Yawe hakuacha ukali wa kasirani yake nyingi, kwa sababu hasira yake iliwaka juu ya Yuda kwa ajili ya vitendo vya kukasirikisha, ambavyo Manase alifanya juu yake.

27Naye Yawe akasema: “Nitawafukuza watu wa Yuda kutoka mbele yangu kama vile nilivyofanya kwa watu wa Israeli. Nitaukataa muji wa Yerusalema ambao niliuchagua niliposema: ‘Jina langu litakuwa mule.’ ”

Mwisho wa utawala wa Yosia(2 Sik 35.20–36.1)

28Mambo mengine ya Yosia na yote aliyofanya yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.

29Wakati wa kutawala kwake, Neko mufalme wa Misri alikwenda mpaka kwenye muto Furati kwa kukutana na mufalme wa Asuria. Naye mufalme Yosia akaondoka kwa kupigana naye; lakini Neko mufalme wa Misri alipomwona akamwua kule Megido.

30Wakubwa wake wakaibeba maiti yake katika gari na kuirudisha Yerusalema walikomuzika katika kaburi lake mwenyewe. Kisha watu wa Yuda wakamuchukua Yoahazi mwana wa Yosia, wakamupakaa mafuta na kumuweka kuwa mufalme kwa pahali pa baba yake.

Mufalme Yoahazi wa Yuda(2 Sik 36.2-4)

31Yoahazi alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na tatu alipoanza kutawala, akatawala kwa miezi mitatu akiwa kule Yerusalema. Mama yake aliitwa Hamutali, binti ya Yeremia wa muji wa Libuna.

32Yoahazi alitenda maovu mbele ya Yawe kama yote babu zake waliyofanya.

33Kusudi asiendelee kutawala akiwa kule Yerusalema, Neko mufalme wa Misri alimufunga kule Ribla katika inchi ya Hamati, akawalipisha watu wa Yuda kodi ya kilo elfu tatu na mia ine za feza na kilo makumi tatu na ine za zahabu.

34Neko mufalme wa Misri akamuweka Eliakimu mwana wa mufalme Yosia kwa pahali pa baba yake Yosia, akabadilisha jina lake kuwa Yoyakimu. Lakini alimupeleka Yoahazi mbali. Naye akafika Misri na kukufia kule.

Mufalme Yoyakimu wa Yuda(2 Sik 36.5-8)

35Mufalme Yoyakimu akamupa Mufalme wa Misri feza na zahabu, lakini akailipisha inchi kodi kusudi aweze kutimiza mapenzi ya Mufalme wa Misri ya kupewa feza. Akawalipisha wanainchi feza na zahabu. Kila mumoja alitoa kufuatana na kiasi mufalme alichoamuru, naye akamupa Neko mufalme wa Misri.

36Yoyakimu alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na tano alipoanza kutawala, na akatawala akiwa Yerusalema kwa muda wa miaka kumi na mumoja. Jina la mama yake lilikuwa Zebuda binti wa Pedaya wa muji wa Ruma.

37Yoyakimu alitenda maovu mbele ya Yawe, kama vile yote babu zake waliyofanya.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help