1Mufalme Daudi na viongozi wa Walawi, wakachagua wazao wa Asafu, wa Hemani, na wa Yedutuni, kwa kuongoza katika kazi ya kutabiri kwa kutumia vinubi, na vinanda na matoazi. Haya ndiyo majina ya wale waliochaguliwa kwa kuongoza ibada, pamoja na aina ya kazi iliyofanywa na kila kikundi:
2Wana wa Asafu: Zakuri, Yosefu, Netania na Asarela. Hao walikuwa chini ya uongozi wa Asafu aliyetabiri wakati wote chini ya uongozi wa mufalme.
3Wana wa Yedutuni: Gedalia, Seri, Yesaya, Simei, Hasabia na Matitia. Wao walikuwa chini ya uongozi wa baba yao; na walitabiri kwa kutumia vinubi, na wakimushukuru na kumutukuza Yawe.
4Wana wa Hemani: Bukia, Matania, Usieli, Sebueli, Yeremoti, Hanania, Hanani, Eliyata, Gidalti, Romamuti-Ezeri, Yosibekasa, Maloti, Hotiri na Mahasioti.
5Mungu alimupatia Hemani aliyekuwa akitabiria mufalme, wana hawa kumi na wane, na wabinti watatu, kama vile alivyoahidi kwa kumutukuza.
6Wana wake wote walipiga muziki kwa matoazi, vinanda na vinubi, kwenye ibada katika nyumba ya Yawe wakiwa chini ya uongozi wa baba yao. Asafu, Yedutuni na Hemani walikuwa chini ya uongozi wa mufalme.
7Hesabu yao pamoja na wale wandugu zao Walawi waliofundishwa kumwimbia Yawe, wote waliokuwa wafundi, ilikuwa mia mbili na makumi nane na wanane.
8-31Wakapiga kura juu ya utaratibu wa kazi, kwa wakubwa kama vile kwa wadogo, kwa walimu kama vile kwa wanafunzi. Haya ndiyo majina ya wakubwa wa vikundi ambao kura iliwaangukia:
ya kwanza: Yosefu wa jamaa ya Asafu;
ya pili: Gedalia
ya tatu: Zakuri
ya ine: Isiri
ya tano: Netania
ya sita: Bukia
ya saba: Asarela
ya nane: Yesaya
ya kenda: Matania
ya kumi: Simei
ya kumi na moja: Azareli
ya kumi na mbili: Hasabia
ya kumi na tatu: Sebueli
ya kumi na ine: Matitia
ya kumi na tano: Yeremoti
ya kumi na sita: Hanania
ya kumi na saba: Yosibekasa
ya kumi na nane: Hanani
ya kumi na kenda: Maloti
ya makumi mbili: Eliyata
ya makumi mbili na moja: Hotiri
ya makumi mbili na mbili: Gidalti
ya makumi mbili na tatu: Mahasioti
ya makumi mbili na ine: Romamuti-Ezeri
Kila mukubwa pamoja na watu wengine wa jamaa yake walikuwa kikundi kimoja cha watu kumi na wawili.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.