Kumbukumbu la Sheria 13 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1“Kila kitu ambacho nimewaamuru, mufanye angalisho mukitende; musiongeze kitu wala musipunguze kitu.

2“Kukitokea nabii au mutabiri wa kutumia ndoto kati yenu na kuwapatia kitambulisho au ajabu fulani,

3kisha neno, vitambulisho au maajabu aliyowaambia yakitokea, na akisema: ‘Tufuate miungu mingine, miungu ambayo hamujapata kuijua, na tuitumikie’,

4musisikilize maneno ya nabii huyo au mutabiri wa kutumia ndoto, kwa maana Yawe, Mungu wenu, anawatumia kwa kuwajaribu kusudi ajue kama munamupenda yeye Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wenu wote na roho yenu yote.

5Mufuate na kumwogopa Yawe, Mungu wenu, na kushika amri zake na kutii sauti yake. Mumutumikie na kuambatana naye.

6Lakini nabii huyo au mutabiri wa kutumia ndoto atauawa, kwa sababu atakuwa amewafundisha uasi mbele ya Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa katika inchi ya Misri na kuwakomboa kutoka katika utumwa, kusudi muache njia ambayo Yawe, Mungu wenu, aliwaamuru kufuata. Hivi ndivyo mutakavyokomesha uovu kati yenu.

7“Ikiwa ndugu yako wa tumbo moja, au mwana wako, au binti wako, au muke wako unayemupenda sana au rafiki yako mupenzi, atakushawishi kwa siri akisema: ‘Twende tuabudu miungu mingine’, ambayo wewe wala babu zenu hamwijui,

8miungu ya watu wanaoishi karibu nanyi au miungu ya watu wanaoishi mbali tokea incha moja ya dunia mpaka incha nyingine,

9usikubali kushawishiwa wala kumusikiliza, au kumuhurumia wala usimwachilie wala usimufiche;

10lakini utamwua. Mukono wako unapaswa ukuwe wa kwanza wakati wa kumwua halafu wengine wote watafuata vilevile.

11Umupige mawe mpaka akufe, kwa sababu amejaribu kukuvuta mbali kutoka kwa Yawe, Mungu wako, ambaye alikutoa toka utumwa katika inchi ya Misri.

12Hivyo, Waisraeli wote watasikia na kuogopa, na hawatafanya uovu kama huo hata kidogo.

13“Mutakapoishi katika miji ambayo Yawe, Mungu wenu anawapa, labda mutasikia

14kwamba watu fulani wa ovyo ovyo kati yenu, wamewashawishi watu wa muji wakisema: ‘Twende tuabudu miungu mingine’, ambayo bado hamukujua,

15basi mutapeleleza na kufanya uchunguzi na kuuliza kwa uangalifu. Na kama ni kweli kwamba jambo la kuchukiza limetendeka kati yenu,

16hakika mutawaua kwa upanga watu wa muji huo. Mutauteketeza kwa upanga kabisa na ngombe wote vilevile.

17Mutakusanya vitu vyote mulivyoteka katika kiwanja cha muji na kuchoma kwa moto vitu vile vyote kama vile sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Yawe, Mungu wenu. Muji huo utakuwa lundo la mabomoko milele, nao hautajengwa tena.

18Kitu ambacho kimekwisha kutolewa kiteketezwe musikitwae, kusudi Yawe aache ile hasira yake mbaya. Yawe, Mungu wenu, atawaonyesha rehema na kuwafanya ninyi mukuwe wengi sana kama vile alivyoahidia babu zenu,

19kama tu mutatii sauti yake, mukishika amri zake zote ambazo ninawapa hivi leo na kufanya kile kinachokuwa sawa mbele yake.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help