1 Mambo ya Siku 25 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Waimbaji wa hekalu

1Mufalme Daudi na viongozi wa Walawi, wakachagua wazao wa Asafu, wa Hemani, na wa Yedutuni, kwa kuongoza katika kazi ya kutabiri kwa kutumia vinubi, na vinanda na matoazi. Haya ndiyo majina ya wale waliochaguliwa kwa kuongoza ibada, pamoja na aina ya kazi iliyofanywa na kila kikundi:

2Wana wa Asafu: Zakuri, Yosefu, Netania na Asarela. Hao walikuwa chini ya uongozi wa Asafu aliyetabiri wakati wote chini ya uongozi wa mufalme.

3Wana wa Yedutuni: Gedalia, Seri, Yesaya, Simei, Hasabia na Matitia. Wao walikuwa chini ya uongozi wa baba yao; na walitabiri kwa kutumia vinubi, na wakimushukuru na kumutukuza Yawe.

4Wana wa Hemani: Bukia, Matania, Usieli, Sebueli, Yeremoti, Hanania, Hanani, Eliyata, Gidalti, Romamuti-Ezeri, Yosibekasa, Maloti, Hotiri na Mahasioti.

5Mungu alimupatia Hemani aliyekuwa akitabiria mufalme, wana hawa kumi na wane, na wabinti watatu, kama vile alivyoahidi kwa kumutukuza.

6Wana wake wote walipiga muziki kwa matoazi, vinanda na vinubi, kwenye ibada katika nyumba ya Yawe wakiwa chini ya uongozi wa baba yao. Asafu, Yedutuni na Hemani walikuwa chini ya uongozi wa mufalme.

7Hesabu yao pamoja na wale wandugu zao Walawi waliofundishwa kumwimbia Yawe, wote waliokuwa wafundi, ilikuwa mia mbili na makumi nane na wanane.

8-31Wakapiga kura juu ya utaratibu wa kazi, kwa wakubwa kama vile kwa wadogo, kwa walimu kama vile kwa wanafunzi. Haya ndiyo majina ya wakubwa wa vikundi ambao kura iliwaangukia:

ya kwanza: Yosefu wa jamaa ya Asafu;

ya pili: Gedalia

ya tatu: Zakuri

ya ine: Isiri

ya tano: Netania

ya sita: Bukia

ya saba: Asarela

ya nane: Yesaya

ya kenda: Matania

ya kumi: Simei

ya kumi na moja: Azareli

ya kumi na mbili: Hasabia

ya kumi na tatu: Sebueli

ya kumi na ine: Matitia

ya kumi na tano: Yeremoti

ya kumi na sita: Hanania

ya kumi na saba: Yosibekasa

ya kumi na nane: Hanani

ya kumi na kenda: Maloti

ya makumi mbili: Eliyata

ya makumi mbili na moja: Hotiri

ya makumi mbili na mbili: Gidalti

ya makumi mbili na tatu: Mahasioti

ya makumi mbili na ine: Romamuti-Ezeri

Kila mukubwa pamoja na watu wengine wa jamaa yake walikuwa kikundi kimoja cha watu kumi na wawili.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help