1Nasi vilevile tunazungukwa na kundi kubwa kama lile la wale walioshuhudia imani yao. Basi tutupilie mbali vitu vyote vinavyotusonga, nazo zambi zinazotufunga upesi na tukimbie kwa juhudi sana katika mashindano tunayowekewa.
2Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.
3Kwa hiyo mumukumbuke yule aliyevumilia kutendewa na wenye zambi kwa chuki kubwa, kusudi musipate kuchoka wala kuregea.
4Kwa maana katika vita munayofanya kwa kushinda zambi, hamujapigana bado mpaka kufa.
5Na zaidi ya hii, mumesahau maonyo haya Mungu anayotoa kwenu kama wana wake?
“Mwana wangu, usizarau azabu ya Bwana
wala usiregee wakati anapokukaripia.
6Kwa maana, Bwana anamwazibu yule anayemupenda,
yeye anamupiga kila mutu anayemukubali kuwa mutu wake.”
7Muvumilie maadibisho; kwa maana Mungu anawatendea ninyi kama wana wake. Tena, ni mwana gani asiyeazibiwa na baba yake?
8Ikiwa hamuadibishwi na Mungu sawa vile watoto wake wote wanavyoadibishwa, basi ninyi si wana wa kweli wa Mungu, ninyi ni wana haramu.
9Na ikiwa wababa zetu wa kimwili walituadibisha, nasi tuliwaheshimu, jambo hilo halionyeshi zaidi kwamba tunapaswa kumuheshimu Baba yetu wa kiroho na kupata kuishi?
10Wababa zetu wa kimwili walituadibisha kwa siku chache kufuatana na vile walivyoona kuwa vema. Lakini Mungu anatuadibisha kwa mafaa yetu kusudi tupate kushirikiana naye katika utakatifu wake.
11Maadibisho yoyote wakati yanapotolewa yanaonekana kama ni tendo la huzuni wala si la furaha. Lakini kwa mwisho yanawaletea wale waliofundishwa nayo, maisha ya amani na ya haki.
Maagizo na maonyo12Basi muitie tena nguvu mikono yenu inayopooza, nayo magoti yenu yanayoregea.
13Mujitengenezee njia zenye kunyooka, kusudi mwenye ulema wa miguu asiteguke, lakini apate kupona.
14Mujikaze kwa kuishi katika amani na watu wote na kuishi katika utakatifu, kwa sababu hakuna mutu asiyeishi katika hali hiyo atakayemwona Bwana.
15Muangalie vizuri, kusudi hata mutu mumoja asijikoseshe mwenyewe kupata neema ya Mungu, wala asikuwe sawa shina la mumea unaotoa matunda machungu na kuleta fujo kati yenu na kuambukiza watu wengi.
16Vilevile muangalie vizuri, kusudi hata mutu mumoja asikuwe mwasherati au mwenye kukufuru Mungu kama vile Esau aliyeuzisha haki yake ya muzaliwa wa kwanza kwa ajili ya chakula kidogo tu.
17Kama munavyojua, nyuma ya pale alikataliwa wakati alipotaka kupokea baraka toka kwa baba yake. Yeye hakukuwa tena na namna ya kugeuza tendo lake ijapokuwa alitafuta baraka ile kwa machozi.
18Ninyi hamujafikia kwenye kitu kinachoweza kuguswa kama vile Waisraeli walivyofikia kwenye mulima Sinai. Mulima ule uliwaka moto, ulifunikwa na giza nzito, nao ulikuwa na uvumi wa zoruba juu yake.
19Vilevile juu yake kulisikilika mulio wa baragumu na ngurumo ya sauti. Nao Waisraeli waliposikia sauti ile wakasihi wasiambiwe tena neno,
20kwa sababu hawakuweza kuvumilia agizo walilotolewa: “Hata nyama akigusa mulima anapaswa kuuawa kwa kutupiwa mawe.”
21Na mambo yale yaliyoonekana yalikuwa ya kuogopesha sana, hata Musa akasema: “Ninaogopa na kutetemeka!”
22Lakini ninyi mumefikia kwenye mulima Sayuni na kwenye muji wa Mungu Mwenye Uzima, ndio muji Yerusalema wa mbinguni, kunakokuwa maelfu na maelfu ya wamalaika.
23Lakini ninyi mumefikia kwenye mukutano wa furaha wa wazaliwa wa kwanza wa Mungu walioandikwa majina zao katika mbingu. Mumefikia vilevile karibu na Mungu, anayekuwa mwamuzi wa watu wote na kwenye nafsi kunapokuwa roho za watu wenye haki waliofanywa kuwa wakamilifu.
24Mumefikia karibu na Yesu anayekuwa mupatanishi wa agano jipya, na kwenye damu yake iliyomwangwa inayosema nasi maneno mema zaidi kuliko damu ya Abeli.
25Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni?
26Katika wakati ule sauti yake ilitetemesha dunia, lakini sasa ametuahidi hivi: “Nitatetemesha dunia mara moja tena, wala si dunia tu, lakini mbingu vilevile.”
27Neno hili “mara moja tena” linaonyesha kwamba vitu vilivyoumbwa vitatikiswa na kutoweka, kusudi vile visivyoweza kutikiswa vipate kudumu.
28Basi kwa kuwa tunakubaliwa kuwa washiriki wa ufalme usioweza kutikiswa, tukuwe watu wenye shukrani. Tuonyeshe shukrani ile kwa kumwabudu Mungu kwa njia inayomupendeza kwa heshima na woga,
29kwa maana Mungu wetu ni kama moto wenye kuteketeza.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.