Zaburi 63 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Hamu ya kuwa pamoja na Mungu

1Zaburi ya Daudi wakati alipokuwa katika jangwa la Yudea.

2Ee Mungu,

wewe ni Mungu wangu.

Moyo wangu unakutafuta,

roho yangu inasikia kiu yako,

ninasikia kiu yako kama inchi inayokauka kwa ukosefu wa maji.

3Nina hamu ya kukuona katika pahali pako patakatifu,

nione nguvu yako na utukufu wako.

4Wema wako ni bora kuliko maisha.

Nitakusifu kwa midomo yangu.

5Nitakushukuru maisha yangu yote,

nitakuomba nikikuinulia mikono yangu.

6Roho yangu itafurahi kama mwenye kushiba minofu yenye mafuta,

kwa shangwe nitaimba sifa zako.

7Ninakukumbuka ninapokuwa katika kitanda,

ninafikiri juu yako usiku kucha,

8maana wewe umenisaidia siku zote.

Nitashangilia chini ya kivuli cha mabawa yako.

9Roho yangu inashikamana nawe kabisa;

unanilinda kwa mukono wako wa kuume.

10Lakini hao wanaokusudia kupoteza maisha yangu,

watatumbukia chini kwenye makao ya wafu.

11Watauawa kwa upanga,

maiti zao zikuwe chakula cha mbweha.

12Lakini mufalme atamufurahia Mungu;

nao wote wanaoapa kwa jina la Mungu watamusifu,

lakini vinywa vya waongo vitafungwa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help