1Zaburi ya Daudi.
Usikie maombi yangu, ee Yawe!
Ulitegee ombi langu sikio, maana wewe ni mwaminifu;
unijibu kwa sababu ya haki yako.
2Usinitie katika hukumu mimi mutumishi wako,
maana hakuna yeyote anayekuwa mwenye haki mbele yako.
3Waadui zangu wamenifuatilia,
wameniangusha chini kabisa,
wameniikalisha katika giza kama mutu aliyekufa zamani.
4Roho yangu imeregea kabisa;
moyo wangu unaugua.
5Ninakumbuka siku za zamani,
ninafikiri juu ya yote uliyotenda,
ninawazawaza matendo yako.
6Ninakunyooshea mikono yangu.
Ninakuhitaji wewe,
kama inchi kavu inavyohitaji mvua.
7Ee Yawe, unijibu haraka;
maana roho yangu imeregea kabisa!
Usinigeuzie mugongo,
kusudi nisikuwe kama wale wanaoshuka katika shimo la wafu.
8Kila asubui unionyeshe wema wako,
maana ninakutumainia.
Unifundishe mwenendo wa kufuata,
maana ninakutolea moyo wangu.
9Uniokoe, ee Yawe, kutoka waadui zangu,
maana ninakimbilia kwako.
10Unifundishe kutimiza mapenzi yako,
maana wewe ni Mungu wangu!
Roho wako muzuri aniongoze katika njia sawa.
11Ulinde uzima wangu, ee Yawe, kwa ajili ya jina lako,
uniondoe katika taabu, kwa ajili ya haki yako.
12Kwa ajili ya wema wako uwakomeshe waadui zangu,
uwaangamize wote wanaonitesa,
maana mimi ni mutumishi wako.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.