1Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yoasi mwana wa Yoahazi katika inchi ya Israeli, Amazia mwana wa Yoasi mufalme wa Yuda akaanza kutawala.
2Alipoanza kutawala alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mitano, naye akatawala akiwa Yerusalema kwa muda wa miaka makumi mbili na tisa. Mama yake aliitwa Yoadani wa Yerusalema.
3Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe, lakini hakukuwa kama babu yake Daudi. Akafanya mambo yote kama vile baba yake Yoasi.
4Nafasi za kutambikia kwenye milima hazikuharibiwa na watu waliendelea kutambika na kufukiza ubani kwa nafasi zile.
5Wakati Amazia alipojiimarisha katika mamlaka, aliwaua watumishi waliomwua mufalme baba yake.
6Lakini hakuwaua watoto wa wauaji kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Sheria ya Musa, Yawe alipotoa amri akisema: “Wazazi hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto hawatauawa kwa ajili ya wazazi wao; lakini kila mutu atauawa kwa ajili ya zambi zake mwenyewe.”
7Amazia aliwaua Waedomu elfu kumi katika Bonde la Chumvi. Aliutwaa kwa nguvu muji wa Sela na kuuita Yokiteli, na hivi ndivyo unavyoitwa mpaka sasa.
8Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yoasi mwana wa Yoahazi, mujukuu wa Yehu, mufalme wa Israeli akisema: “Ukuje tupigane.”
9Lakini Yoasi mufalme wa Israeli akamupelekea Amazia mufalme wa Israeli ujumbe, akisema: “Siku moja muti wa mubaruti wa Lebanoni uliuambia muti wa mwerezi wa kule Lebanoni: ‘Umwoeshe binti yako kwa mwana wangu.’ Lakini nyama wa pori akapita pale na kuukanyagakanyaga mubaruti ule.
10Sasa, wewe Amazia umewashinda kabisa Waedomu, na moyo wako unakufanya ujivune. Ufurahie utukufu wako, ukae katika nyumba yako; kwa nini kujitafutia taabu zitakazokuangamiza wewe mwenyewe pamoja na watu wako wa Yuda?”
11Lakini Amazia hakujali. Kwa hiyo Yoasi mufalme wa Israeli akatoka akaonana uso kwa uso na Amazia kule katika vita Beti-Semesi, katika inchi ya Yuda.
12Watu wa Yuda walishindwa na watu wa Israeli na kila mumoja alirudi kwake.
13Yoasi mufalme wa Israeli alimuteka Amazia mufalme wa Yuda mwana wa Yoasi mwana wa Ahazia kule Beti-Semesi. Halafu akauendea Yerusalema na kuubomoa ukuta wake kutoka kwenye Mulango wa Efuraimu mpaka kwenye Mulango wa Pembeni, umbali wa karibu metre mia mbili.
14Alitwaa zahabu yote na feza, hata na vifaa vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Yawe na katika hazina ya nyumba ya kifalme. Vilevile alibeba mateka, kisha akarudi Samaria.
15Matendo mengine yote ya Yoasi, ushujaa wake na vita alivyopigana na mufalme Amazia wa Yuda yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.
16Yoasi akakufa, akazikwa katika makaburi ya kifalme kule Samaria. Mwana wake, Yeroboamu akatawala kwa pahali pake.
Kifo cha mufalme Amazia wa Yuda(2 Sik 25.25-28)17Amazia mwana wa Yoasi mufalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano nyuma ya kufa kwa mufalme Yehoasi wa Israeli mwana wa Yoahazi.
18Matendo mengine yote ya Amazia yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.
19Mupango wa kumwua Amazia ulifanyika Yerusalema. Kwa hiyo akakimbilia Lakisi, lakini waadui walituma watu wa kumwua kule.
20Maiti yake ililetwa juu ya farasi na kuzikwa katika makaburi ya kifalme katika Yerusalema katika muji wa Daudi.
21Kisha watu wote wa Yuda wakamukamata Azaria akiwa na umri wa miaka kumi na sita, wakamufanya kuwa mufalme kwa pahali pa Amazia baba yake.
22Nyuma ya kifo cha baba yake, Azaria akaujenga upya muji wa Elati na kuurudisha kwa Yuda.
Mufalme Yeroboamu wa pili wa Israeli23Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Amazia mwana wa Yoasi, mufalme wa Yuda, Yeroboamu mwana wa Yoasi, mufalme wa Israeli, akaanza kutawala akiwa kule Samaria, na akatawala kwa muda wa miaka makumi ine na mumoja.
24Alitenda maovu mbele ya Yawe; hakuacha zile zambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi.
25Aliikomboa inchi yote iliyokuwa mali ya Israeli, kutokea Pito la Hamati mpaka bahari ya Chumvi. Hivi ndivyo Yawe alivyoahidi kwa njia ya mutumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gati-Heferi.
26Ni kwa sababu Yawe aliona taabu kubwa Waisraeli waliyopata maana hakukuwa mutu yeyote wa kuwasaidia.
27Lakini Yawe hakukuwa amesema kwamba ataangamiza inchi ya Israeli kabisa, halafu akawaokoa kwa njia ya mufalme Yeroboamu mwana wa Yoasi.
28Mambo mengine ya Yeroboamu, yote aliyofanya, vita alivyopigana kwa ushujaa, na jinsi alivyoikomboa Damasiki na Hamati na kuifanya mali ya Israeli, yote yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.
29Yeroboamu akakufa na kuzikwa katika makaburi ya kifalme na mwana wake Zakaria akatawala kwa pahali pake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.