Isaya 16 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Moabu inaomba musaada kutoka Yerusalema

1Mupeleke wana-kondoo kwa mutawala wa inchi,

mupeleke kutoka Sela katika jangwa mpaka kwenye mulima Sayuni.

2Kama ndege wanavyohangaika na kurukaruka,

wakiwa wamefukuzwa kutoka chicha zao,

ndivyo wabinti wa Moabu wanavyokuwa

kwenye vivuko vya Arnoni.

3Wamoabu wanawaambia watu wa Yuda:

Mutuongoze, mutuamue.

Mueneze ulinzi wenu juu yetu,

kama vile usiku unavyoeneza kivuli chake.

Mutufiche sisi wakimbizi;

musitutoe sisi tuliofukuzwa.

4Wakimbizi wa Moabu waishi kwenu,

mukuwe kimbilio lao mbali na mwangamizaji.

Mutesaji atakapokuwa ametoweka,

mateso yatakapokuwa yamekoma,

na wagandamizaji kutoweka katika inchi.

5Kisha utawala wa wema utazinduliwa katika hema ya Daudi.

Mutawala atakuwa mwaminifu.

Atahukumu kufuatana na sheria ya Mungu,

atakuwa mwepesi wa kutenda kwa haki.

6Watu wa Yuda wanasema hivi:

Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu,

tunajua jinsi alivyojivuna sana;

tumesikia juu ya majivuno, kiburi na mazarau yake;

lakini majivuno yake hayo ni bure.

7Sasa Wamoabu wanalia;

wote wanaomboleza juu ya inchi yao.

Muomboleze kwa ajili ya pigo hilo kubwa,

na juu ya maandazi ya zabibu za Kiri-Hareseti.

8Mashamba ya Hesiboni yamefifia,

vilevile na zabibu za Sibuma

ambazo ziliwalewesha wakubwa wa mataifa.

Zikafika Yaweri na kusambaa hata katika jangwa,

chipukizi zake zikafika hata ngambo ya bahari.

9Kwa hiyo ninalia pamoja na Yaweri

kwa ajili ya mizabibu ya Sibuma.

Machozi yananitoka kwa ajili yenu,

enyi miji ya Hesiboni na Eleale;

maana vigelegele vya mavuno ya matunda na ya ngano vimetoweka.

10Furaha na shangwe zimetoweka katika shamba lenyi mavuno mengi.

Kwenye mizabibu hakuna kuimba tena,

wala kupiga vigelegele.

Hakuna tena kukamua zabibu ndani ya vikamulio,

sauti za furaha za mavuno zimekomeshwa.

11Hivyo, nafsi yangu inalilia Moabu kama kinubi,

na moyo wangu kwa ajili ya muji wa Kiri-Heresi.

Mungu atawaangamiza Wafilistini

12Watu wa Moabu wanapojitokeza kuabudu mungu wao,

wanapojichokesha huko juu pahali pa ibada,

wanapokwenda pahali pao patakatifu kwa kuomba, hawatakubaliwa.

13Hili ndilo jambo Yawe alilosema wakati uliopita juu ya Moabu.

14Lakini sasa Yawe anasema hivi: Nyuma ya miaka mitatu kamili, ikihesabiwa kama vile mutumishi anavyohesabu siku zake, utukufu wa Moabu utapunguka. Ingawa watu wake ni wengi, watakaobaki wazima watakuwa wachache na wazaifu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help